Tamthilia ya kijiba cha moyo iliandikwa na Timothy M.Arege ambaye ni mwandishi mtajika wa lugha na fasihi ya kiswahili. Timothy ni mhadhiri katika chuo kikuu katoliki cha Afrika mashariki nchini Kenya.
Timothy aliandika tamthilia nyingine zikiwemo chamchela, Mstahiki meya na nyinginezo.
Utangulizi.
“Moyo hupenda, moyo huchukia, moyo hukinai, moyo huhurumia, lakini moyo unapopatwa na dhiki ni rahisi kujua unaponzwa na nini.”
Tamthilia ya kijiba cha moyo ni tamthilia inayoangazia maisha ya Sele kudhaniwa kuwa mgonjwa, kunyimwa haki zake, na kutotetewa kwa namna yeyote anapopambana na waiotaka kuiba moyo wake halafu akabaki na kijiba.
Sele ni kijana ambaye amebadilika kitabia katika familia, moyo wake umepatwa na kutu, familia yake imekosa kupata utulivu kwa kughasiwa na ugonjwa wake. Sele kila tendo analiona kuwa ni uonevu , sele ana kijiba cha moyo. Je mawaidha ya bibi yatautibu ugonjwa wa Sele?
Dhamira ya mwandishi..
Timothy ananuia kutuonyesha uongozi wa kiimla
uliotapakaa katika nchi nyingi za bara la Afrika na kukita mizizi pale.
Tamthilia hii ni miongoni mwa kazi za kifasihi zinazo chunguza uhusiano uliopo baina ya ubepari wa
mataifa na hali duni ya kiuchumi iliyojiri mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa mtindo wa
kinaya. Mwandishi anatalii maudhui ya kiuchumi na mfumo wa kibepari ambao licha ya
kuwakandamiza wakazi wa mabara ya Afrika unapunguza nafsi za wafanyikazi na
kuwafanya kujihisi kuwa duni. Mahusiano haya yameendelezwa kwenye misingi ya
udhalimu.
Mwandishi ameelezea maonevu haya kwa kinaya akitumia sitiari pevu ili kukejeli mfumo mzima wa uelewaji wa dhana ya uhuru katika uzalishaji mali.
Katika tamthilia hii mwandishi pia analenga kutuonyesha kuwa uongozi uliopata mashiko yake kwenye mfumo wa kibepari, umemiliki nyenzo za kimsingi za uzalishaji mali kupitia kwa ufisadi, uongo na zaidi katika kuwakandamiza wale waliopata mwangaza wa kuona njama hii ya kunyanyaswa. Hili hutekelezwa ili kuzuia juhudi za wale waliopata mwamko mpya
kisiasa dhidi ya kuwazindua wanyonge wengine katika jamii. Mwandishi kupitia kwa
mhusika nguli (Sele), anasawiri uhusiano uliopo baina ya mataifa ya ulimwengu wa
kwanza ambayo huyapa misaada na kuyamiliki mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa
kuyafanya yakose kujitegemea. Mwandishi anasawiri kwa kina misaada inayotolewa kwa
mataifa machanga na kuonyesha kuwa misaada hii haiwafai Waafrika ila tu ni chombo
kinachotumiwa ili kuweza kupata fursa ya kuwanyonya Waafrika rasilimali zao. Hii ni
kinaya kwa kuwa Waafrika wenyewe hawaelewi hali hii.
Arege analenga kutuonyesha kuwa hali ya uhitaji katika mataifa mengi ya bara la Afrika
imesababishwa na unyonyaji wa nguvu za wakazi wake kwa malipo duni. Anaeleza kuwa
mipango ya kuyasukuma mbele kimaendeleo mataifa machanga barani Afrika ambayo
inaamuliwa na kuwekwa na mataifa yanayodai kujitegemea ni chanzo cha kudorora kwa
maendeleo yanayotarajiwa. Hii inatokana na ukweli kwamba walioshikilia (wakoloni)
nguzo za mfumo huu wa kibepari waliwafumba macho wakazi wa nchi changa kwa
kuwapa misaada isiyowafaa.
Falsafa ya mwandishi.
Mwandishi ameongozwa na falsafa ya “UJinga ni Ugonjwa“Nchi zenye nguvu zinatumia aina zote za kutoa misaada ili kumiliki rasilimali za mataifa aina ya tatu juu ya ujinga na kutoelewa kinachofaa kufanywa. Hili linachorwa vizuri na mhusika sele alipojitoa kupigania haki wengine wakafikiri ni mgonjwa(ujinga).
Mtazamo wa mwandishi.
Mwandishi ameegemea Mtazamo wa kisiasa yaani kiyakinifu; Kuungana, kujitahidi na kujikomboa kimawazo ni suala liwezalo kusaidia waafrika
kujiendeleza kwa misingi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hiki kinabainika baada ya
kutamatisha kusoma tamthilia hii ambapo inabainika kuwa ugonjwa wa Sele si
ule wa kawaida kama ulivyochukuliwa na wahusika tamthiliani bali kuzinduka kutokana na mwamko mpya wa kisiasa na kijamii.
Msimamo wa mwandishi. katika tamthilia ya kijiba cha moyo mwandishi anamsimamo wa kimapinduzi kwani amejadili matatizo yanayochangia kukwama kwa ujenzi wa jamii mpya. Msimamo wake umebainishwa kutokana na jinsi alivyochora mhusika Sele, akijaribu kujiokoa na kujikomboa kimawazo wengine wakifikiri ni mgonjwa lakini akakosa kupata washabiki werevu. (kijiba)
Wahusika katika tamthilia ya kijiba cha moyo.
Wahusika ni viumbe wa kisanaa wanaopatikana katika kazi ya fasihi na wenye sifa za
kibinadamu. Aghalabu huwa na sifa za kimaadili, kitabia, kiitikadi, kifalsafa ambazo
hutambulishwa na wanayoyasema (mazungumzo) na wanayoyatenda (matendo),
Wamitila (2002).
1.Sele- mumewe Aisha na mtotowe Musa na Zainabu. Sele kulingana na tamthilia ana sifa zifuatazo;
. Ni mdadisi: katika Kijiba cha Moyo tunaweza kusema Sele ni
mdadisi kutokana na tabia yake ya kuuliza maswali mengi. Alimdadisi daktari
alipokwenda hospitalini pia tunajuzwa kuwa Sele alimuuliza daktari
maswali mengi alipokuja kwao kumtibu. Kwa mfano:
Sele: Naelewa lakini nipe nafasi kuuliza swali
kabla ya kuanza.
Daktari: (Hana stahamala tena.) Sitaki maswali yako
mengi. Siku ile nyingine umeniuliza maswali
mengi ya kunipotezea muda. Mimi ndiye
daktari; nakuuliza maswali wajibu. (Kimya)
wewe ni wa kujibu, Sasa wewe unataka
kunihoji . Hili tendo linadhihirisha udadisi wa mhusika Sele.
Sele, Ni mwenye kughasiwa na ugonjwa wa moyo.
Sele ni mgonjwa kutokana na mavazi ya wagonjwa aliyovaa na daktari si mgonjwa bali ni
daktari kwa sababu amevaa sare za kazi na glovu tayari kutibu wagonjwa.(uk 52)
.Ni mwenye huruma. Tendo la Sele la kukataa kuwala vidagaaa, linamsawiri kama
mhusika mwenye huruma. Sifa hii imedhihirika kupitia mazungumzo ya Zainabu na
Bi. Rahma(uk 15-16) Sele anakwepa kula vidagaa, kwa kuwa anawaonea
huruma kwa kuliwa na papa naye awale.
. Ni mtetezi wa wanyonge. Sele anaonekana kama mtetezi wa wanyonge. Kwa kusema „vinavyoliwa huku
vinatazama‟ inamaanisha vidagaa ni wanyonge hawawezi kujitetea. Hivyo basi
anapinga tendo la papa la kuwala vidagaa; kwa kutokula vidagaa yeye mwenyewe.
. Ni mwenye kutoridhika. Tendo la Sele katika tamthilia ya Kijiba cha Moyo la kutaka kufanyiwa „plastic
surgery‟ linadhihirisha sifa yake ya kutoridhishwa na maumbile yake na nia yake ya
kutaka kuyabadili. Hili limedhihirika katika kurasa 31-36. Hali hii ya Sele
inawakilisha mataifa ya Kiafrika yasiyoridhishwa na hali zao na kutaka kuiga mataifa
ya ng‟ambo.
. Ni mwenye hasira. Sele amesawiriwa kama mwenye hasira na
asiyependa kusumbuliwa. Haya yamedhihirika kupitia namna anavyoongea kwa
ukali kama ifuatavyo:
Sele: (Kwa sauti ya juu.) Wewe umejua kama
mimi sitaki mtu kunisumbua halafu unanijia
kwa fujo. Dharau tu! (uk.33)
.Ni mwenye kujichukia. Sele anavyochukia maumbile yake. Hivyo
kumfanya kujichukia. Chuki hii ndiyo chanzo cha ndwele yake na ndicho kijiba chake
cha moyo. Chuki hii ya Sele inaashiria jinsi mataifa yanayoendelea yanavyokosa
kujithamini.(uk33-34)
.Ni mwenye sura ya kupendeza.
Sele kama kijana mwenye sura
ya kupendeza yenye pua laini iliyochongeka vizuri na midomo mikubwa. Vilevile ana
mataga na weusi uliokoza na kukolea. (Uk 43)
.Ni mkaidi. Tunamuona Sele anakaidi mashauri ya jamaa zake na pia anakaidi kumeza dawa kwamba yeye si mgonjwa.
2. Aisha-mkewe Sele.
.Ni mwenye kupenda raha. Hili linadhihirishwa pale alimomwambia mumewe kwamba waende kujistarehe (uk 03)
.Ni mwenye mapenzi na kumjali mume wake. Hili linadhirika anapoingia chumba walimo wazee wake na kuwapuuza akienda mbio kutafuta vitabu kuvisoma ili aelewe ugonjwa wa mume wake ili aweze kumsaidia.(uk20)
.Ni msomi. Amesawiriwa kama msomi. Sifa hii inadhihirika kupitia tabia
yake ya kusomasoma vitabu. Hili linadhihirika kupitia mazungumzo baina ya Aisha,
Zainabu na Bi. Rahma(uk18)
.Ni mwenye heshima. Heshima ya Aisha inadhihirika pale anapowheshimu wazee wake kwa kutowaita majina.
3.Zainabu-mamake Sele na mkewe Musa.
.Ni mwenye kumjali mwanawe Sele. Zaiabu tunamuona anatembea juu chini akimtafutia dawa la kumtibu. Tena mwenye hamu kusikiliza muuguzi Jamila wakati alipokuwa anamtibu kwake nyumbani (uk88)
.Ni mvumilivu kwani tunamuona katika tamthilia nzima anavumilia na ugonjwa wa mtotowe hata ingawa alimtusi wakati mwingine.
.Ni mwenye matumaini kuwa mtoto wake atapona ugonjwa wa moyo.
4.Jamila-Bintiye Hassan. Ni msomi. Jamila anadhihirika kama msomi na kupitia maelezo yake
tunaweza hatimaye kuufahamu ugonjwa wa Sele.(uk90)
.Ni muuguzi Aliyemuugua sele.
.Alisoma na Sele . Hili linathibitishwa kwenye (uk88) wakati zinabu na Bi:Ramhma walipokuwa wanamgojea Jamila na Bi Rahma akasema “watu waliosoma pamoja hawakosi kupatana”
5.Daktari.
.Ni mkatili kwani tunamuona katika tamthilia ndiye aliongoza waliomtembelea sele na kumpekuapekua alipokuwa amelala. Pia alimkataa kuuliza maswali kuhusu ugonwa wake Sele.
.Ni msomi kwani ni daktari kiutaalamu.
6.Amri-Babu yake Sele.
.Ni mwenye mapenzi hasa wa Sele juu ya ugonjwa wake.
7.Musa-Babake Sele.
Hajali kuhusu ugonjwa wa sele.
Maudhui katika tamthilia ya kijiba cha moyo.
Maudhui katika kazi ya fasihi ni jumla ya mawazo yote yanayozungumzwa pamoja na mtazamo wa mwandishi juu ya mawazo hayo.
1. Ubepari. Ni mfumo wa kiuchumi unaowezesha watu wachache kumiliki rasilimali na njia kuu za uchumi wa nchi kwamfano Madaktari watatu waliomjia Sele wakati alipolala kitandani na kumpekuapekua hudhihirisha ubepari.
Mwandishi kupitia mhusika Sele anasawiri uhusiano uliopo baina ya mataifa ya ulimwengu wa kwanza (viongozi) ambayo huyapa mataifa ya ulimwengu wa tatu misaada isiyofaa kv matibabu ya Sele, ila tu ni chombo cha kupata fursa ya kugawanya rasilimali zao.
2. Ugonjwa/Magonjwa. Ni kuwa katika hali ya kusababishiwa hali mbaya kwamfano Sele anaoekana akivaa sare za wagonjwa na Daktari kavaa sare za udaktari maanake kuna mgonjwa na mtibu.
Pia tunamuona Sele ni mgonjwa wa moyo, Jamila anathibitisha kwenda kwake hospitalini anapotoka kumhudumia(uk 88)
Muuguzi jamila pia anaeleza kwamba ugonjwa wa sele haujafikia kiwango cha kutisha (uk89).
3. Elimu. Ni mfumo wa mafunzo yanayopatikana shuleni, vyuoni, au katika maisha.
Jamila ni msomi kwani ni muuguzi aliyemhudumia sele. Mazungmzo ya Zinabu na Bi Rahma kwamba Sele na Jamila walisoma pamoja unadhihirisha usomi wake.(uk 88)
4. Mapenzi. Ni hali ya kuingiwa moyoni kuthamini mtu au kitu zaidi ya mwingine au kingine.
Aisha anamoenda sana mumewe Sele ndiposa anaingia chumba walimo wazee wake na kuwaluuza akitafuta vitabu akikusudi kusoma ili aelewe ugonjwa wa Sele aweze kumsaidia(uk18)
5. Mabadiliko. Ni hali ya kubadilika kutoka hali moja kwenda hali nyingine.
Sele alibadilika baada ya kugundua kwamba anagandamizwa lakini wengine hawakumuelewa ili wamtolee msaada ya kujikomboa na kuwatetea wanyonge -mambo hayakufaulu.
7. Ukoloni. Ni hali unapokuta nchi moja inatawaliwa na nchi nyingiine.
Tendo la madaktari kumzungukazunguka na kumpekuapekua Sele mara wakishauriana na kumuashiria kisha kusema kwa pamoja “bado amelala” kinaashiria wakolni walivyokuja bara la Afrika wakachunguza rasilimali, na wakaona bado waafrika wamelaala na ndipo kuamua kutwaa rasilimali hizo. (Uk79)
8. Unyanyasaji. Ni hali ya kudharau mtu kwa kiburi au kwa kujiona bora dhidi yake.
Tendo la madaktari watatu kuja kumpekuapekua huku na kule mwili mzima ni ishara ya kudharau na kumnyanyasa.
Tena kunyimwa fursa ya kuuliza daktari na kutopewa habari kuhusu tests zake hospitalini ninishara ya kumnyanyasa kiakili.
9. Ukatili. Ni hali ya kutokuwa na huruma.
Ukatili unajitokeza pale daktari anapompiga dawa sele akiwa anajua sele si mgongwa ila tu kwa hamu ya kumyakua pesa zake.(uk52-53) “staki kupoteza muda, time is money bwana” ni ishara ya ukatili.
10.Utumwa. Ni mfumo unaotoa fursa kwa binadamu kumiliki binadamu mwingine kama mali yake.
Utumwa unadhihirika pale ambapo Sele ananyimwa fursa ya kupata matokea ya habari kuhusu “tests” zake hospitalini (uk60, 61)
11.Utabaka. Hi ni hali ya ubaguza wa kiuchumi, kisiasa na kijamii inayotenganisha watu wa hali duni na wale wa hadhi ya juu. Utabaka unadhihirika pale tunapoona Sele anahudumiwa lakini kwa ghari na akasema nipe “deposit yangu” (uk. )
12. Ndoa. Ni maafikiano rasmi baina ya mwanamke na mwanamume. Ndoa inashihirika kati ya Sele na Aisha pamoja Musa na Zainabu.
13. Uvuvi.
14. Ukosefu wa nidhamu.
Ukosefu wa nidhamu katika tamthilia ya kijiba cha moyo unaonyeshwa pale Aisha alipoingia chumba waliomo wazee wake na kuwapuuza baada ya kuwasalamia tu na akaingia kwenye chumba kingine akaaanza kutafuta vitabu vya kusoma iki aelewe ugonjwa wa sele. (Uk20)
Tamathali za Usemi katika tamthilia ya kijiba cha moyo.
Kazi ya fasihi, haihusiani na kuwasilisha mawazo tu, bali kuyawasilisha mawazo hayo
kisanaa. Habari au wazo fulani haliwezi kuelezwa au kuwasilishwa kwa wasomaji bila
kuzingatia hali ya kuwepo kwa usanii wowote. Mawasiliano yote ya kisanaa huhitaji
kuwasilishwa kwa mbinu za kimvuto, ile njia inayompa raha au ladha tamu msomaji
anapojaribu kuufuatilia ujumbe wa mwandishi wa kazi ya fasihi. Nakwahivy, zifuatazo ndizo baadhi ya tamathali za Usemi nilizoweza kuchambua katika tamthilia ya kijiba cha moyo;
1.Tashbihi ni tamathali ya usemi ambapo watu ama vitu viwili au zaidi hulinganishwa au
hufananishwa na watu ama vitu vingine.
Kwa mfano, Sele akielezea umahiri wake katika uogeleaji
anasema:
… Kisha nikapumzika juu ya mawimbi
kama gogo huku chini yangu maji yakipiga
na kutoa povu. (uk. 2)
“Na mimi nahisi kama sisi
tunayumbishwa mithili ya miti
msimu wa kipupwe… “(uk. 29)
“Linaweza kuwa dogo na athari
zake ziwe kubwa, kama tone la
mafuta ya taa kisimani- huhangaisha
mtaa mzima… “(uk. 50)
2. Tashihisi. ni tamathali ya kukipa kitu kisichokuwa
na uhai mkamilifu sifa za kitu chenye uhai kinachojitegemea katika mazingira yake.
Katika tamthilia ya Kijiba cha Moyo,
Sele anatuchorea taswira ya starehe ya bahari na uzoefu wake katika uogeleaji. Anaeleza:
“…Nikapiga mbizi. Nikapambana na Mawimbi chini kwa chini. Nikayapenya.
Nikataka nitokezee huko wanakokaa papa.
Nilipoibuka nilikuwa palee! Mbali huko.
Kisha nikapumzika juu ya mawimbi kama
gogo huku chini yangu maji yakipiga kutoa
povu. Mimi juu, papa chini. Siku hizo nilitaka
niwe bingwa wa dunia”. (uk. 2)
Mtindo huu pia unajitokeza katika maelezo ya Aisha kuonyesha namna ilivyomwia
vigumu katika kutambua ugonjwa anaougua Sele. Anaonyesha kuwa hali hii ni ngumu
anaposema:
“…Kama lililotiwa hamira, linafura
na kujaa fikirani. Kichwa kinakuwa
kizito kama nanga…” (uk. 20)
Jambo limepewa uwezo wa kufura na kujaa na pia kufanya kichwa kuwa kizito. Hii ni
tashhisi ambayo mwandishi ametumia ili kuonyesha namna mchanganyiko wa mawazo
ulimpata .
3.Methali ni kifungu cha maneno yanayotumiwa
pamoja kisanii, kwa njia ya kufumba na kupigia mfano jambo fulani.
Tamthilia ya Kijiba cha Moyo imetawaliwa na methali mbalimbali kwa nia ya mwandishi
ya kukuza ujumbe wake. Bi. Rahma analalamikia mapishi ya kisasa na kushuku kuwa
huenda ndiyo yanamkosesha Sele hamu ya chakula. Anamwambia Zainabu:
“… Watavilaje vyakula vya kuharakishwa?
Heri huvutwa kwa subira mama. Vyakula
visivyopata kutua sufuria, vipi vitatua
moyoni?” (uk. 14)
Methali anayoitumia Bi. Rahma ina maana kwamba kizazi cha kisasa hakina subira
katika kutekeleza majukumu hasa kimapishi.
Mwenye nguvu mpishe (uk 29)
Mchana watasema usiku watalala(uk 34)
Pole pole ndio mwendo (uk26)
Methali nyingine katika tamthilia ni “mhitaji zote ni mtumwa” (uk25).
Continue reading “MWONGOZO WA TAMTHILIA YA KIJIBA CHA MOYO-Timothy M Arege..”
