ALL TEACHERS ARE EQUALLY IMPORTANT MR PRESIDENT M7

*AN OPEN LETTER TO THE PRESIDENT OF UGANDA ON SALARY DISCRIMINATION IN PUBLIC SERVICE*

*By your Muzukulu*
*Peter Katusabe of* *Kagadi.*

First of all, ihave no credentials to say hello Shenkuru? Simply because i’m no body in government. I hold no special rank in UPDF, NRM or Local Government leadership, im simply an academician your excellency. Im simply an ordinary citizen born by a couple of economically vulnerable bafuruki immigrants in Ruteete Settlement scheme that hosts over 20000 former banyakigezi natives who were re settled in bunyoro in 1960s through the bilateral arrangement between Ngorogoza ( mukiga prime chief) and omukama Sir Winyi Tito Rukirabasaija of Bunyoro kitara in early 60s.

Mr president, my background as an imigrant descendant gave me courage to persue education to change the plight many of our ancestors faced when they turned down missionary education and opted to provide casual labor in tea plantations and construction sites. Many banyakigezi are scattered the whole country not because of their wish, but because their ancestors are everywhere as aresult of casual laborforce in factories and farm estates. A few lucky banyakigezi like Rugunda, Mbabazi, Mutebire, Nzeyi(RIP), Besigye, Mateke, Mulenga, Nuwagaba, Bahati, Nzeirwe, Bitature, keiwha, Kagonyera, the list is long your excellency, are a reflection of atrue banyakigezi generation that were able to obtain missionary education through good schools like Ntare, Butobore, immaculate heart, mbarara high, Nyakasura, Kyegobe, Mutorere among other powerful schools. The above gentlemen came from similar poor family backgrounds like me or even worse. What saved them was that the education sector by then was largely a government service and one’s head only stood for him or her.

Your excellency you remember your days in Ntare with my neighbor Matia Kasaija, your economic background never mattered but rather your level of intellect at Junior level. Junior education by then was purely in government hands and was an open space for every ugandan academically talented to showcase his capacity at the performance in the cambridge Junior exams. This is how the makerere university was then a centre of excellence for the country’s most cream.
With the coming of the beast of Washington codnamed *liberalisation* , Jaja you were misadvised by the imperialists whom you have for long opposed, to liberalise everything and let the market forces determine the future of every citizen.

Banks collapsed ,  you are aware KCB bank is the most successful foreign bank here mr president while UCB was swallowed by stanbic bank SA. Our Uganda railway corporation is in permanent hideout, our UTL is winding up, Our UTC transport company fell flat, everything was swallowed by imperialists and we got subjugated in 1995.

Your excellency,  I would address you on anumber of things,  but i am going to concentrate on your great love for Scientists against other proffessionals in the country

*THE COLLAPSE* *OFTHE ECONOMY* *OVER PERPETUAL* *SALARY DISPARITY**
Mr president,  as soon as you privatised,  the education sector was sold to imperialists.The intention of the brettonwoods institutions in New york is to create class strata where there is sharp class division between masters and servants. One class deprives the other of all its natural advantages and perpetually makes it its servant through the capitalist approach.

As soon as you left education to private sector,  mr president the other first cream group of banyakigezi vanished. They got divided in to two. The masters and the slaves. Im sorry to use banyakigezi because i found them very familiar to me, since im one of them.
Liberalisation meant that government would nolonger determine merit of talent but rather one’s economic and political status.Primary education was left to dogs as soon as UPE was introduced and investment per capita on every pupil stood at 3000 Ush per annum.( UPE capitation grant). This affected learning in UPE coupled with high teacher pupil ratio and high textbook pupil ratio. Twaweza research findings of 2016 indicated that only 10% of pupils in P6 could read the P4 class English passage.Eventually since 1997 todate,  UPE comfortably enjoys front position of pupils in failed grades and division four. UPE pupils rarely pass in division one and those who afford first grade in UPE like i did in 2003, are simply extra ordinary. Its of recent that a primary teacher started earning 400,000 monthly your excellency. We pay tribute to James Tweheyo’s spirited fight that saw 100℅ teacher salary enhancement.
Mr president, the poor pupils from UPE are immediately put aside of the sytem as the previous National merit schools like Ntare and Bweranyangi eliminate them through the cut throat competition where their lowest S1 entry grades are aggregate 4&5.
Your bazukulu from kyamate, Ruteete COU, mutunguru primary schools are shown red card never to enter the first world schools.
Those who enter first world govt schools like Buddo, Ntare, Mbarara high, SMACK,  Gayaza,  Nabisunsa,  St Henrys,  Uganda matyrs Namugongo are children of your cabinet ministers like Frank Tumwebaze, Robina Nabbanja,  Cris Baryomunsi, Jim Muwhezi, Haruna kasoro, Peter Ogwang etc. These are primarily educated at Homisdallen,  Flobetto,  Kampala parents, Good times infants etc where school fees per term is 2M UGX as same ministers approve for us the economically vulnerable kids 8000shs per year in UPE schools.

Eventually mr president,  your UPE bazukulu are dumped in 3rd world USE schools where learning never take place and the highly demotivated secondary teachers are ingaged in produce buying,  boda boda,  retail shops and rearing animals. Teaching in USE schools stand at 40℅ as 60℅ of time is never committed to learning. What happens at end of S4,  your UPE graduates who constitute 90℅ of OLevel pass with flying colors of F9 in maths, English,  chemistry, physics, biology and ICT. Mr president its on this level that politicians and technocrats get their children excell with agg 8, 9 and 10 in the other first class govt schools. These join S5 with PCB, PCM, BCM , PEM and at failure MEG.

Upon S6,  they advance to makerere, Kyambogo, Busitema, Gulu and Mbarara to persue medicine, Engneering, Computer science and Veterinary. These scholarships are funded by my poor mother in Ruteete who is taxed on every household item such as sugar, soap, airtime, petrol, clothes, everything. The money mr Rujuki collects from me and my villagemates is what pays school fees for doctor students at makerere. These are children of katumba wamala, Jacob Oulanya, Edward Sekandi, Bright Rwamirama, Keneth Omona, Richard Twodong the list is endless.

On the other hand mr president,  we your poor bazukulu from public schools are compelled to offer arts subjects like History, RE, Fine Art, Economics, Literature etc and our courses at University are SWASA, Development studies, Psychology, BBA, Arts with education etc.

Mr president, those who fail to get tax payers money at A level have introduced Students Loan scheme to borrow money from treasury and persue science courses(90℅) of the scheme and leave 10% to relevant arts courses.

Mr president,  as soon as the children of your ministers graduate, are absorbed in civil service as Doctors, Engneeers, agriculturalists and researchers. Their fathers in your cabinet find it shameful for their children to earn 720, 000 UGX  like i earn at the gombolola as a graduate Arts cadre officer and have instead convinced you to make their entry basic pay 2,500, 000UGX and classified their scale as U4science for justification of this impunity and capitalist symptom.

Consequently mr president, one officer like CDO at Gombolora is paid 600k monthly and is the focal person for sub county planning and cordination of all development plans and interventions like Emyooga , YLP, UWEP and parish model. The CDO is the clinical officer of rural transformation and has the onus of transforming the 68℅ households still battling abject poverty. All the huge investment plans in attaining vision 2040 are cordinated and implemented by the poorly remunerated social scientists at sub counties and parishes. Eventually they are not productive and not committed to their jobs but have rather adopted same style like secondary teachers i ealier mentioned who spend 60% on their errands and 40% teaching your poor bazukulu. The outcome of this type of education i have already analysed.

*LONG TERM EFFECT*

The long term effect mr president is that just as Karl max stated, capitalism breeds a system that eventually leads to its collapse. The notion that development will come from scientists alone is adisillusion, misguided and politically motivated egocentric mal advise given by the above rulers that get chance to reach you mr president. The duty to organise state development mr president is aresponsibility of planners and social scientists who research development policies and design their application. Unfortunately these are not engneers nor doctors. These are people who have mastered economics, history, geography and and public policy and can design development models like parish development model mr president.

As you are aware, the engines of implementation of the much anticipated parish model are parish chiefs mr president who by their background are arts students with public administration, Development studies or SWASA. I have not seen doctors and engneers being solicited to fill these vacancies at parish level mr president

Therefore mr president, owing to this very long discourse and practical analysis,  i call upon an establishment of an independent Salary review commission to address the issue of Salary disparity in civil service and harness wagebills in MDAs.

I would recommend a 30% difference between the two cadres of same rank. Assuming a veterinary doctor at Gombolora earns 3, 000, 000,UGX Community Development Officer who share same U4 scale should earn 2, 100,000 and this becomes standard yardstick in all sectors of public service.

This should also be proceeded with radical public service reform including abolishment of duplicate agencies and authorities as you earlier recommended to avoid heamorage of state resources in paying redundant human resource duplicating services in public service and local governments.

I equally recommend that science teachers only advance 30℅ disparity against their arts counterparts for practical allowance other than proffessional ridicule on arts teachers.

Thank you your excellency,  This is my humble opinion as your muzukulu who went through UPE, USE, Public University at Kyambogo on Govt scholarship,  qualified with a first class in Development Studies and is currently a junior cadre humbly serving at degree scale of U4L that attracts 720,000 against my coleague science cadres of U4sc whom you pay 2, 400, 000 monthly your excellency.

Surprisingly its me mr president  who cordinates their activities and ensure that your clarical call on poverty eradication is implemented as per your good vision for your bazukulu by 2040 where no muzukulu should be less than 1000USD per capita .

God bless you mr president, God bless your visionary leadership and God guide you in establishing an independent salary review commission.

Regards to you from your iron lady RDC Ruteraho Lilian of Kagadi,  Your friend Ndugu Mfashingabo, Mrs Adrin Tibaleka your strong revolutionary cadre and thank you for granting us Kagadi and Kakumiro Districts and appointing our daughter Robina as leader of govt business. The Kigumba Kabwoya Kyenjojo turmack is also fully completed and Mubende Kakumiro Kibaale Kagadi muhooro road is in excellent shape. We are only waiting your good finance minister to fund Muhorro Ndaiga 40km stretch and have our region a next hub of economic growth your excellency.

Im sorry where i have offended any scientist, my honest opinion is based on rural experience and hands on experience of what is taking place in implementing vision 2040 as guided by HE the president.

I would also feel proud if you allowed me your excellency to work with the talented brains at the Parish model National secretariat and make this excellent program an international benchmark upon which developing countries would come here and be assisted on application of this model in five years from today.

Ualimu nimechoka: vipi nitambulike

*Ualimu nimechoka*

*Vipi Nitambulike?*

Nashika kalamu yangu, yalo kitwani nandika
Kwenye huu ulimwengu, lini nije tambulika
Tena mujue jina langu, lisije sahaulika
Ni vipi Nitambulike, walimwengu munijue?

Ama ni hii siasa, ndio mutanitambua
Niishi kua anasa, ila mukinichagua
Bali marufu nakosa, Je vipi tanitambua?
Ni vipi Nitambulike, walimwengu munijue?

Na nikijita pasta, miujiza kuzitunga
Tena wana wa munguwe, mnifuate ja kupinga
La inahitaji bidii, hata kanisa kujenga
Ni vipi Nitambulike, walimwengu munijue

Nikiwa mkubwa Gaidi, Redioni tasikika
Taliban na Alikaidi, Alshabab Nitambulike
Bali mimi si Lokech, Mogadishu wanizike
Ni vipi Nitambulike, walimwengu munijue?

Muziki pia Jameni, umarufu upo sana
Ni muige Bobiwine, nikamfikie Akon
Ila sipendi usani, shabiki takosekana
Ni vipi Nitambulike, walimwengu munijue.

Ukomedia nishike, Ila mpamire nishinda.
Nimuige mariachi, Matusi kwa kike Sina.
Nimfate Madrat,  chiko njama tiyari.
Ni vipi nitambulike walimwengu munijue.

arigumaho810@gmail.com.

@ni hayo路‍♂️

Sikimbilie kulea

Sikimbilie kulea
Usinione mzazi,ukadhania rahisi
Hakika hino ni kazi,isiyo nao wepesi
Ukijaribu huwezi,ndugu utakwenda kasi
Jipe muda ndugu yangu,sikimbilie kulea.

Kulea kuna gharama,sio bwerere ni ghali
Kujituma ni lazima,changamoto kukabili
Kupo ndu yangu kukwama,sikufichi kiukweli
Jipe muda ndugu yangu,sikimbilie kulea.

Sikiliza kwa makini,nakuomba ufahamu
Kulea sio utani,tambua ni hali ngumu
Kulea ja u vitani,kujihami ni muhimu
Jipe muda ndugu yangu,sikimbilie kulea.

N’omba uwe na subira,usije ukasumbuka
Kulea kuwe ni bora,na kwepesi kwa hakika
Ukuwe mlezi bora,tena kwa kumakinika
Jipe muda ndugu yangu,sikimbilie kulea.

Namalizia kulonga,haya yatosha rafiki
Mbele mie sitasonga,ila jepushe na dhiki
Mapema anza jipanga,uipeke dhihaki
Jipe muda ndugu yangu,sikimbilie kulea

MWONGOZO WA MAUDHUI KATIKA TUNGO ZA MUYAKA BIN-HAJI.

 Utangulizi.

Muyaka bin Haji ni kiumbe wa kihistoria na msanii mkongwe katika historia ya usanii, miongoni mwa wasanii wa kabla ya karne ya ishirini. Muyaka alizaliwa mjini Mvita katika ukoo wa Myinyi Malindi, miongoni mwa koo kumi na mbili za Waswahili, na aliishi kati ya 1776-1840.

Kitabaka,Muyaka alikuwa mtu wa wastani. Katika uhai wake, Muyaka alikuwa na mwigiliano na watu wa jamii yake katika kila tabaka.. Alikuwa mcheshi na mpenda zaha , na alifanya utafiti na wengi miongoni mwa watawala wa Mombasa – Mbari ya Mazrui, na hata watu wa tabaka lake.

Muyaka alikuwa mfanyabiashara mashuhuri, ingawaje hakufanikiwa sana katika biashara yake..

Kazi hii ya biashara ilimpeleka katika sehemu mbalimbali za  za ulimwengu wa biashara kama vile Bara Hindi, Uarabuni, Bukini, Ngazija, Pembe na Unguja. Nyingi ya tungo zake zinasimulia maisha haya.

 Kazi nyingi za Muyaka hasa zilijitenga na masuala ya kidini moja kwa moja, maudhui ambayo yalikuwa yameutawala uwanja wa tungo za nyakati hizo, na kushughulikia maswala mbalimbali ya maisha ya jamii kwa ujumla. Hata hivyo, swala la dini hakulipiga teke, bali alifunua hapa na pale katika usanii wake.

Wasanii wengi wa ushairi wa kabla ya karne ya Ishirini walijikita katika maudhui ya kidini, na wote walifuata mtindo mmoja wa kuandika ushairi wao, hasa katika utangulizi ambapo ilikuwa ni kama miongoni mwa kunga za ushairi kuwa ni lazima msanii aanze kazi yake ya kwa kumtaja Mola na kutoa shukurani kwake, na baadaye amtaje Mtume Mohamed na kumsalia, pamoja na maswahaba wake.

Kinyume na haya yote, ushairi wa Muyaka haukufuata mtindo huo wa kidini aidha

katika utangulizi wala mwili wake. Kwa kiasi kikubwa Muyaka alifaulu kuutoa ushairi nje ya maudhui ya kidini na kuanza Kutalii katika masuala ya kilimwengu , walimwengu na ulimwengu wao.

 Muyaka anatumia mashairi yake kuisawiri na kutupa picha halisi ya jamii yake.

Haya yote yanajitokeza wazi katika dhamira ya mashairi yake na yote anayoyazungumzia kuhusu jamii yake husika. Tungo za Muyaka zinajitokeza kama kio halisi cha jamii yake kwakuwa zinagusia  na kuzungumzia masuala mengi yanayoikumba na kuikabili jamii yake.

UHUSIANO WA MAISHA YA BINADAMU NA TUNGO ZA MUYAKA.

  1.  MAPENZI NA NDOA

Mapenzi na maisha ya ndoa ni mambo ambayo Muyaka ameyapa uzito sana katika kazi yake. Hili ni dhihirisho kamili la maisha ya waswahili na binadamu kwa ujumla kwamba mtu hawezi kuishi pweke kama kisiwa. Katika mashairi yake Muyaka amelijadili suala la mapenzi kwa uzito huku akitia chuku katika umuhimu wa kuwa na mpenzi na mwisho kuishia katika ndoa kwa manufaa ya mtu binafsi na kwa jamii pia.  Mfano wa tungo zake anazozungumzia mapenzi ni kama vile,

“Siupati Usingizi” (Uk. 200), anasema:

Risala wangu basiri, leo napenda kutuma,

Enenda ndiwa huuri, Mwenye cheo na heshima,

Fika ukamuhubiri, haya takayokutuma,

Namuapia karima, siupati usingizi.

Wisapo mpa salamu, ndiwa asio mfano,

Mwema wa kutakalamu, fasihi yakwe maneno,

Ni mwema wa tabasamu, mchache wa matukano,

Hasa himuwaza neno, siupati usingizi.

Wisapo mkurubia ndiwa, mwema wa mangani,

Enda kwa kunyeyekea, upomoke maguuni,

Kisa umweleze pia, yangu yaliyo mwoyoni,

Mato yangu hayaoni, kwa kukosa usingizi.

Tungo zake nyingine zinazozungumzia mapenzi ni kama vile”Mahaba” (uk. 184)), “Kitambi changu” (uk. 174), “Kwamba Wajua Mapenzi” (uk.2-4), “Tusiambiane Uongo”(uk. 221), “Kuonana na wewe” (uk. 238), “Hilo Langu Ndilo Lako”  (uk. 254), “Siuwati mtondoo” (uk. 272) “Harusi ya Bwana Muyaka” (uk. 278), “Utavaa Nguo Gani” (uk. 280),

“Mahaba nusu Wakiya” (uk. 304), “Madanganyo ni Maovu” (uk. 304) na “Musiwate Kuonana” (uk. 314) miongoni mwa mengine.

Katika tungo hizi, Muyaka anaelezea mbinu za kumbembeleza msichana na kumnasa katika mapenzi. Anayafafanua mapenzi kwa undani na kuleza ni sifa zipi zinazofaa kujitokeza baina ya wapendanao ndipo mapenzi ya kweli yawepo. Anataja sifa za binti mzuri ambaye anastahili kuwa mrembo lakini mwenye heshima, asie na matukano na myenyekevu.

 Katika shairi lake la “Siupati Usingizi” (uk. 200) anamusifu mpenzi wake kuwa ni mwema wa tabasamu na hana matukano na ni mrembo wa kulinganishwa na njiwa. Muyaka anamuomba aliyemtuma afikapo kwa yule binti kabla ya kumpa risala ambembeleze binti yule kwa kunyenyekea na kupomoka miguuni.

Haya yalikusudiwa kumchora binti yule kama mtu wa maana na kumuonyesha jinsi mapenzi yake yanahitajika na jinsi anavyopendwa.

Muyaka aliisawiri jamii ya Waswahili kama iliyojaa mahaba na yenye kuwaheshimu wanawake.

Muyaka anasisitiza suala la uzuri wa kuoa na sifa za wakuolewa anaposema:

Oa, kwamba u muozi, uzoeleo kuowa

Oa, mato maolezi, na mboni ukikodowa

Oa, Maji maundazi, meupe kama maziwa

Oa, sizi ndizi ndowa, asokuoa ni yupi?

  • UKOSEFU WA UAMINIFU

Mara kadhaa,Muyaka alionekana akiulaani ukosefu wa uaminifu katika maisha ya ndoa na mapenzi. Haya ni baadhi ya mambo yanayovunja uhusiano mwema baina ya wachumba au hata mke na mume.

Katika shairi lake la “Kwamba hutaki Nambia” (uk. 322), anamuomba mkewe

ajitoe kimasomaso juu ya fikra na matamanio yake juu ya Muyaka badala ya kupigana chenga.

Katika “Anamkejeli Mtu” (uk. 310) anazungumza juu ya ujanja aliofanya bwana mwengine mpaka akamzini bibi ya mtu mwengine. Anasema:

Nipaziwe nipaziwe, khabari zako mwandani,

Nambiwe hivi nambiwe, simba kulala shakani,

Kunyakua kama mwewe, nyamangwa kumla ndani,

Firigisi na maini, ndivyo apendavyo simba.

Hii ni ishara tosha kwamba katika jamii yake Muyaka palikuwepo na changamoto ya ukosefu wa uaminifu baina ya wanandoa na uzinifu baina ya wanajamii.

Muyaka anaelezea jinsi ukosefu wa uaminifu na uzinifu unavyosababisha kuyumbayumba kwa ndoa na hata kuvunjika na jinsi ni dhambi kuzini na suala lililopingwa na dini ya Kiisilamu.

  •  ELIMU NA JAMII.

Wakati Muyaka, watu wa Mombasa walipenda sana watoto wao wasome hasa wakati huo wakifunzwa kusoma na kuandika ili waweze kupata maarifa. Kulikuwepo na shule za kufunza kusoma na kukariri Koran pamoja na mafunzo kuhusu kazi nyingine za dini ya Kiisilamu kama vile aina tofauti tofauti za Maulidi.

Zaidi ya hayo mafunzo yaliendelezwa katika vyuo vilivyopatikana katika miskiti na mafunzo yakitolewa na Wanachuoni ama waliokuwa na elimu ya masomo mbalimbali ya Kiisilamu.

Muyaka alifahamu kuwa jamii yoyote ile ilihitaji elimu na maarifa ili kufaulu.

Wakati mwengine, Muyaka alizungumzia mambo fulani fulani tofauti ya maisha kwa kunasihi, kufundisha au hata kuonya. Wakati mwingine pia alizifuata hisia za watu na kuzichemsha bongo zao katika maswali ya jamii yaliyo na ukinzani mkuu, kama vile katika “Kasa ni Halali?” (uk.312):

Nna tembe masiala, mno yamenikikisa,

Zamani nilipolala, wavyele waliniusa,

Huzundukana akila, mato yakipesa-pesa,

Wakauza, “Huyu K’asa, ni halali, haramu?”

Kwani sikupata jibu, kwa kuchelea makosa,

Vifunueni vitabu, nyote wasomi darasa!

Munipe njema jwabu, mpatela kufuasa,

Munambie “Huyu K’asa, ni halali, ni haramu!”

Muyaka alitumia tungo kama hizi kwa dhamira ya kuwafanya kuwachochea wanajamii na wasomi  wafikirie ili wapata maarifa na kuelimika maana kila jamii huhitaji watu wenye elimu ili ifanikiwe.

  •   UTABAKA.

Katika nyakati za Muyaka, Waarabu walikuwa na ufanisi mkubwa sana mjini Mombasa lakini ufanisi wao pamoja na utawala wa Wamazrui haukudumu milele.

Kwa hivyo waliokuwa juu baadaye waliporomoka na hatimaye wakayaonja maisha ya ulitima. Ingawaje kwa kawaida baada ya kupanda marafiki huwakimbilia na kuwakata urafiki lakini wao walioporomoka urafiki hukoma, lakini Muyaka hakufanya hivyo bali aliwafariji na kuwa nao karibu sana kama walivyokuwa pamoja wakati wa ufanisi wao. Mpomoko wa ufanisi wa Mombasa anauzumgumzia katika shairi

lake la la “Ulimwengu” (uk.153):

Ai, ulimwengu jivu, ujileo vumbivumbi,

Walifile waangavu,wali na wao ujimbi,

Vianga havia mbivu, viwili vya urofumbi,

Wale walimbika kambi, leo ndio walimbikwa.

Ndiyo hali ya dunia, huleta vyema na vimbi,

Ambaye yamtatia, maninga yakwe hufumba,

Usingizihupotea, kwa mawazo tumbitumbi,

Walo walimbika kambi, leo ndio walimbikwa.

Muyaka alieleza jinsi watu katika jamii huwa katika matabaka tofauti lakini si ajabu kumuona aliyekuwa katika tabaka la juu la wenye mali na fedha ameshushwa hadhi hadi tabaka la chini la masikini.  Jamii huwa na mabadiliko kila wakati na kuna  kipindi ambapo waliokuwa maskini hupanda ngazi na kuwa wenye mali nyingi na wale waliokuwa na mali kushuka ngazi na kuwa masikini.

 Katiaka shairi lake la “Ukiwa Wako” (uk.209), Muyaka anatueleza kuhusu kijana

mmoja alieponda fedha zake hadi kuwa maskini.  Kijana huyo alirejea kwa mamaye na kudai fedha au ajidunge kwa kisu ila mamaye anamkataa na kumzomea kwa jinsi alivyozipunja fedha zake na mwishowe anamtimua Anasema:

Ndipo mamae kawaza, pamwe na kuzingatia,

Fedha zako umezizosa na leo zimekwishia

Kisu sikukutaza twaa upate jitia

Mbele zangu nondokea wende na ukiwa wako

  •  UZALENDO NA VITA

Tungo nyingi za Muyaka alizoandika wakati wa ukoloni wa Waarabu wa Omani laini ya Sayyid Said mjini Mombasa yalijikita sana katika uzalendo na vita hasa kutokana na hali halisi ilivyokuwa nyakati hizo. Katika enzi hizi, Mombasa ilikuwa kama uwanja wa vita, mara kwa mara wenyeji walijikuta katika harakati hizo za kivita. Muyaka anaonyesha jinsi wenyeji walivyopambana na kuzikata nyororo za ukoloni na dhuluma, au hata kupinga juhudi za kutawaliwa.

Katika shairi lake la , “Vikija Mtaviweza” (Abdulaziz 1979:133-134) anasema:

Kongowea haitui, hamtaki kuituza,

Mshishile uadui, kutaka kuipinduza,

Ndipo ikashika kawi, kutaka wafanikize,

Vikija mtaviweza, au mwatakia mabo?

Watani upeketefu, wa mambo kuyageuza,

Gongwa ni mji dhaifu, naona ni mwina wa Chiza,

Hutatia watifu, wasione muwangaza,

Vikija mtaviweza, au mwatakia mambo?

Muyaka anataja pia vifaa na zana walizotumia katika vita kama vile: mata, mafumo, ngao, p’anga, p’anga-kule, vitara, msu, ngurumza na fimbo. Pia anataeleza palikuwepo na ngoma na michezo mahususi ya kuwafunza vijanajinsi ya kutumia zana za vita vizuri na suala la vita kwa ujumla.

Kwa mfano, Muyaka anataja ngoma ya kizungup’ia, ambao ulikuwa ni mchezo wa vita uliohitaji matumizi ya nguvu uliochezewa katika fukwe za bahari.Mashairi mengine yalikuwa ya kuwatia ari wenyeji wa pwani kwa ujumla dhidi ya uvamizi na ukandamizaji wa Waarabu kama vile “Mjenga Nyumba Halali” (uk.124), “Kafa Li Man Hadhara” (uk.133), “Mwatupa Shauri

Gani?” (uk.136), “Mwima wa Chiza” (uk.143), “Kongowea Ja Mvumo” (uk.146).

Wakati mwingi palizuka mzozo na vita baina ya watala wa makabila ya Mombasa wenyewe na Muyaka aliyaelezea haya katika baadhi ya tungo zake na kusimulia jinsi watawala wawili wapiganiapo uongozi wananchi hushindwa ni yupi wa kufuata. Anasema:

Kwa vuma mwamba wa iwe, baharini watokota.

Ni mngumi na chongowe, wamo wawili wateta.

Hatuyui mmoyawe, tutakaye mfuata,

Zimewatatia t’ata, watatuzi tatuani.

  •  USALITI.

Jamii ilikumbwa sana na changamoto ya usaliti katika vita vya ukombozi wa Mombasa. Wakati mwingi, usaliti katika vita na juhudi za ukombozi ni jambo la kutarajiwa. Mara nyingi, Muyaka aliukashifu usaliti dhidi ya uzalendo na harakati za kujiokoa na maadui, kwa stihizai.

Katika tungo nyingine, Muyaka aliwakashifu vizalia wa Mombasa waliokwenda Zanzibar kumpongeza Sultan baada ya kushindwa kwa Mombasa na Zazinzibar katika vita.

 Anasema, “Vyema Mungelikulaje” (uk.152)

Mlio mkila nyemi, kwa furaha na urembo,

Mvuatile ulimi, wala hamsemi jambo

Na kauli hazatami, zilokuene na umbo

Viwi mwaramba vyombo, vyema mgelikulaje?

Wala hamchi kwambiwa, mmejikaza masombo

Hulaje visivyoliwa, mkiendea makombo?

Na maneno mkitowa, kama wanwaji wa tembo

Viwi mwaramba vyombo, vyema mgelikulaje?

Hula mkishindilia, ili kujaza matumbo

Shehena mkipakia, kama shehena ya chombo

Hamuoneli viwaya, mumuonela mwajimbo

Viwi mwaramba vyombo, vyema mgelikulaje?

  •  UTAMADUNI

Muyaka katika tungo zake  alizungumzia sana kuhusu suala la utamaduni na mila. Aliusifu utamaduni wa watu wa pwani na mila alizoziona zina umuhimu sana katika jamii. Alisisitiza suala la wanajamii kujikita katika utamaduni na mila na kuepuka kupotoka kutokana na mtagusano baina yao na watu wa jamii nyinginezo. Tamaduni na mila hizi ni kama zifuatavyo:

i. Chakula

Chakula kikuu cha watu walioishi Mombasa wakati huo kilikuwa ni mseto wa  mchele na mtama uliopikwa na nazi,kwa kitoweo cha samaki, nyama au mbonga. Pia, inaonekana pia katika wakati wa Muyaka, jamii yake pia ilitumia ngano, matundana samli kama chakula pia.

 Katika ubeti mmoja wa shairi lake anaeleza  jinsi ngano ilitumika kama “chakula mbadala” hasa na watu wa tabaka la juu.

Anasema:

Ai ngano na samli, viliwa vyema khiyari,

Vitu viawavyo mabali, Renu na Baunagari,

Apo mwende akali, Mola humjaza kheri,

Ai ziwa na sukari! Itakapokukutana.

Katika  shairi la “Panda” Uk. 190. Anasema:

Panda nganu na mpunga afudhali ya viliwa

Panda wimbi na kimanga vipawa vya kupewa

Panda usitunde ch’anga, tauwa mbivu tauwa

Panda ni wakouluwa, panda darajani, panda!`

ii. Mavazi

Katika baadhi ya tungo zake Muyaka anataja mavazi ya wanaume Waswahili kuwa Kanzu, vazi lenye mikono mirefu na linafika miguuni lililotengenezwa na malighafi tofauti lakini jeupe lilivaliwa sana. Chini ya kanzu  nguo iliyojulikana kama kitambi ama kikoi kilivaliwa. Baada ya kanzu vazi jingine lililojulikana kama Kizibao liliibuka ambalo haikuwa lazima liwe na mikono mirefu na lilikuwa angavu.

Kitambaa kilichofungwa kiunoni kilitumika sana ili kuzuia Kanzu kumsumbua alioivaa wakati akifanya kazi na pia kitambaa hicho kilitumika kushikia silaha kama vile visu, upanga, majambia  na pembe za unga wa bunduki.

 Muyaka anasema “jifungetoni

masombo” kuwaomba wakaze vikoi vyao. Nao wanawake wengi wa uswahilini walivalia leso ama visutu vilivyotengenezwa kwa pamba.

Wanaweka waliokuwa maskini walivalia kaniki na leso zilizotengenzwa kwa pamba hafufu na ya bei rahisi. Pia walivalia mikufu, shanga na vipuli mbali mbali.

 Katika shairi lake la “Si Wanawake wa Huja(uk.172). Anasema:

Ukiwaona kwa mbali, kwa vikuku na viganja

Wamba ni wake wa kweli ukienda wakidhi haja

Kanan ni batili swiswi na wao mamoja,

Si wanawake wa huja yalla ni yale mavao.

iii. Usafiri

Wakati wa Muyaka usafiri ulijikita sana katika matumizi ya barabara kwa kutumia wanyama kama vile punda na farasi kama inavyojitokeza katika shairi la “Mfuga Punda” (uk. 206).

 Piapalikuwepo ule usafiri wa baharini uliotumia mitumbi na mashua hasa kwa minajili ya usafiribaina ya visiwa vilivyokuwa karibu. Pia, wanabiashara waliotoka mbali  kama vile India naUarabuni walitumia meli katika usafiri wao.

Muyaka anaeleza jinsi alivyosafiri kwa mashuakatika safari zake.

 Anasema:

Simba ndume na wambuji, sikizanitatongoa,

Naketele vitongoji, na safari za mashua,

Leo nakumbuka mbiji, ya kutweka na kutua,

Ai, pato na pewa, litako kukutana.

Katika utungo wake wa “Kimbinji Changu”, (uk 168). Anasema:

Nastahabu kimbiji, kidau changu cha kwanza.

Kingwawa mlejileji, k’welea haikupanza,

Na kufa Ngozoa – Maji, yali usiku wa iza,

Ndipo leo hakiwaza haangama kazeeka.

Kiwizo changu kiwizo nilipo hikioleza

Chalikuwa cha matezo nami kikinipumbaza

Hatusa nacho Ufunzo mawimbi kutoa kweza,

Ndipo leo hakiwaza haangama kazeeka.

  •  DINI, MILA NA DESTURI.

Wakati wa Muyaka palikuwa na mila na itikadi nyingi hasa zilizotumika kama sheria za kuongoza jamii. Mfano ni kuwa mwanamke hakuruhusiwa kwenda pamoja na mumewe kwenye sherehe za kijamii na pia alihitajika kumvalia mumewe nguo mpya wala si kutoka nayo kwenda kuwaringia watu wa nje.

Mila na desturi hizi zilisisitizwa sana kwa kuwa zililinda mienendo na umoja wa jamii.

Yeyote yule aliyetenda kinyume na mila na desturi hizi alichukuliwa kama aliyepotoka na hata alihitaji adhabu kama vile kupewa talaka kwa mwanamke yeyote yule aliyepatika akizini nje ya ndoa.

Katika utungo wa “Kitambi Changu” (uk 174). Muyaka anasema:

Kitambi changu cha gomba, nilichokupa hidaya

Kumbe hivi hujipanmba ukenda kuzinginya

sikujua kana kwamba kuwa yatakuwa haya

hivi sasa nivulie nipe kitambi changu

Katika uk.176 anaendelea kusema:

Kwamba sina kazi nacho mama t’ampelekea:

ndicho kitu apendacho atakwenda jivalia

kwako nimefanya kicho siwezi kukuatia

sikuatik’ono moja! kitoe kitambi changu.

Kando na mila na desturi, dini ilichukua nafasi kubwa sana katika jamii ya wakati huo.

Dini ambayo ilikuwa imekita miziz wakati huo ilikuwa dini ya Kiisilamu. Sheria na kanuni za kiisilamu zilisisitizwa sana katika kuyangalia maadili ya wanajamii.

Dini ilitumika katika kuonya na kuelimisha wanajamii kuhusu kila suala la kila siku.

Katiaka “Mke wa Risasi” (uk. 300) anamlaani mtu mwengine aliyemhaba na kumtaka mapenzi mke wa marehemu Risasi aliyekuwa katika eda.

Kulingana na imani ya Waislamu, mjane akiwa katika eda hatakikani kuolewa wala kujiingiza katika shuguli za mapenzi, lakini bwana huyu, alivunja sheria na kumtaka mapenzi mjane wa Risasi.

  •  MAGONJWA NA KIFO

Muyaka anazungumzia pia magonjwa yaliyoikumba jamii yake na dhiki inayo ambatanishwa na magonjwa hayo. Anaeleza jinsi mtu apatwapo na ugonjwa  matokeo hayatabiriki. Yanaweza kuwa raha au huzuni, kulingana na hali itakavyokuwa , ikiwa ndwele imeshindwa nguvu na afya au kinyume chake. Abdulaziz, (1979: 156, tanbihi ya 4) anasema:

Ai, mpewa na pato lipalo mtu kukuwa,

Angawa mwana mtoto wa kutishika kachewa,

Akiwa na upasito wa kutamani ukiwa,

Ai, ndwele na afuwa, itakapo kukutana

Pana tungo amabazo Muyaka aliziandika akiwa mgonjwa sana. Katika utungo wa “Aha” (uk.188). Anasema:

Aha! Sengambile, Aha! Ndwele yaniuma.

Aha! N’ambe, sina siha, muwili wangu mzima.

Aha! Kutoona raha, ndipo aha! nikasema.

Aha! Sambile kwa wema, nasema, kwa ndwele sii

Katika shairi la “K’ongowea yaugua” (uk.202).

K’ongowea yaugua kwa kite na uguzi,

Kwa mambo kuyaugeua, kugeua mageuza,

Rabi, Ngwaipa afua! Na kuiafu si kazi,

Kutanani wamaiza shauri jema mtende.

Muyaka anazungumzia pia suala la kifo na kulielezea kama jambo lisiloepukika na mwili wa mfu huwezi ukalindwa kutokana na funza. Katika shairi lake la “Kifo Kikimbizwa Funza”

(uk.172), anasema:

Kifo kikimbizwa funza chawekwa mahali gani

Sikifakie kifunza, ukakitia shimoni,

Ndanini kujiumiza, kujitia mashakani?

Wapeni mabaniani, mahali wafakiweka.

  1.  UCHUMI.

Uchumi wa Mombasa katika nusu ya karne ya kumi na tisa ulikuwa umeimarika sana na kupanuka. Baadhi ya vitega uchumi alivyovitajaMuyaka katika tungo zake ni kama vifuatavyo:

i. Kilimo

Kilimo ni mojawapo wa vitega uchumi viliyvokuwa muhimu sana katika uchumi wa Mombasa wakati huo na familia zote zilizojiweza kifedha zilikuwa na mashamba katika sehemu za bara zilizozunguka kisiwa cha Mombasa. Mashamba haya yalikuwa chanzo cha mapato kwa familia zilizomiliki mashamba haya.

 Walikuza mpunga, mahindi, wimbi, mihogo, nazi, machungwa, maembe, ndizi na mboga za aina tofauti tofauti.

Katika  tungo za Muyaka, anataja vyakula walivyopanda wakulima wa Mombasa wakati huo.

Katika utungo wake wa “Panda” (Uk.190). Anasema:

Panda nganu na mpunga, afudhali ya viliwa

Panda wimbi na kimanga, vipawa vya kupewa

Panda usitunde ch’anga, tauwa mbivu tauwa

Panda ni wakouluwa, panda darajani, panda!`

ii. Uvuvi

Uvuvi ulikuwa miongoni mwa vitega uchumi vikubwa na maarufu  na hulka ya Waswahili .

Samaki walikuwa rahisi kupatikana na kwa wingi na samaki  walitumika sana kama chakula.

iii. Ufugaji

Wanyama kama vile  ng’ombe, mbuzi, kondoo, kanga pia walifugwa ili kuwapa maziwa na nyama. Waswahili ila hawakuweza kufikisha kiwango walichohitaji kwa matumizi yao ya kila siku na waliagizia ziada kutoka bara. Pia wanyama kama vile punda na farasi walifugwa kwa minajili ya usafiri.

Katika utungo wake Muyaka “Mufuga Punda” (uk. 206), anasema:

Mfuga hufuga ng’ombe, k’ashika bubu k”akama

Na samli lembe-lembe k’iwa na haja k’atuma

Na nyama riade nitube niwe katika hishima

Mfuga-p’unda-kilema hukujambia mashuzi

Mfuga hufuga mbuzi myama mwenye madhihala

Ukawacha yako kazi na wala pasiwe na ila

Ukaenda katika zizi kumchinja na kumla

Mfuga-p’unda, madhila hukujambia mashuzi

iv. Utengenezaji wa mashua.

Lazima palikuwepo na maeneo ambapo palitengenezwa mashua lakini si viwanda vikubwa kama vile vilivyopatikana karibu na  Lamu. Vyombo vya baharini vilivyotengenezwa katika eneo hili vilikuwa vidogo vilivyotumika katika uvuvi na usafiri baina ya visiwa vilivyokuwa karibu.

v. Ufinyanzi.

Ufinyanzi uliendelezwa sana na watu wa kabila la Wajomvu na Muyaka anawarejelea kama

“Wafinyanga Vyungu”

vi. Uhunzi.

Wahunzi wakijulikana sana kama wafua-vyuma walikuwepo na walijihusisha na utengenezaji wa majembe, mashoka, visu, misumeno, pete na kulabu. Wafua-fedha  walitengeneza vitu kama vile mikufu kama vile shanga. Wabanyanas kutoka India.

vii. Mafundi wa ngozi.

Wapo waliojihusisha na utengenezaji ngozi ili kutengeneza ndala, ngao, mishipi na majalada ya vitabu.

viii. Ushonaji.

Jukumu hili liliachiwa wanawake walioshona  mavazi kama vile kofia, jokho na aina fulani ya k’anzu na mashati.

Palikuwepo pia na utengenezaji wa vikapu, makuti ua kuezeka paa, kamba, majamvia na nyavu za kushikia samaki. Katika utungo wake Muyaka, anasema : “Ukukuu wa kamaba si upya wa

ukambaa” (uk. 260)

  1.  BIASHARA.

Biashara ilikuwa moja wapo wa shughuli iliyokuwa muhimu zaidi baina ya Mombasa na watu wa bara. Misafara ya wafanyabiashara ilitoka Mombasa kwenda magharibi kupitia Taita, Maasai na kwenda mbali zaidi hadi kiwango cha kufika katika fukwe za ziwa la Victoria.

Kaskazini magharibi, wafanyabiashara hao walisafiri hadi kufika maeneo ya ziwa Baringo. Wafanyabiashara hao walinufaika na pembe za ndovu na faru, chumvi, mikeka, kamba na mifugo wakibadilishana na bidhaa zao kama vile shaba, shanga, chuma na nguo.

Mombasa ilikuwa na uhusiano wa moja kwa moja wa kibiashara baina ya Mombasa na India na biashara hii ilihusisha ubadilishanaji wa nguo na nafaka kutoka India na Pembe za ndovu pamoja na watumwa kutoka Afrika Mashariki.

Muyaka anaisuta india katika shairi lake anapokejeli kuwa ingawa India ndiko kunakotengenezwa nguo kunao wengi wanaotembea uchi.

Muyaka anasema “Hindi ndiko kwenye nguo na wendao uchi wako” (uk.160).

HITIMISHO.

Kutokana na kuwa Muyaka aliishi na kuweza kuingiliana na watu wa matabaka mbali mbali, maisha ya jamii kwa ujumla ndiyo maswala makuu yanayojitokeza katika tungo zake. Kama tulivyoona, mashairi ya Muyaka yanatumika kama chombo cha kusawiri na kuchora  jinsi jamii yake ilivyo kwa kuzingatia maswala mbali mbali ya jamii husika.

Maswala haya ni kama vile uhusiano wa watu mbali mbali, siasa, uchumi, yanajitokeza sana katika mengi ya mashairi yake.

Maswala haya yanamuwezesha Muyaka kuihusisha hadhira kikamilifu kwani yalikuwa ni mambo ya maisha yao ya kila siku.

Kupitia tungo zake Muyaka tunaweza kuelezea jamii yake ilivyokuwa kwa kuegememea katika jinsi anavyoisawiri jamii husika.

NAFASI YA KISWAHILI-UGANDA.

Swahili Basics and Useful Phrases for Travelers to East Africa
Ikiwa unapanga safari kwenda Afrika Mashariki, fikiria kujifunza maneno ya kiswahili ili kuweza kuzungumza na watu unaokutana nao kwa lugha yao wenyewe huenda mbali kuziba pengo la kitamaduni. Ukiwa na tajriba inayofaa, utapata kuwa watu ni marafiki zaidi na wanasaidia sana kila uendako.

Nani Anazungumza Kiswahili?

Kiswahili ni lugha inayozungumzwa sana katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, na hufanya kama lugha ya kawaida kwa watu wengi wa Afrika Mashariki (ingawa sio lazima kuwa ndio lugha yao ya kwanza). Nchini Kenya na Tanzania, Kiswahili ni lugha rasmi pamoja na Kiingereza, na watoto wa shule za msingi kawaida hufundishwa kwa Kiswahili. Waganda wengi wanaelewa Kiswahili tena kwa sasa kimewekwa kama somo la lazima kwenye mtaala mpya wa madarasa ya chini ya sekondari yaani kidato cha kwanza na cha pili, ingawa ni nadra kuzungumzwa nje ya mji mkuu, Kampala. lakini wengine husema wanyankore waishio magharibi mwa nchi uganda ndio wamekibeba kiswahili hadi hapa kilipo. Lugha rasmi ya Visiwa vya Comoro mara nyingi huainishwa kama lahaja ya Kiswahili.


HISTORIA FUPI YA KISWAHILI NCHINI UGANDA
Kiswahili ni lugha ya asili iliyotokea katika pwani ya Kenya. Katika karne ya 20 kiswahili kilikuwa kimeishaimarika na kukubariwa nchini Kenya na Tanzania lakini Uganda kilikuwa bado hakijaenea. Kiswahili kilifanya majukumu mengi katika ya nchi hizo mbili Kenya na Tanzania.

Kifursa, kutumika kwa lugha ya Kiswahili katika vita vya guerrilla kati ya wanajeshi wa NRA Walioongozwa na Museveni na wale wa rais Obote ndicho kilichokipa Kiswahili fadhila katika macho ya viongozi wa NRM. Hatimaye kikapewa kipaumbele kutumika katika makundi ya wanajeshi baada ya rais Museveni kupata uongozi. (tafsiri yangu)
Whiteley (1969) anaripoti kuwa Kiswahili kiliendelea kutumiwa na polisi, sehemu za Kaskazini kuwasiliana na watu ambao hawajui Kiingereza na Luganda. Vilevile Wanilotiki wa Uganda walitumia sana Kiswahili kuwasiliana na makabila mengine. Kiswahili kilitumika pia kwenye mipira, na sehemu nyingine ambazo Kiingereza na Luganda havikuhitajika au havikuwezekana kutumika.
Kulingana na Mukama (1995) kabaka mutesa 1 ambaye alikuwa anaongoza wakati huo alikuwa anapenda lugha. Kama ndilolililokuwa la muhimu siku hizo Kiswahili kilikuwa kimeishaenea katika maeneo mengi ya afrika mashariki pamoja na Afrika Ya kati juu ya biashara.
Wakati wamisionari walipofika Uganda kama H.m stanely (1864) Kiswahili kilianza kuenea juu ya kusambazwa kwa injili lakini baada yao kujifunza lugha nyingiine Kiswahili kikabaki nyuma.

Whiteley (1969) anaripoti kuwa Kiswahili kiliendelea kutumiwa na polisi, sehemu za Kaskazini kuwasiliana na watu ambao hawajui Kiingereza na Luganda. Vilevile Wanilotiki wa Uganda walitumia sana Kiswahili kuwasiliana na makabila mengine. Kiswahili kilitumika pia kwenye mipira, na sehemu nyingine ambazo Kiingereza na Luganda havikuhitajika au havikuwezekana kutumika.
Kingine, kuja kwa wote wasome ya shule za msingi (UPE), serikali inalaumiwa kwamba wote wanaoacha kusoma shuleni ni kwa ajili ya kutojua kingereza katika shule za misingi (1981, December 2oo4).Hata hivyo, kwa urahisi wanaweza wakazungmza katika Kiswahili.
Kiswahili ni lugha inayotumiwa katika vyombo vya habari. Sasa hizi televiseni ambazo zinakuja zinaendelea kutumia Kiswahili kamaRadio FM OPG, Mbale FM,Uganda Radio zinachangia katika kukuza Kiswahili katika nchi nzima ya Uganda. Hata hivyo Uganda inakaribia kuanzisha magazeti yanayotumia Kiswahili. Hivi vyote vitasaidia katika kuelimisha watu na kuwaangazia kuhusu masuala yanayowakabili. Mfano thabiti ni kwamba wakati ugonjwa wa ebola ilipokuwa inasambaa katika Uganda ya kaskazini, wakati huo Kiswahili kilikuwa kinatumika kuelimisha watu kuhusu jinsi ya kujiokoa na kuelewa usafi wa watu binafsi.

Katika siasa, wanajeshi wanatumia Kiswahili kuendeleza umoja na kukomesha ukabila. Katika Uganda ya kaskazini, Kiswahili ndiyo lugha inayotumiwa kupigania uhalifu na ukosefu wa usalama inayoletwa na uasi. Kupitia njia hiyo, Kiswahili ni kifaa cha kuleta umoja wa makabila inayotamaniwa leo.
Sasa, wanasiasa wanaowakilisha Uganda katika bunge la afrika masahriki wanatumia lugha ya Kiswahili. Hata nyumbani, wagombea viti vya ubunge kutoka kaskazini, mashariki, na magharibi wanatumia lugha ya Kiswahili katika kampeni zao. Juu ya yote, mbio uraisi haiwezi ikakamilika bila wagombezi kutumia Kiswahili. Hii ni maanakwamba hivi karibuni lugha ya Kiswahili itachukua jukumu la kuleta demokrasia kati ya wanaUganda na hatimaye itachukuliwa kiraia kutumika katika elimu kama ilivyo Kenya na Tanzania.
Katika biashara, jukumu la Kiswahili la Kiswahili linaweza kukaguliwa. Inabidi kieleweke kwamba lugha hii iliingia Uganda hasa juu ya Biashara na imechangia sana kitaifa na kimataifa. Juu ya hayo yote, lugha hii ni lugha muhimu katika kuleta umoja. Inatumiwa katika thieta na barabarani na wakomedia kubrudisha watu.
Nordic Journal of African Studies 15(2): 154–165 (2006) Kiswahili and Its Expanding Roles of Development in East African Cooperation:
A Case of Uganda
MWENDA MUKUTHURIA
Egerton University, Kenya.

MATATIZO YALIKIKUMBA KISWAHILI NCHINI NCHINI UGANDA.

Upotwashwaji wa Kiswahili NCHINI UGANDA hutokea kwa namna kadhaa kwamfano,) MAGANGA anatufahamisha kwamba lugha ya maandishi ya Kiswahili chini uganda ilianza kutumika katika Baraza la Kifalme la Buganda na Bunyoro, hata kabla ya ukoloni (1862). Nchini Uganda Kiswahili kilitumika katika shughuli za biashara, dini na mila.
Wakoloni walipofika walikuta lugha hii inatumika, ingawa sio kwa kiwango kikubwa.
Wakoloni walikitumia katika maswala ya kiserikali na kidini. Lakini maendeleo ya Kiswahili nchini Uganda yalikuwa duni sana ukilinganisha na Tanganyika na Kenya.
Maganga, (1997) anaeleza kuwa Sababu zilizokifanya Kiswahili nchini Uganda kuwa duni sana ukilinganisha na Tanganyika na Kenya ni kama ifuatavyo:
(a) Waganda walikiona Kiswahili kwamba ni lugha ya ki-Islamu, na Waislamu ni maadui wa dini ya Kikristo, na kwa hiyo, Waislamu ni maadui wa Wakristo. Hivi ndivyo ilivyoaminika wakati ule huko Uganda.Kwa mantiki hiyo, kukipenda Kiswahili waliona ni kuwakaribisha Waislamu ambao ni maadui wakubwa wa Wakristo, kwani Kiswahili kilimaanisha Uislamu.
(b) Katika kufundishia elimu, mkazo zaidi ulikuwa katika matumizi ya Kiingereza na lugha ya Bunganda. Kiswahili kilitumika katika sehemu chache tu kwa upande wa Elimu, kama vile Jimbo la Mashariki (isipokuwa Busoga), sehemu za Kaskazini na Magharibi ya Nile.Kwa msingi huo, Bunyoro, Toro, Ankole na Buganda hazikufundishwa lugha ya Kiswahili.
(c) Watawala na viongozi pia walipinga kuenezwa kwa Kiswahili nchini Uganda. Kabaka Daudi na Maaskofu wa Uganda walipinga kuenezwa kwa Kiswahili nchini Uganda; badala yake walipendelea lugha ya Buganda iwe lugha rasmi ya Uganda.Kutokana na hatua hii, Kiswahili kilitengwa kuhusishwa katika shughuli au mipango ya maendeleo ya Uganda.
Kiswahili kilididimizwa zaidi na Tume ya Kifalme ya Afrika Mashariki ambayo ilizuia kutumika kwa Kiswahili na Vyombo vya Serikali, Kiingereza peke yake ndicho kilichopewa kipaumbele badala ya Kiswahili
(d) Nchini Uganda Kiswahili kilifikiriwa kwamba ni lugha ya watumwa. Na kwa kuwa Kiswahili kilitumiwa zaidi na Polisi na Wanajeshi ambao, kwa bahati mbaya mara nyingi walikosa nidhamu, wananchi wengi waliichukia lugha hii kwa kuinasibisha na utumwa.Kwa msingi huo, Waganda kwa ujumla wao hawakuwa tayari kukipokea Kiswahili.
(e) (Mnamo, 1960)na(Maganga, 1997) Serikali ya Uganda iliporuhusu na kulazimisha Kiswahili kitumike nchini Uganda; Kiingereza na lugha za kikabila zilikuwa tayari zinatawala mawasiliano Uganda nzima.
(f) Kwa ujumla wakati wa ukoloni, matumizi ya Kiswahili nchini Uganda yalibakia sehemu za Kaskazini tu, tena mapolisi, wanajeshi na madereva wa taksi tu, ndio waliotumia Kiswahili; na watumishi hotelini waliongea Kiswahili cha kibiashara.
Uchanganyaji wa Kiswahili na kingereza na pia kutumia Kiswahili kwa maneno yasio sanifu na pia utumizi wa Kiswahili ulioathiriwa na sarufi ya lugha za kikabila hususan kimatamshi na kimuundo.



Ikiwa unasafiri nchini Rwanda au Burundi, Kifaransa labda itakufikisha mbali kuliko Kiswahili, lakini maneno machache hapa na pale yanapaswa kueleweka na juhudi zitathaminiwa. Kiswahili pia huzungumzwa katika sehemu za Malawi, Zambia, DRC, Somalia, na Msumbiji. Toleo la mwaka wa 2019 la chapisho la kumbukumbu Ethnologue linakadiria kuwa lahaja za Kiswahili huzungumzwa kama lugha ya kwanza na watu takriban milioni 16, na kwamba zaidi ya watu milioni 82 huizungumza kama lugha ya pili. Hii inafanya Kiswahili kuwa lugha ya 14 inayozungumzwa zaidi ulimwenguni.

	

MANENO YA UKOO-

1. Kaweto => Mwanamke anayeolewa na mwanamke mwingine ili amzalie katika ndoa yake.
2. Mkembe => Kijana aliyebaleghe na hajaoa.
3. Mlungizi => Ndugu anayezaliwa baada yako.
4. Mtawa => Mwanamke anayewekwa ndani kwa ndani na kuangaliwa asitoke ovyo.
5. Mziwanda => Mwana wa mwisho.
6. Mhavile => Mume wa Shangazi.
7. Mhale => Mume wa Halati.
8. Mkwerima => Jina ambalo wazazi wa mke humwita mume wa binti.
9. Ahali => Jina jingine la mke.
10. Kirimale => Mke aliyepewa talaka. Pia huitwa Mtalaka.
11. Mwamu => Kaka wa mke wako.
12. Suriama => Mtoto wa suria
13.Mjukuu-Mtoto wa mtoto wa nyanya
13.Kitukuu-Moto wa mjukuu
14.Kilembwe-Mwana wa kitukuu
15.Kilembwekeza-Mwana wa kilembwekeza
16.Amu-Kaka wa baba
17.Bavyaa-Mzazi wa kiume wa mume wako
18.Mavyaa-Mzazi wa kike wa mume wako
19.Binamu-Mwana wa kiume wa amu
20.Bintiamu-Mwana wa kike wa amu
21.Mkoi-Mwana wa mjomba/shangazi
22.Shemeji-Ndugu wa mume/mke
23.Wifi-Mke wa kaka
24.Mwamu-Kaka wa mke
25.Mnuna-Ndugu anayekufuata

SARUFI FAFANUZI.

Sarufi fafanuzi inakusudi kutoa maelezo yasiyo ya hukumu ya muundo wa kisarufi ya  lugha fulani. Ni uchunguzi wa jinsi lugha inavyotumika, kwa maandishi na kwa usemi/mazungmzo. 

Wanaisimu ambao wamebobea katika sarufi fafanuzi huchunguza kanuni na mifumo ambayo inategemea matumizi ya maneno, vishazi, virai, na sentensi.
Kwa maana hiyo, kivumishi "fafanuzi" ni cha kupotosha kidogo kwani sarufi fafanuzi hutoa uchambuzi na ufafanuzi wa sarufi ya lugha, sio ufafanuzi tu.

Sarufi fafanuzi haitoi ushauri bali inaelezea kwa kina njia au kanuni ambazo wasemaji wa asili/ wazaawa hutumia katika lugha yao. 

Sarufi fafanuzi ni uchunguzi wa lugha kwa undani na matumizi yake.
Kwa lugha yoyote hai, sarufi fafanuzi kutoka karne moja itatofautiana na sarufi fafanuzi ya karne ijayo kwa sababu lugha itakuwa imeishabadilika.

Mfano katika ya kinyankore-kikiga  ya karne ya kumi inatofautiana na hii inayotumiwa katika karne hii ya ishirini ( 20th century). Mfano neno “taata” maana yake ikiwa mzazi wa kiume limebadilika kuwa “muzeeyi” katika karne za hivi karibuni.

Kwaufupi sarufi fafanuzi ni sarufi matumizi.

Sarufi fafanuzi ni seti ya sheria na kanuni kuhusu lugha kulingana na jinsi inavyotumika. Katika sarufi fafanuzi hakuna lugha sahihi au mbaya.Inaweza kulinganishwa na sarufi ya maagizo, ambayo ni seti ya sheria au kanuni kulingana na jinsi watu wanafikiria lugha inapaswa kutumiwa.

Kama ilivyoelezewa hapo juu, sarufi fafanuzi inajaribu kuelezea matumizi ya lugha kulingana wazungumzaji wa asili ya lugha hiyo. 

Sarufi fafanuzi inadokeza kwamba mamlaka pekee ya kile kilichopo katika lugha ni kile wasemaji wake wa asili wanakubali na kuelewa kama sehemu ya lugha yao. Kwamfano katika lugha ya kinyankore- kikiga tunakubali kwamba neno “empunu” maana yake ni nguruwe na ni hivyo hivyo tu isipokuwa labda neno limekatazwa na wanyankore kutolitumia kwa maana hiyo. Lakini kila mzungmzaji atakuwa anaelewa kuwa “empunu” ni nomino yenye maana ya nguruwe.

Kwa kuhitimishwa suala la isimu fafanuzi, ikumbukwe kwamba isimu fafanuzi ya lugha hubadilika wakati baada ya mwingine na pia isimu fafanuzi ya lugha moja ni toafauti na ya lugha nyingine kwa kutegemea watumiaji lugha hiyo.






arigumaho810@gmail.com.




DHIMA/UMUHIMU WA VIPERA VYA FASIHI SIMULIZI.

Kabla ya kuangazia fasili ya fasihi simulizi,  ni muhimu sana kwanza kuangalia fasili ya Fasihi ni nini? Nakwahivyo  Meyer, m (2005) anasema “Fasihi haiwezi kuwa na fasili moja kwasababu ya ugumu na uhalisi wake kama ilivyo katika maisha yenyewe. Hakuna fasili ya fasihi ambayo kwayo itaridhisha kila mmoja kwa sababu fasili zote zinaegemea katika upekee wa kazi za watu husika”.(tafsiri ni yangu). Nakwahivyo, nitajadili fasili za wataalamu tofauti kulingana na mawazo yao katika kazi tofauti  walizozishuhudia halafu nitoe fasili yangu binafsi.

  kwa mujibu wa Wamitila (2003:13) anasema kuwa fasihi ni sanaa inayotumia lugha na ambayo hujishughulisha na binadamu pamoja na maisha yake na huathiri, hugusa na huacha athari fulani na hupatikana katika umbo ambalo linatambuliwa na jamii fulani.

Naye Senkoro (2011) anasema kuwa fasihi ni sanaa itoayo maudhui yake kwa kutumia lugha ya maneno ambayo hutambwa ama kuandikwa. Fasili hii ina maana kwamba nyenzo kuu ya fasihini lugha na huweza kuwasilishwa kwa maumbo mawili yaani maandishi na masimulizi.

Hivyo, kutokana na fasili hizi, Fasihi ni sanaa inayotumia lugha kuwasilisha ujumbe unaomhusu binadamu na mazingira yake itolewayo kimdomo au kimaandishi.

 Sanaa ni ufundi wa kuwasilisha fikra na hisia za binadamu kama vile maneno, maandishi, uchoraji, uchongaji,ufinyanzi n.k.

Fasihi simulizi

Nakwahivyo, fasihi simulizi imefasiliwa na wataalamu mbalimbali wa fasihi kama vile Wamitila (2002) anasema kuwa fasihi simulizi ni fasihi ambayo huwasilishwa kwa njia ya mdomo kwa kusimuliwa, kuimbwa, kutongolewa au kughaniwa.

 (Wamitila 2003) katika Nyang’hani (2016:19) fasihi simulizi ni dhana inayotumika kurejelea kazi ambazo kimsingi hupokezanwa kwa njia ya masimulizi au midomo. Tawi hili la fasihi linatumiwa katika jamii kwa njia ya kupashana maarifa yanayohusu utamaduni fulani, historia ya jamii, matamanio yao, mtazamo wao na historia yao        Katika fasili yake wamitila, anaangazia sana kusudi la fasihi simulizi katika jamii kuwa ni kusimulia matukio ya kiutamaduni, kihistoria, matamanio na mawazo ya wanajamii hao kuhusu maisha walimokulia, wanamozungukia na watakamoishi siku zijazo kwa njia ya midomo.

Naye (Mulokozi 1996:22) anafasili Fasihi simulizi kuwa ni fasihi inayotungwa au kubuniwa na kuwasilishwa kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia Maandishi. Hivyo simulizi na tukio linalofungamana na muktadha  fulani wa kijamii na kutawaliwa na mwingiliano wa mambo kama fanani (msanii), hadhira, fani inayotendwa, tukio, mahali na wakati.

TUKI (2004) inatoa fasili ya fasihi simulizi kuwa ni fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine kwa njia ya mdomo kama vile hadithi, ngoma, na vitendawili. Fasili hii ina maana kuwa nyenzo kuu ya uwasilishwaji wa fasihi simulizi ni mdomo na kwamba fasihi simulizi hurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine baada ya kuhifadhiwa.

Lakini fasili hii ya TUKI ina mapungufu yake kwa mfano haijaelezea hiyo fasihi simulizi inahifadhiwa wapi ili iweze kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine ila kwa mujibu wao njia kuu ya kuwasilisha fasihi simulizi ni mdomo kwa maana kwamba hakuna njia nyingine inayoweza kutambulisha fasihi simulizi zaidi ya njia ya mdomo pekee.

Fasihi simulizi ni sanaa inayobuniwa ikawasilishwa na kusambazwa kwa lugha ya mdomo. Vyombo vyake vikubwa ni mdomo na sauti ya binadamu katika hali ya kuumba, kusimulia, kuiga, kughani, kutambara, kutega, miradi yote yanatolewa kwa mdomo na ishara za mwili (Mazrui na Symbo. 1992:2),

Msokile (1992 :3) anasema kuwa fasihi simulizi ni kazi ya sanaa inayotumia lugha. Kazi hiyo huifadhiwa kwa kichwa na kusambazwa kwa njia ya masimulizi ya mdomo. Anamalizia kwa kusema kwamba, fasihi simulizi imekuwa ikirithishwa kutoka kizazi hadi kizazi. Fasili hii ina

ubora wake kwa sababu ni kweli fasihi simulizi hurithishwa kutoka kizazi hadi kizazi na pia njia kuu ya uwasilishaji wake ni masimuliizi ya mdomo, lakini kwa upande mwingine ina mapungufu

kwa sababu inaonesha njia moja tu ya uhifadhi wa fasihi simulizi kwa maana kwamba fasihi

simulizi huhifadhiwa kichwani tu, haijazungumzia njia zingine za uhifadhi wa fasihi simulizi

zilizotokana na maendeleo endelevu ya sayansi na teknolojia kama vile vinasa sauti, kanda za

kurekodi na maandishi.

Kutokana na fasili hizo, natoa kauli kwamba Fasihi simulizi ni sanaa inayotumia lugha  simulizi  na utendaji inayowasilishwa kwa hadhira kwa njia ya ana kwa ana, kupitia tanzu zake na kuhifadhiwa kwa njia ya kicwa, kurekodi na njia nyingine za kielektroniki ili iweze kubaki na kurithiswa  kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

Umuhimu wa vitendawili.

c) Kukuza uwezo wa kufikiri/kudadisi k.m vitendawili na chemshabongo.

d) Kufariji k.m mbolezi na methali k.m. ‘Baada ya dhiki faraja’.

e) Vipengele vya fasihi simulizi k.v mashairi, nyimbo, nahau, hutumiwa katika uandishi wa fasihi

andishi.

f) Kuhifadhi historia ya jamii k.m. mighani, visaviini, mapisi, tarihi n.k.

g) Kukejeli tabia zinazokiuka matarajio ya jamii k.v soga, methali, n.k.

h) Kuendeleza tamaduni za jamii kwani husawiri imani na desturi za jamii. k.v kitendawili

‘Nyumbani mwetu mna papai lililoiva lakini siwezi kulichuma.’ – Mtu hawezi kumwoa dadake.

i) Kuunganisha watu pamoja kwa kuwajumuisha pamoja wakati wa ngoma, kuimba, utambaji, n.k.

j) Kukuza lugha k.v. misimu inapokita kimatumizi na kujumuishwa katika lugha sanifu.

k) Kukuza uwezo wa kutumia lugha kadiri mtu anapoendelea kuwasilisha k.v. hotuba, vitanza

ndimi husaidia kuboresha matamshi na kutofautisha maana za maneno.

l) Kuza uwezo wa kubuni k.v. malumano ya utani, vitanza, ndimi ngonjera, n.k.

m) Kukuza uzalendo kwa kufanya wanajamii kuonea fahari jamii zao na kuiga mashujaa au watu

waliotendea jamii makuu.

n) Kuonya na kutahadharisha wanajamii dhidi ya tabia hasi k.v. ulafi, uchoyo, n.k.Dhana ya pili ya kufasili katika makala hii ni tanzu ambapo dhana imefasiliwa na wataalamu

Umuhimu wa vitendawili

a) Kuburudisha jioni baada ya kazi.n

b) Kukuza ubunifu wa kuvitunga kwa kulinganisha vitu katika mazingira ili kuviunda.

c) Kuimarisha uwezo wa kukumbuka.

d) Kukuza uwezo wa kufikiri kwani mfumbiwa huhitaji kufikiri sana ili kupata jibu.

e) Kuleta umoja na ushirikiano katika jamii kwa kuleta watu pamoja wakati vinategwa.

f) Kuimarisha ujuzi wa kujieleza kwa lugha.

g) Kupanua ujuzi wa mazingira wa mtoto.

h) Kuendeleza utamaduni wa jamii k.m. Nyumbani mwetu mna papai lililoiva lakini. siwezi

kulichuma

 Ndugu wa kiume asimuoe nduguye wa kike.

i) Kukejeli au kudharau tabia mbaya k.m. Wazungu wawili wanachungulia dirishani

Umuhimu methali.

a) Kukuza uwezo wa kufikiri kwani mpokezi hufikiri ili kupata maana ya ndani.

b) Kuonya dhidi ya matendo yasiyofaa k.m. ‘Mchimba kisima huingia mwenyewe’na ‘Ukiambiwa

jiambie usijeishia kumbe.’

c) Kufariji walio katika hali ngumu, Baada ya dhiki faraja, Hakuna marefu yasiyo na ncha,

Liandikwalo ndilo liwalo, Ajaliwalo ndilo apatalo.

d) Kuhimiza watu kujitahidi maishani/kuonyesha jambo jema huja kwa kufanyiwa kazi k.m.

‘Mtaka cha mvunguni sharti ainame,’ ‘Chumia juani ulie kivulini.’

e) Kupamba lugha iwe na mvuto kwani huwa na usanii mkubwa.

f) Kuhimiza ushirikiano, ‘Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, ‘Jifya moja haliijiki chungu.’

g) Kuelimisha mtu ajue jambo muhimu k.m. ‘Usione kwenda mbele kurudi nyuma si kazi’, ‘Pema

usijapo pema ukipema si pema tena.’

h) Kushauri k.m. ‘Enga kabla ya kujenga’ na ‘Mchama ago hanyeli.’

i) Kufupisha maadili katika ngano.

j) Kubuni lakabu k.m. ‘kikulacho.’

k) Kufunza maadili k.m. kuwa na subira-‘Subira huvuta heri.’

l) Kuhimiza kutokata tama k.m. ‘Bandu bandu huisha gogo’ ‘Papo kwa papo kamba hukata njiwe.’

m) Kuonyesha umuhimu wa kuthamini jamaa zako kuliko marafiki k.m. ‘Damu ni nzito kuliko

maji’ ‘Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.’

n) Kuonyesha umuhimu wa kuthamini vitu vyako-‘Usiache mbachao kwa msala upitao’ ‘Afadhali

dooteni kama ambari kutanda,’

o) Kukashifu ubinafsi k.m. ‘Mwamba ngoma huvutia kwake’ ‘Kila mchukuzi husifu mzigo wake.’

p) Kukashifu kiburi k.m. ‘Maskini akipata matako hulia mbwata’ ‘Zingwi zingwi lipe nguo utaona

Umuhimu semi

a) Kuonya k.m methali, ‘Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.’

b) Kukuza uwezo wa kufikiri k.m. vitendawili na chemsha bongo.

c) Kutafsidi lugha au kupunguza ukali wa maneno k.m. nahau ‘jifungua’ badala ya ‘zaa’.

d) Kuburudisha k.m. vitendawili, chemsha bongo na vitanza ndimi.

e) Kuhifadhi siri k.m. nahau, misemo, misimu.

Umuhimu wa mighani

a) Kutambulisha jamii kwani kila jamii ina aina yake ya mighani.

b) Kuhifadhi na kumbusha historia yajamii.

c) Kusifu mashujaa katika jamii.

d) Kuhimiza ujasiri miongoni mwa vijana.

e) Kuelimisha jamii kwa kuwapa maarifa ya kukabiliana na adui au changamoto.

f) Kukuza uzalendo kwa kuhimiza watu kuiga mashujaa na kupigania jamii.

g) Kuonya dhidi ya matendo hasi kama vile usaliti.

h) Kuhimiza watu kutokata tama.

Umuhimu ngano za mtanziko

a) Hutuerevusha jinsi ya kupambana na hali ngumu.

b) Kuonya/kutahadharisha dhidi ya kujiponza.

c) Kukuza uwezo wa kupima mambo na kuteua lililo muhimu.

d) Kuonya dhidi ya kutenda bila kuwaza kwa kina.

Umuhimu ngano za mashujaa

a) Kuhimiza uzalendo na ujasiri miongoni mwa vijana.

b) Kuhimiza ujasiri miongoni mwa vijana.

c) Kusifu mashujaa katika jamii

d) Kuelimisha jamii kwa kuwapa maarifa ya kukabiliana na changamoto, inda na ila.

e) Kuhimiza uzalendo kwa kuhimiza watu kuiga mashujaa na kupigania jamii.

f) Kuonya dhidi ya matendo hasi k.v. ukatili.

g) Kuhimiza watu kutokata tamaa

Umuhimu ngano za mazimwi

a) Kukashifu tabia ya uovu, ulafi, na ukatili.

b) Kutahadharisha dhidi ya kuwa na ulafi, ukatili n.k.

c) Kutia moyo waliodhulumiwa kuwa waliowanyanyasa wataadhibiwa siku moja.

Umuhimu wa visasili

a) Kueleza asili ya mambo kama vile kifo, utamaduni n.k.

b) Kueleza utaratibu wa kutekeleza desturi k.v. mahari.

c) Kuhalalisha baadhi ya mila na desturi za jamii k.v. ulipaji mahari, uabudu miti, n.k.

d) Kukitisha mizizi imani fulani ya watu.

e) Kupunguza athari za majanga kama vile kuhalalisha kifo.

f) Kutambulisha jamii kwani kila jamii ina aina yake ya visasili.

g) Kuhifadhi historia na utamaduni wa jamii

Umuhimu ngano za hekaya

a) Hutahadharisha watu dhidi ya kuhadaika kwa wepesi.

b) Huonya dhidi ya matokeo yanayoweza kuwapata wanaojinyakulia mali kwa udanganyifu.

c) Kuonya dhidi ya usaliti. d) Kukashifu viongozi dhalimu na matendo maovu

MWONGOZO WA TAMTHILIA YA CHEMA CHAJIUZA-Innocent Agume.

MWONGOZO KAMILIFU WA TAMTHILIA YA CHEMA CHAJIUZA.

MWALIMU JOHNPAUL ARIGUMAHO.

arigumaho810@gmail.com.0778514179.

INKSIRI

MwongozoKamilifu wa Chema Chajiuza ni kazi ambayo imejadili kwa muhtasari ploti au muundo wa tamthilia ya Chema Chajiuza ukionyesha kila kitendo na kila onyesho visa vikuu vilivyotendeka.Pia, wahusika na sifa zao tukirejelea kurasa wanapojitokeza, maudhui pamoja na ufafanuzi vipatikanamo tamthiliani chema Chajiuza bila kusahau mbinu za kifani na kisanaa mwandishi alizotumia kupamba lugha ili kukamilisha ujumbe wake.

TABARUKU.

Natabaruku kazi hii kwa mama yangu mpendwa Bi katekista Katushabe Beatrice na wowote wanaojali.

Pia, bila kuwasahau wataalamu na wakiwemo Mwalimu Abaho Rogers, Simon kawaida, Ariiho Edwin, Vicent Muhereza, Earnest Muwuta Mwase. Mwenyezi Mungu awabarike na kuwapa kila la kheri.

SHUKRANI.

Mchakato mzima wa kukamilisha kazi hii haukuwa kwa bidii zangu kama Johnpaul Arigumaho bali iliweza kukamilika kutokana na michango pamoja na misaada ya watu wengine.

Kwanza mwenyezi mungu sina kikomo kumshukuru kwa kila kitu.

Tena, shukrani zangu za pekee zimwendee Mh.Innocent Agume aliyebobea sana na kuangalia kwa undani kilichomo katika kizazi cha leo kwa kutunga tamthilia ya Chema Chajiuza, shukrani sana mheshimiwa.

Vilevile, sina budi kuwashukuru wa ambao hawaniachi nyuma bali kila mara nikiwafikia wananielekeza katika njia inayostahili na hao ni Mh.Mhadhiri Bwana Kubakurungi Abraham, Mh.Mhadhiri Bi-Asiimwe Caroline PamojaMh.Mhadhiri Bi-Ninsiima Betty. Moyo wangu ndio unaojua jinsi ninavyojihisi juu ya ninyi.

Tamthilia hii ya chema chajiuza iliandikwa na Innocent Agume aliyezaliwa wilayani Ntungamo magharibi mwa Uganda. Innocent ni mwandishi aliyeinukia kwa kasi na mwenye jicho la ndani katika uga wa fasihi na lugha.

Tamthilia hii ya chema chajiuza inazungumzia juu ya unafiki na wema unaopatikana katika kizazi cha leo.

Mwandishi anasema kwamba wengi wanapoajiriwa wanajidai ni wafanyakazi waadilifu na wenye bidii kwelikweli, kumbe ni vinyonga wanaogeuza rangi ili wawasaliti marafiki na kuwaibia waajiri wao!

Tunaona injinia Bakehena anaonyesha unafiki wake kwa kupunja na kuiba pesa za mwajiri wake kabaila Bumaali na mwishowe akafutwa kazini halafu maisha yake yakabadilika kuwa magumu sana.

Lakini miongoni mwa watu wengi, kuna wachache wazuri na wenye wema.

Yeye Bwana Kwatampola katika tamthilia tunamuona anaonyesha wema wake kwa kuwa mfanyakazi mwadilifu na mwaminifu kwa mwajiri wake kabaila Bumaali na kisha akatunukiwa na zawadi kubwa Iliyokuwa ndoto yake kila siku na ndio sababu chema chajiuza.

PLOTI/ MUUNDO WA TAMTHILIA.

Muundo huwa ni mtiririko wa visa na matukio katika kazi za kifasihi. Hapa, tutaangalia jinsi mwandishi Innocent alivyofuma matukio kwa muhtasari kutoka kitendo cha kwanza hadi kitendo cha nne na mawazo makuu yaliyomo.

KITENDO CHA KWANZA.

ONYESHO LA KWANZA.

Hapa, tunamuona Bwana Kwatampola nyumbani kwake kakoba anazungumza na mke wake Kunihira juu ya kukosa kumkuta Mzee Bumaali.

Bwana Kwatampola tunamuona baada ya kuambulia patupu anapanga miadi na mtumishi kumpigia simu ili amkute Kabaila Bumaali.

Pia, tunamuona Injinia Bakehena anafutwa kazini na analalamika juu ya kabaila Bumaali kwa kumfukuza.

Vilevile, tunamuona Kunihira analalamika juu ya mume wake kwamba labda alirogwa kwakuwa pesa anazozipata kutoka kwa Bumaali hazitumiki vyema iwezekanavyo.

ONYESHO LA PILI.

Hapa tunamuona Bumaali na Kwatampola wameketi uani. Bumaali anamwelezea Kwatampola kwamba alipata kidosho na anataka akitengenezee jumba huko Nyamitanga. Bumaali amempa Kwatampola milioni thelathini (30) ili ashughulikie kazi nzima ya kujenga ugo halafu atajenga jumba zima. Milioni thelathini ni za vifaa na vibarua. Bumaali anamwambia Kwatampola kwamba injinia bakehena alimuibia pesa na asimsaliti kama yeye.

ONYESHO LA TATU.

Hapa, tunawaona Mzee Bahemuka na mke wake Bi-Shogora njiani wanamtembelea mwanao Kwatampola

huko kwake Kakoba. Mzee Bahemuka anatembea kwa kuinama na na kuiweka mikono yake juu ya mkongoji alioulaza mabegani kwake. Bi-shogora na mumewe Bahemuka wanatembea wakizungumuzia juu ya mtoto wao kwamba ni maskini mzuri tena mwadilifu. Tunawaona wamefika Kakoba nyumbani kwa Kwatanpola mtoto wao, mke wake Kwatampola Kunihira anawakaribisha kwa heshima na kumpa mcheja wake Bi-Shogora maji ya Rwizi ya kunywa kupuuza joto la njia. Papo hapo, Kunihira anawaelezea kwamba mtoto wao babake Ben yumo kitandani na Ben mwenyewe ameenda shuleni.

Vilevile, Kwatampola anakuja kutoka kitandani na kuwasalamia badaaye anaondoka nje na babake halafu Kunihira akabaki nyumbani na mcheja wake Bi-shogora wakijadiliana.

Baada ya muda mchache, tunawaona Bahemuka na mke wake bi shogora wanaondoka kurudi kwao Rwampala.

KITENDO CHA PILI.

ONYESHO LA KWANZA.

Hapa, tunawaona Kwatampolana mkewe Kunihira nyumbani kwao wanazungumuza pamoja. Kwatampola anamwambia mkewe kwamba Mzee Bumaali amemuita asubuhi na kumpa kandarasi ya mradi kujenga ugo na badaaye atajenga jumba zima huko Nyamitanga.

Tunawaona pia Kwata na mkewe Kuni wanaondoka kwenda kule Nyamitanga pale jumba litakapojengwa. Tunaona Kuni amepewa kazi ya kupikia wajenzi wote na kwata anawasimamia wajenzi wake.

ONYESHO LA PILI.

Hapa, tunamuona kabaila Bumaali anamshukuru kwatampola kwa kujenga ugo vizuri na kwa muda uliokuwa unatakikana. Bumaali anampa kwata bunda la noti ya shilingi milioni mbili ili azigawanyie vibarua wake kwa kazi waliyoifanya na Kwata anashukuru sana.

Pia, tunamuona Bakehena anazungumuza na Kwatampola kuhusu masuala ya pesa alizopewa na kabaila Bumaali halafu anaenda maramoja hadi nyumbani kwa kwata na kumwelezea Kunihira kwamba mume wake Kwata amepewa hela nyingi sana na ameenda mjini mbarara kuzitumia ovyoovyo.

Tunamuona Kunihira baada ya kusikia ujumbe huo anashutuka na kumuita Ben kwa kumtusi kwamba ni mjinga kama babake kwa hasira.

 Papohapo, tunamuona Kwata anaingia. Mkewake anaanza kulalamika juu ya ujumbe alioupokea ya kwamba amepewa hela na ameenda mjini kuziharibu kumbe kwata alikuwa ameenda kuvinunua vifaa vya ujenzi.

Tunamuona Kunihira maramoja anaingia nyumbani na kuchukua begi yake kubwa na kurudi kwao Kabale. (talaka inafanywa). Tunamuona Ben mtoto wao analia juu ya kuachwa na mamake lakini babake Kwata anambembeleza na halafu anamtwaa Rwampala kwa mzee Bahemuka na Bi-shogora ili wamlee hadi mamake atakaporudia.

ONYESHO LA TATU.

Hapa, tunamuona Kwatampola na wajenzi wake mkutanoni huko Nyamitanga katika uwanja wa ujenzi. Kwata anawagawanyia hela alizopewa na kabaila Bumaali juu ya kazi nzuri waliyoifanya ya kujenga ugo.

Tena, Kwata anawaelezea wajenzi kwamba alikumbwa na vita vya kibinafsi, tamaa na mwishowe mke wake akamuacha.

Wajenzi wanakabidhiwa hela na kila mtu akachukuwa shilingi 36956.52. Wote wajenzi wanamshukuru kwata na kabaila Bumaali.

KITENDO CHA TATU.

ONYESHO LA KWANZA.

Hapa, tunamuona Kunihira Nyamitanga katika uwanja wa ujenzi tena jikoni kwa upishi anawahudumia wajenzi.

Tunawaona wajenzi wote na mainjinia wanafanya kazi kwa bidii.

ONYESHO LA PILI.

Hapa, tunawaona kwata na mainjinia watatu wanaongea kwa sauti za chini sana.

Injinia wa tatu anamwambia kwata kwamba yeye ni msomi hataki vitu vya upesiupesi. Pia tunamuona injinia huyo anamshukuru kwata kwa kazi nzuri.

ONYESHO LA TATU.

Hapa, tunamuona Injinia Bakehena nyumbani kwake chumbani mwake anazungumuza na mke wake Nabaganzi. Nabaganzi anamwambia mume wake kwamba Kabaila Bumaali anamtangaza kwa marafiki zake wote ya kwamba alimuibia pesa.

Pia, tunamuona Bakehena anapanga kuelekea mjini Fortportal kutafuta kazi ya kufanya ili naye aajiriwe kama wengine.

KITENDO CHA NNE.

ONYESHO LA KWANZA.

Hapa, tunamuona Nabaganzi anaongea na kwatampola katika uwanja wa ujenzi huko nyamitanga. Tunaona kwatampola amempa Nabaganzi kazi ya ufagizi na anashukuru sana.

ONYESHO LA PILI.

Katika onyesho hili, tunawaona Bumaali, Akello na wajenzi wote huko Nyamitanga katika kasri na wanakagua kazi waliyoifanya kwa muda.

Kabaila Bumaali anashukuru sana Kwata hadi kiasi cha kumbusu mkononi juu ya kazi nzuri aliyoifanya na wajenzi wake wote.

Pia, tunamuona injinia wa pili anahakikisha uzuri wa Bwana Kwatampola kwa kusema kwamba hata mitaimbwa, rangi na mabati viliibwa lakini Kwata alitumia pesa zake mwenyewe kununua vipya.

ONYESHO LA TATU.

Hapa, tunaona wageni washerehekeaji wakiendelea kumwajika wakiwemo wafanya biashara mashuhuri, wanasiasa, wanadini wake na waume wote Nyamitanga uani wa kasri la Machu.

Pia, tunawaona wageni waalikwa na wasioaalikwawote wanakaribishwa. Mziki unaendelea kupigwa polepole na Mc-bob king. Watu wote wamefurahi sana.

Bwana harusi Bumaali na Bi-harusi Machu nao wanakaribishwa. Mziki unadundwa tena na Mc.Bob king mfawidhi.

Vilevile, tunaona Bumaali anatoa hotuba kwa kushukuru kila mtu na mke wake wa kwanza Bi-Akello.

 Bumaali anazawadia kwatampola juu ya wema wake kwa kumpa kisanduku chenye funguo na hati ya maandishi yaliyo ya kumpa jumba hilohilo alilojengea Machu la Nyamitanga.

Bila shaka tunamuona Kunihira anatoka shoti juu ya yale aliyoyasikia na wanakuja kumhudumia kwa kumuzoea pale alipokuwa ameanguka. Kunihira anapelekwa Mbarara Regional Referal hospital.

Vivyohivyo, Bumaali anahitimisha kwamba atarudi kwake Makenke na wake wake wote wawili na kumwachia kwata jumba la Nyamitanga.

WAHUSIKA NA SIFA ZAO KATIKA TAMTHILIA YA CHEMA CHAJIUZA.

Wahusikani viumbe hai au visivyohai vinavyoshirikishwa katika kazi yeyote ya kifasihi ili kujenga maudhui na dhamira ya mwandishi.

Wahusika wanaweza wakawa kama vile wanyama, ndege, wadudu, nakadhalika. Tunaainisha wahusika hao kwa makundi tofauti kama vile wahusika wakuu, wahusika wadogo na wahusika wasaidizi.

Hivyo basi, katika tamthilia hii ya chema chajiuza, kuna wahusika kadhaa mwandishi aliowatumia kufikisha ujumbe wake kwa hadhira na baadhi yao ni;

KWATAMPOLA: Mhusika huyu ana sifa zifuatazo;

  • Ni mhusika mkuu kwani tunamuona anajitokeza aghalabu katika tamthilia nzima.
  • Ni mzazi kwani tunamuona katika tamthilia anambembeleza mtoto wake aitwaye Ben. (uk 23)
  • Ni mume kwani katika tamthilia tunamuonandiye aliyeoa Kunihira.
  • Ni mwanake Mzee Bahemuka na Bi-Shogora kwani tunawaona wanakiweza wakati walipomtembelea kwake Kakoba.(uk 23)
  • Ni mfanya kazi kwani tunamuona hata alizawadiwa juu ya wema wake katika kazi ya kujenga jumba la Machu huko Nyamitanga.(uk 115)
  •  Ni mtiifu kwani tunamuona katika tamthilia anamtii mwajiri wake Kabaila Bumaali hata kufika kiwango cha kutomuita jina lake bali kumuita Mzee.
  • Ni mwenye mapenzi kwasababu kinawekwa wazi katika tamthilia na mke wake Kunihira wakati alipo toka shoti akaacha karamu akaenda naye hostitalini. Pia anampenda mtot wake Ben kwa kumuimbia nyimbo za kumbembeleza baada ya mamake kufanya talaka(uk 47)

KUNIHIRA: Mhusika huyuni mhusika mkuu na ana sifa zifuatazo kulingana na jinsi anavyochorwa katika tamthilia.

  • Ni mke wake kwatampola kwani hata tunaona katika tamthilia anamuita Bi-Shogora mcheja wake tena ndiye anayechorwa kama mke wake kwata katika mchezo. (uk 49)
  • Ni mhusika mkuu kwani tunamuona anajitokeza aghalabu katika vitendo vyote.
  • Ni mamake Ben kwani tunamuona katika tamthilia anamuacha mtoto Ben na kufanya talaka. (uk 25)
  • Ni mjasiri kwani tunamuona katika tamthilia anajiunga mkono na wafanya kazi wa kiume na kuwapikia au kuwahudumia kama mpishi. (uk 32)
  • Ni mvumilivu kwani tunamuona anavumilia maisha yao ya kimaskini na mume wake Kwata hadi walipobadilika kuwa watajiri.(uk 27)
  • Ni mtiifu kwani anamtii mume wake Kwatampola kwa kuitika wito wa kupikia na kuishi na vibarua.
  • Ni mwenye mapenzi kwani kinawekwa wazi katika tamthilia ya kwamba alivumilia umaskini wao pamoja mumewake Kwatampola, hakuna mapenzi yanayozidi uvumilivu huo. (uk 27)
  • Ni mfanya kazi kwani tunamuona anahudumia vibarua kwa kuwafanyia kazi ya kuwapikia huko Nyamitanga. (uk 32)

BUMAALI: Mhusika huyu ana sifa zifuatazo kulingana na jinsi anavyochorwa katika tamthilia ya chema chajiuza;

  • Ni mume kwani alimuoa Bi-Akello na Bi-Machu hasa katika sherehe za kumuoa mke wa pili (uk 113)
  • Ni kabaila au mtajiri mkubwa sana kwani ana nyumba nyingi mjini Mbarara na tena alipompa Kwata milioni 30 ni ishara ya utajiri. (uk 13)
  • Ni mume wao Bi-Machu na Bi-Akello kwani anawatambua wakati wa sherehe za kumuoa Machu mke wake wa pili huko Nyamitanga. (uk 113)
  • Ni mwenye mapenzi kwani tunaona katika tamthilia anamjengea jumba Machu na anakiweka wazi pale ambapo tumemuona anamsimulia Kwata kuhusu kidosho chake alichopata huko Rwebikona, huo ni upendo wa kiwango kikubwa kubwa. (uk 116)

BI-AKELLO: Mhusika huyu ana sifa zifuatazo kulingana na jinsi anavyochorwa katika tamthilia ya chema chajiuza;

  • Ni mkewe wa kwanza wa Bwana Bumaali kwani kinaoneshwa katika tamthilia katika sherehe za kumuoa mke wa pili Bi-Machu. (uk 113)
  • Ni mvumilivu kwa kuvumilia maisha ya kuolewa kwa mke wa pili kwani si rahisi hata hakipatikani  mtu kuvumilia kama yeye hasa katika kizazi cha leo.(uk 112)
  • Ni mtiifu kwani anamtii mume wake Bumaali kwa kukubali yote aliyomwambia.
  • Ni mwenye moyo wa kupa kwani tunamuona anakubali kumpa zawadi kwatampola kwa kazi aliyoifanya.(uk 105)

BI-MACHU: Mhusika huyu ana sifa zifuatazo kulingana na jinsi anavyochorwa katika tamthilia ya chema chajiuza;

  • Ni mtoto wa Daudi kwani tunawaona Kwata na mke wake wanasema kwamba, kunihira atakuwa mcheja kwake kwani wana uhusiano yao na Daudi.(uk 29.)
  • Ni mwenye mapenzi kwani alikubali harusi juu ya mapenzi.(uk 113, 116)

NABAGANZI: Mhusika huyu ana sifa zifuatazo kulingana na jinsi anavyochorwa katika tamthilia ya chema chajiuza;

  • Ni mke wake Injinia Bakehena kwani tunawaona kwao baada ya kufutwa kazini wanazungumuzia jinsi ya kutafuta kazi (uk 81)
  • Ni mjasiri kwani anajiunga na wajenzi huko Nyamitanga kwenye uwanja wa wajenzi na kufanya kazi ya ufagizi bila kuogopa. (uk 90)
  • Ni mwenye mapenzi kwani tunamuona anakubali kuishi na mume wake Bakehena hata baada ya kufutwa kazini.(uk 81)
  • Ni mvumilivu kwasababu ukweli unaonekana pale alipoamua kufanya kazi ya ufagizi huko kwenye uwanja wa ujenzi Nyamitanga. (uk 90)
  • Ni mfanya kazi kwani tunamuona anaacha familia yake na kwenda huko Nyamitanga kwenye uwanja wa ujenzi na kufanya kazi ya ufagizi bila kuaibika kama mwanamke aliyekuwa mtajiri muda mchache nyuma. (uk 90)

BAHEMUKA:Mhusika huyu ana sifa zifuatazo kulingana na jinsi anavyochorwa tamthiliani chema chajiuza;

  • Ni mume kwani ni mume wake Bi-Shogora kwani tunawaona wote wanakaribishwa nyumbani kwa kwatampola. (uk 23)
  • Ni babake kwatampola kwani tunamuona Bahemuka alipokuwa anaelekea kakoba anazungumuza na mke wake kwamba walimzaa mtoto maskini mwadilifu na mwema na atazikwa na wengi. (uk 21)
  • Ni mwenye mapenzi. Je kwatampola alitoka wapi? Ni juu ya mapenzi kati ya Bahemuka na Bi-Shogora. Pia, anampenda mtoto wake Kwata ndipo akamtembelea (uk 23)

BI-SHOGORA: Mhusika huyu ana ssifa zifuatazo kulingana na jinsi anavyochorwa katika tamthilia ya chema chajiuza;

  • Ni mke wake mzee Bahemuka.
  • Ni mzazi kwani ndiye mamake Kwatampola kulingana na tamthilia.(uk 23)
  • Ni mwenye mapenzi kwani isipokuwa mapenzi asingemtembelea mtoto wake Kwatampola kumuona huko Kakoba, huo ni upendo wa mama kwa mtoto. (uk 23)
  • Ni mtiifu kwani anamtii na kumheshimu mume wake Bahemuka.

BAKEHENA: Mhusika huyu ana sifa zifuatazo kulingana na jinsi alivyochorwa katika tamthilia ya chema chajiuza;

  • Ni mwizi kwani tunamuona katika tamthilia aliiba pesa za kabaila Bumaali mwajiri wake na kufutwa kazini. (uk 13)
  • Ni mwenye mapenzi kwani anampenda mke wake Nabaganzi. (uk 81)
  • Ni mfanya kazi kwani tunamuona ni injinia mjenzi wa nyumba. (uk 13)
  • Ni mvumilivu kwani anavumilia maisha ya umaskini hata bila kujiua baada ya kufutwa kazini.
  • Ni mume kwani ni mume wake Nabaganzi.(uk 13, 81)

MAUDHUI KATIKA TAMTHILIA YA CHEMA CHAJIUZA:

Maudhui ni jumla ya mambo, mawazo, mafunzo, maoni na ujumbe unaowasilishwa na mwandishi wa kazi ya kifasihi.

Hivyo basi, Johnpaul (2019) kwa maoni yangu nasema maudhui ni ujumbe, mawazona mafunzo yanayopatikana katika kazi yeyote ya kifasihi na jinsi msanii anavyosisimua hisia kuhusu kazi hiyohiyo.

Katika tamthilia ya chema chajiuza, mwandishi Innocent Agume alishughulikia maudhui kadhaa, na baadhi ya hayo ni kama vile;

  • MAPENZI: Mapenzi ni hali ya mvuto na upendo alionao mtu kwa mtu mwingine. Katika tamhilia hii ya chema chajiuza upendo huonekana kati ya Kwatampola na mkewe Kunihira (uk 27), Mzee Bahemuka na Bi-Shogora (23), Bakehena na Nabaganzi (uk 81), Bumaali na wake wake wawili yaani Bi-Machu na Bi-Akello (uk 116) (uk…)
  • UJASIRI: Hii ni hali ya kutokuwa na uoga aukutoogopa kitu chochote kwamfano, katika tamthilia hii ya chema chajiuza ujasiri unaoneka pale Nabaganzi na Kunihira walipojivunia na kufanya kazi na wajenzi wanaume bila uoga. (uk 32, 90)
  • UTUMISHI: Ni hali ya kufanyishwa kazi kwa malipo au kutolipwa. Katika tamthilia hii, Kwatampola anasema kwa kumjibu Bumaali ‘’ taja mtumishi wako yuko tayari kutimiza wajibu’’ (uk 12), Bakehena, Nabaganzi, Kunihira na wajenzi wengine ni watumishi. r
  • UZAZI: Hii ni hali ya kuzaa. Kwamfano katika tamthilia hii ya chema chajiuza mwandishi Innocent anatuonyesha kwamba Kwatampola na Kunihira walimzaa Ben (uk 47), Bahemuka na Bi-Shogora walimzaa Kwatampola (uk 21), lubengula alimzaa Bumaali nk rejelea(uk 12)
  • NDOA: Ni mafanikio rasmi baina ya mwanamume na mwanamke ili waweze kuishi pamoja kama mke ne mume. Katika tamthilia hii ya chema chajiuza, ndoa inapatikana kati ya Bwana Kwatampola na Kunihira, Bumaali na wake wake wawili (uk 116, 113), Bakehena na Nabaganzi nakadhalika.
  • WIZI: Ni tendo la kuchukua kitu kisicho chako bila ruhusa la mwenyewe. Kwamfano mwandishi anatuonyesha kwamba mitaimbwa, rangi na mabati yaliibwa huko katika uwanja wa ujenzi(uk 102) Pia, injinia Bakehena alimuiba Bumaali mwajiri wake na kisha akafutwa kazini. (uk 13) rejelea tena (uk 55)
  • MABADILIKO: Ni hali ya kugeuka kwa mambo. Katika tamthilia hii, mwandishi Innocent anatuonyesha wahusika wengi ambao maisha yao yalibadilika kama vile Kwata kutoka umaskini kuwa mtajiri (uk 115), Bakehena alibadilika toka utajiri kuwa maskini alipofutwa kazini (uk 81).
  • UTAJIRI: Ni hali ya kuwa na mali au fedha nyingi sana. Kwamfano tamthilia hii ya chema chajiuza inatuonyesha kwamba kabaila Bumaali ni mtajiri kwakuwa anamiliki nyumba nyingi na pia anampa kwata milioni thelathini za kununua vifaa vya kujenga ugo na kulipa vibarua (uk 13) Kwatampola ni mtajiri baada ya kupewa jumba la Nyamitanga (uk  115)
  • Kinyume cha utajiri, pia kuna maudhui yaUMASKINI katika tamthilia hii ya chema chajiuza: Umaskini ni hali ya kutokuwa na hela au mali. Kwamfano tunaonyesha wahusika wengi ambao ni maskini kama vile Kwatampola alikuwa maskini kabla ya kuzawadiwa na jumba kwani tunaona alikuwa analala katika kiota kama ndege (uk27), Bakehena badaaye aligeuka kuwa maskini hadi kufika kiwango cha kutafuta kazi huko Fortportal (uk 13), Nabaganzi hadi kufika kufanya kazi ya ufagizi (uk 90), Kunihira anasema Ben ameenda kwa jirani kuona Runinga na huo huonesha umaskini. nk.
  • NDOTO: Ni maono yanayotokea usingizini. Kwamfano katika tamthilia ya chema chajiuza, tunamuona Kwatampola aliota kuwa mtajiri halafu akawa (uk 02)
  • UTIIFU: Ni tabia ya adabu au nidhamu, hali tendo au uwezo wa kufuata amri au kutii. Kwamfano Kunihira anamtii mume wake Kwatampola, Kwatampola anamtii Bumaali kwani tunamuona anampa hata kutomuita jina bali humuita ‘’Mzee’’
  • UVUMILIVU: Ni hali ya kuvumilia maisha magumu. Kwamfano katika tamthilia ya chema chajiuza , mwandishi Innocent anachora Nabaganzi kama mvumilivu kwakuwa anavumilia hali ya umaskini na kfanya kazi ya ufagizi baada ya mume wake kufutwa kazini (uk 13), kwatampola na mkewe wanavumilia maisha ya umaskini (uk 27) nk
  • ELIMU: Ni mafunzo yanayotolewa na jamii kwa watu ama darasani au pasipokuwa darasani. Kwamfano tunamuona Injinia wa tatu ni msomi (uk…), Ben anasoma(uk 09)nk
  • UTENGANO: Ni hali au tendo la kuachana na kukaa mbalimbali na kitu kingine  bila kushirikiana. Kwamfano katika tamthilia ya chema chajiuza, tunaona utengano kati ya Kwatampola na Mke wake Kunihira alipofanya talaka, Machu anatengana na familia yake na kuolewa kwa Bumaali (uk 47, 113)
  • NYIMBO: Ni sauti zilizopangwa kimziki. kwamfano katika tamthilia ya chema chajiuza, mwandishi Agume Innocent anatuonyesha mziki unadundwa na mc.Bob King katika sherehe ya harusi ya kumuoa Bi-Machu (uk 111).
  • UTAMADUNI: Hii nimila, asili, jadi na desturi zinazofutwa na kundi la jamii Fulani. Kwamfano tunamuona Bumaali anasema ‘’kulingana na mila na desturi zetu, Kwatampola hatalajiwi kuwa katika kalamu hii’’ (uk 113). Hii ni kwasababu katika tamthilia mwandishi anatuonyesha kwamba Kwata ni ami yake Machu.

MBINU ZA KIFANI, LUGHA NA SANAA KATIKA TAMTHILIA YA CHEMA CHAJIUZA.

Mbinu au fani na uteuzi wa maneno na kuwekwa katika kazi za kifasihi ili kuifanya lugha iwe ya kuvutia na kupendeza.

Mwandishi wa tamthilia hii ya chema chajiuza Innocent Agume ametumia mbinu kadhaa kuvutisha na kupendesha kazi yake, na baadhi ya mninu hizo ni kama;

  • METHALI: Ni misemo ya hekima yenye maana iliyofumbwa. Kwamfano Katika tamthilia hii, tunaona methali kama haraka haraka haina Baraka (uk 02), kila mbwa na siku yake (uk 13), hakuna siri ya watu wawili (uk 17), dawa ya moto ni moto (uk 49), akufanyia kwa dhiki ndiye rafiki (uk 43), mtenda mema hulipwa mema (uk 105).
  • SEMI NA NAHAU: Ni fungu la maneno yanayotumika kutoa maana nyingiine badala ya ile ya maneno yaliyotumika. Semi hutumika kuficha maneno makali au kupamba lugha. Mwandishi katika tamthilia hii hutuonyesha semi kam vile vuta nikuvut (uk 21), siku ayami (uk 21), cha mtema kuni (uk 58), kata kauli (uk 14) nk.
  • MASWALI YA BALAGHA: Haya ni maswali au masimulizi yasiyohitaji majibu. Kwamfano katika tamthilia hii ya chema chajiuza mwandishi anatuonyesha maswali kama vile ‘’una nini ambacho ulininunulia nikisahau?’’ (uk 85), ‘’wamejigamba kama wewe, wakajuta badaaye?’’ (uk85), ‘’jina lako sasa halina soko?’’ (uk 87) nk..
  • TAKRIRI: Hii ni mbinu ya kurudirudia neno au fungu la maneno ili kusisitiza ujumbe ulani. Kwamfano katika tamthilia ya chema chajiuza tunaona urudiaji wa maneno kama vile, leo ni leo (uk 14), Kwata anasema ‘’kwa hizo hizo nitafanya kazi yako’’ (uk 14), wasiwasi (uk 13), nyumba ni nyumba bora imesimama (uk 30), dhiki ni dhiki hata iwe ndogo (uk 43), Ben Analia kwi kwi kwi, ‘’mama usiniache mama usiniache’’ (uk 47).
  • TASHIBIHI: Hii ni mbinu ya lugha inayolinganisha vitu au hali mbili tofauti kwa kutumia maneno ya kulinganisha kama vile, kama, mithili ya, sawa na, nk. Na katika tamthilia tunaona mbinu ya tashibihi inajitokeza pale kwamfano ‘’tufe kama mtakatifu Stefano aliyekubali kifo cha kosa ambalo hakulifanya’’ (uk 4), na leo pia nimekuita  kwa kazi ngumu kama mawe (uk 12), amejenga nyumba kubwa kama dunia ya wamasaba wa Bugisu (uk 13), mjinga kama baba yako (uk 45), wanamziki ni kama mbwa (uk 108).
  • KUCHANGANYA NDIMI: Hii ni hali ya kutumia maneno yasiyo ya Kiswaahili katika lugha ya Kiswahili. Kwa mfano, katika Tamthilia hii ya chema chajiuza, kuna maneno kama radio west (uk 99) na posho (uk 99). Pia kuna Balya hardware (UK 14) na ok one two three (UK 108). Mbarara Regional Referal pia inatajwa (uk 116).
  • UTOHOZI: Hii ni mbinu ya kuwasilisha maneno ya lugha nyingine yatamkwe katika Kiswahili. Kwamfno mwandishi anatumia maneno kama hospitalini (uk 115), dereva (uk 116), korasi, sinema nk
  • CHUKU: Hii ni kutilia chumvi ili kusisitiza ujumbe fulani. Kwamfano katika tamthilia hii ya chema chajiuza, mwandishi anatuonyesha chuku kama Bumaali alipomwambia Kwata ‘’nakuamini kushinda ninavyojiamini’’ (uk 13), shogora anasema ‘’maji yamepita kiwango cha baridi, sijabakiza hata jino moja’’ (uk 24)
  • MAJAZI: Hii ni mbinu ambayo mtunzi wa kazi ya fasihi hutumia kufananisha tabia za wahusika na majina yao halisi. Kwamfano katika tamthilia mwandishi alitumia majina kama ‘’Bakehena’’ maana ya kwamba mjifanyia mabaya. Tena kabaila Bumaalai kwakuwa alikuwa mjajiri sana. Kwatampola kwa maana ya kutenda mambo yake kiupole bila kuruka ruka.
  • TASWIRA: Hii ni mbinu inayomfanya msomaji kupiga picha ubongoni. Kwamfano (uk 115) kwatampola tunamuona anapewa zawadi la jumba.
  • UZUNGUMZAJI NAFSI: Hii ni mbinu inayomhusu mhusika anapojizungmzia au kwa kuongea au kuwaza bila kukusudia kusikika na yeyote. Kwamfano tunamuona Kwatampola katika tamthilia anazungmza mwenyewe baada ya kupewa pesa za kujenga ugo (uk 14).
  • HOTUBA: Hii ni mbinu inayotoa mazungmuzo yanayohusu jambo maalumu, kwamfano tunamuona Bi-Akello anatoa hotuba (uk 113), hotuba ya Bumaali (uk 112).
  • KISENGERE NYUMA: Hii ni mbinu ya Sanaa ambayo mwandishi hutumia kusimulia mambo yaliyotokea huko nyuma, kwamfano Bumaali anamuelezea kwata jinsi babake lubengula alivyopenda mchezo huo wa kuoa wengi (uk 12).
  • TAHARUKI: Hii ni mbinu inayoibuka baada ya msomaji kusoma na kubaki na hamu ya kuendelea kusoma. Kwamfno kunihira anapotoka shoti na wakamhudumia pale alipoanguka na kumpeleka hospitalini (uk 115), taharuki inawabakia watu wakijiuliza je, alipofika huko hospitalini palitokea nini? Nk
  • MAZUNGUMZO: Ni majadiliano kati ya watu wawili au Zaidi kuhusu jambo Fulani, kwamfano kuanzia ukurasa wa kwanza hadi ya mwisho ni mazungmzo kwani kuna maogezi kila onyesho.
  • TASHIHISI: Hii ni mbinu ya kupatia kitu kisicho na uhai kuwa na sifa za kiumbe mwenye uhai. Kwamfano Injinia wa kwanza anasema ‘’mawingu yanapiga makofi kwa furaha zako’’ (uk 102) Pia, Bakehena anasema ‘’jina lako litaanza kusafiri mawinguni kama ndege’’ (uk 75).
  • NYIMBO: Ni mbinu ya kutumia nyimbo katika kazi ya kifasihi kufikisha ujumbe kwa hadhira, kwamfano kuna nyimbo katika sherehe za harusi unaoogozwa na Mc-Bob King Mfawidhi (uk 111, 110).

Hivyo basi, ninahitimisha kwa kusema kwamba, ni kweli mwandishi Innocent Agume jicho lake liliangalia ndani ya uga wa fasihi na kuelezea ukweli uliopo katika kizazi cha leo ambacho kimejaa na unafiki kwa wale wanaojidai kuwa ni waadilifu kumbe ni vinyonga vinavyojigeuza rangi na kusaliti wenzao hasa katika uwanjani tunapofanyia kazi, kwamifano Bakehena.

Tena kwakuwa anaelezea kuhusu wema anapotumia mhusika Kwatampola, shukrani kwake kwakuwa hata katika kizazi cha leo wema upo nakwahivyo wale wenye uadilifu ndio wanaoajirika na kufaulu katika maisha ya leo.

Vilevile, napenda kusema kwamba, kwa kweli CHEMA CHAJIUZA na KIBAYA CHAJITEMBEZA.

Hvyo basi nahitimisha kwa kutoa methali katika lugha ya kinyankore inayosemwa kwamba ‘’Nyakwehena akeenyampira naarya’’ yenye maana kwamba mtenda mabaya anajiharibu mwenyewe nikirejelea jinsi Innocent anavyomchora mhusika Bakehena na namna anavyoishia na maisha yake.

Tena wanawake ambao mmepata wanaume wa aina hiyo kama Bakehena, ushauri wangu ni kwamba muwashauri wawe waadilifu na waaminifu ili kujiokoa na matatizo kama haya. 

Kazi hii inaelezea kwa muhtasari Vipengele muhimu yaani ploti/muundo, wahusika, maudhui pamoja na mbinu za kifani na kisanaa vinavyojitokeza katika tamthilia ya chema chajiuza iliyoandikwa na Innocent Agume.

Bila shaka, kazi hii itawafaa walimu na wanafunzi wa somo la Kiswahili katika shule za sekondari, vyuo vya walimu na vyuo vikuu ambao wamekuwa wakipata changamoto ya kuvisoma vitabu vizima, chema Chajiuza kimeisha chambuliwa.

Vilevile, kazi hii itawanufaisha na kuwafurahisha wapenzi wa lugha ya Kiswahili kwa kupata marejelo halisi katika tamthilia yenyewe.

Kwa mantiki hiyo, kazi hii itatoa mchango mkubwa katika harakati za kusoma na kuchambua kazi nyingine za kifasihi.

Hivyo basi, mwandishi wa kitabu hiki Mh.Innocent Agume anafaa zawadi kama ile iliyopewa na Kwatampola kwa kuandika kazi nzuri na inayorejelea mazingira halisi ya kizazi cha leo.

Kazi hii imetengenezwa namwalimu Johnpaul Arigumaho mpenzi halisi wa fasihi na lugha ya Kiswahili.

                                      arigumaho810@gmail.com.

0778514179..

Kila la kheri.

kazi hii bado ni mbegu. ni mwongozo tu sicho kitabu halisi.

Mwalimu Johnpaul Arigumaho.

@arigumaho810.gmail.com

UTENDI WA FUMOLIYONGO

Neno “utendi” linatokana na kitenzi “kutenda” maanake huwa ni kutenda jambo Fulani.
Chaligha (2013), anaeleza kuwa, kumetumika fomula, kuelezea maana ya Utendi kuwa ni E = M + Ms yaani (Epic= Mars + Music/muse), yaani Utendi ni mungu, Muziki na Vita (U=M+V). Akifafanuwa maelezo hayo, Chaligha (kashatajwa), anasema Utendi ni tukio la kimuziki linalozungumzia vita na miungu.


Mawazo hayo yana mashaka, kwa upande wa Utendi/Utenzi wa Kiswahili. Uswahilini, Utendi na Utenzi, tofauti ni matamshi. Tendi Uswahilini si lazima zizungumzie miungu kama aonavyo Chaligha. Uswahilini kote, neno “miungu” ni kufuru.
Chaligha (ameshatajwa), alieleza kuwa, tendi simulizi ni tungo simulizi zenye mtindo wa kifomula, zinazohusu mambo ya ajabu, ya watu wasio wa kawaida. Masimulizi hayo yanasimuliwa kwa njia ya mdomo. Utendi/Utenzi wa Kiswahili hughaniwa katika miktadha mingi kama vile, sherehe na msiba.


Mulokozi (1999), anaeleza kuwa, Utendi ni utungo mrefu wa kishairi wenye kusimulia hadithi ya ushujaa na mashujaa. Kwa jumla, Mulokozi anaona kuwa, Utendi lazima uwe na mhusika shujaa. Mawazo hayo, hayana ukweli wa moja kwa moja kuhusiana na Utendi wa Kiswahili.
Wamitila (2010), anaelezea kuwa, Utendi ni aina ya Utenzi ambao, unazungumzia maisha na matendo ya ushujaa au ya mashujaa wa jamii fulani. Tendi ni simulizi, ambazo husimuliwa na mtunzi na ambazo huchukuwa mkondo unaofanana katika kazi za kishairi. Mawazo ya Wamitila yametoa mwelekeo tofauti na wa Mulokozi (ameshatajwa), juu ya dhana ya Utendi. Utendi/Utenzi na Nathari au Tutumbi hukutana kwenye maudhui lakini si kwenye fani, kila utanzu una mitindo, miundo, kanuni, ada na taratibu zake. Uswahilini, hakuna Utendi ama Utenzi wa kinathari au kitutumbi.


Utendi/Utenzi ni bahari kuu na kongwe ya Ushairi wa Kiswahili. Kusilazimishwe swala na mbuzi- mmoja na wapili ni wa majumbani.
Mawazo ya Wamitila (2010), yana upungufu. Kuna vielezea vya Utendi, havikuhusishwa katika ufafanuzi wake. Vielezea hivyo ni sifa za pekee za fani za Utendi wa Kiswahili, kama vile; muundo wa beti, bahari ndogo ya kila ubeti, vina na mizani pamoja na urefu wa Utendi huo..
Baada ya kutalii mawazo ya wanataalimu waliotangulia, dhana ya Utendi imeweza kuelezeka kwa kupambanuliwa kwa sifa ya Utendi/Utenzi ambao hufuata kaida ya urari wa vina na mizani na huweza kuwa na mhusika shujaa au asiyekuwa shujaa.


Mhusika huyo mkuu, huitwa nguli. Vile vile, tendi, huelezea masuala yanayoihusu jamii, kama vile, masuala ya kijamii, ya kisiasa, ya kiuchumi na ya kiutamaduni.
Masimulizi hayo, hutolewa kwa lugha ya kishairi, ambayo ujumi wa lugha hiyo, hutegemea jamii inayohusika na masimulizi yenyewe yanayotolewa huwa kwa ajili ya jamii, ili kuwa katika mwenendo bora wa maisha ya hapa Duniani na Akhera.
Utendi ni aina ya ushairi na tanzu moja wapo wa fasihi simulizi ambao husimulia Maisha na matendo ya mhusika shujaa au wa visasili.


Utenzi ni ni utungo mrefu wa kishairi unaoelezea juu ya mambo Fulani na maranyingi huwa na pande moja yaani huwa na vina vya kati tu. Utenzi haufuati urari wa mizani.
Katika Kiswahili, kuna tenzi kuu maarufu kama vile utenzi wa tambuka(Bwana mwengu karne ya 18), utenzi wa mwanakupona(mwanakupona karne ya 19), utenzi wa inkshafi(Abdallah bin ally), utenzi wa hayati sokoine(kazi ya Charles mloka karne ya 20), utenzi wa hati na adili(shaban robert), utendi wa Fumoliyongo (muhamad kijumwa 1913)

Utangulizi wa utendi wa Fumoliyongo.


Utendi wa fumoliyongo unamhusu shujaa liyongo. Baadhi ya wataalamu (mbele 1986:138-140) hudai kuwa jina lake lilikuwa “liyongo fumo” sio Fumoliyongo yaani Fumo alikuwa ni babake. Wengine wataalamu wakiwemo (knappert 1983:144)”fumo” ilikuwa tu wadhifa wake sawa na mfalme. Bado kuna utata na mjadala mkubwa kuhusu tarehe ya liyongo, na wengine wanadai kuwa yaweza kuwa kiumbe tu hadithini ambaye hajapata kuishi.
Hata hivyo, kuenea kwa hadithi yake na umashuhuri wake katika mapokezo na matendo ya kiimla ya waswahili yanaashiria kuwa huenda mtu huyo aliishi kweli hata kama habari zake za kuishi zimetiwa chumvi na waenezaji.
Baadhi ya wataalamu (Nabhany 1987, Mbele 1986) wanasema liyongo aliishi karne ya 9 masihiya (miaka ya kikristo)


Wengine wakiwemo Chiraghdin (1973) naKnappert (1983:167) wanasema liyongo aliishi baina ya miaka ya 1160-1204 lakini tarehe inayoelekeya kukubaliwa ni ile ya karne ya 13-14. Hii ni kwasababu kitabu cha Tarekhe ya Pate(Freeman Greenvile 1962:241-299) kinamtaja mtawala wa jimbo la Ozi aitwaye Fumoliyongo aliyeishi kati ya utawala wa Fumomari.
Fumoliyongo alikuwa shujaa wa kitaifa aliyeishi eneo la mto wa Tana kaskazini mwa Mombasa. Babake alikuwa kiongozi wa mji wa shaka.
Babake liyongo alikuwa na watoto wawili yaani Liyongo mwenyewe na kakake Daudi mringwari.


Fumoliyongo alikuwa kiongozi mkuu kaskazini mwa pwani ya Afrika mashariki hapo karne ya 9-13. Anajulikana kama shujaa, kijudu, na mshairi wa mashairi ya jadi, hadithi na nyimbo za waswahili na hasa zilizohusu mila, harusi na densi za gungu. Miji kadhaa pwani huko Tanzania inadai kuwa ndiko alizaliwa. Baadhi ya nyimbo, mashairi na hadithi zake huzungmzia sherehe za harusi za kale, vita, na densi za gungu kama vile wimbo wa “sifu uta wangu (song of the worrier)”. Pengine liyongo anatambulika kama mjuzi wa upiga pinde.


Hadithi za kale za liyongo nyingi zilibeba sifa lingani na zile za ulaya kv Achilles, Sigurd, na Robinhood. Tena aliandika gungu nyngi kama “Sifa la Uta” au “Wimbo wa Mapenzi”
Fumo Liyongo wakati mwingine alikuwa askari na mwandishi wa mashairi katika pwani ya kaskazini ya Afrika Mashariki kati ya karne ya 9 na karne ya 13.


Fumoliyongo alikuwa kijana mwenye kusifiwa mjini kote, mrefu, mwenye matendo ya kishujaa, nguvu zisizo za kawaida aliyeishi ungwana na mashaha eneo la shaka jimbo la ozi.
Kama alivyoeleza Sigurd, liyongo alikufa kutokana na usaliti. Liyongo alisalitiwa na mtoto wake aliyetoboa siri ya nguvu za babake. Liyongo aliweza tu kufa akidundwa sindano ya shaba kitovuni. Hiyo ilikuwa siri kati ya liyongo na mamake aliyejulikana kwa jina “Mbwasho”.lakini liyongo alipoifunua kwa mtotoke, akaangamizwa na damu yake yenyewe.
Inasemekana kwamba, baada ya kifo chake, mwenye nguvu zake Liyongo alizikwa mji wa shaka jimbo la Ozi.

Kuhusu mwandishi wa utendi wa fumoliyongo;


Katika mwaka wa 1913, mwandishi wa mashairi Muhamad bin Omar Al-Bakry aliyejulikana sana kwa jina la Muhamadi Kijumwa aliandika juu utendi maarufu uitwao utendi wa Fumo Liyongo, utendi ambao ulikuwa ukielezea maisha ya Fumo Liyongo, aliyekuwa mshairi na pia mtawala katika eneo la Pate. Kijumwa kama yeye siye mwandishi bali alipata hadithi hiyo kutokana na simulizi za waswahili wa mwambao wa Kenya. Kijumwa hakuiandika hadithi bali alisimulia upya kwa njia ya utendi.


Muhamad kijumwa aliishi 1855-1940 alikuwa mwenyeji wa lamu nchini Kenya. Alikuwa msanii mashuhuri ambaye mbali na kutunga mashairi na tendi, vilevile alikuwa mjomi (mchongaji wa milango yenye nakshi), msanii-msanifu, msawidi (copyist) na mnukuzi wa miswada ya zamani.Habari za maisha yake hazijulikani bali anaanza kujitokeza kwenye miaka ya 1890 ambapo alikuwa anawasaidia watafiti wa kizungu kv Alice werner (1900-1935), William Hichens (miaka ya 1930).


Inasemekana kuwa, muhamad kijumwa alifariki mwanzoni mwa mwaka wa 1940 japo tarehe kamilii haitambuliki wazi mtoto wake Elesha aliishi Lamu. Kijumwa alitunga masahiri mengi yakiwemo utendi wa helewa.

Muhtasari wa utendi wa Fumoliyongo;


Utendi wa Fumo Liyongo unahusu mgogoro kati ya Fumo Liyongo na kaka yake, sultan wa Pate ambaye hajatajwa kwa jina. Mwanzoni utenzi unamdokeza Liyongo akiwa ana umri wa makamo hivi, aidha kimo na nguvu zake za mwili ziliwashangaza wengi kwa hivyo walimsifia mno.
Watu wa kabila la Wagalla walipofika Pate kutafuta chakula ili wanunue, walielezwa sifa za Liyongo na wananchi, halikadhalika Sultani wa Pate alimsifu Liyongo. Kwa kusikia sifa hizo za ajabu, Wagalla walitamani sana kumwona Liyongo, kwa hivyo wakamwandikia Liyongo warakawakimwomba aje ili wamwone.(beti 18,19)


Liyongo akaitikia wito huo, hivyo akapanga safari yake ya kwenda Pate huku amebeba mizigo chungu nzima.(beti 37,38)Kati ya vitu alivyovibeba ni panda, kinu na mawe. Kwa mwanadamu wakawaida, safari hiyo ni ya siku nne lakini Liyongo alichukua siku mbili tu na kufika Pate.
Alipokaribia jijini Pate, alipuliza panda ya kwanza hadi ikapasuka.Alipuliza ya pili nayo vile vile ikapasuka. Alipuliza ya tatu na kuingia mjini hadi barazani kwa sultani.(beti27,30, 31) Watu walishangaa mno kwa sauti kubwa ya panda. Watu wengi wakakusanyika kumwona, alipotua mzigo wake umejaa vitu vingi ambavyo vilitosha kuijaza nyumba nzima. Moja kwa moja, Wagalla wakakiri kuwa kweli Liyongo ni mtu mnene na mwenye nguvu. Wagalla wakatamani sana kuipata mbegu yake, hivyo walimwomba sultani awaruhusu kupata mbegu hiyo, kiongozi huyo akakubali.
Wakafanya mpango wa kumwoza mke wa Kigalla ambaye alimzalia mtoto wa kiume. Sifa za Liyongo zilivyozidi kusambaa ndivyo mgogoro kati yake na Sultan wa Pate ulivyozidi.
Mfalme alihofia kuwa huenda Liyongo angemnyang’anya ufalme hivyo akatafuta njia ya kumwangamiza.
Liyongo alipogundua njama ya Sultan ya kutaka kumwangamiza, akatoroka Pate na kwenda kuishi nyikani pamoja na Wadahalo, Watwa, Wasanye na Waboni.
Mfalme akafanya mpango wa kisiri pamoja na Wasanye na Wadahalo ili wamuue huko mwituni kwa kuwahidi malipo ya reale mia moja iwapo wangemletea kichwa cha Liyongo. Watu hao walifanya urafiki na Liyongo kisha wakashauri wawe wakicheza kikoa
pamoja. Hivyo wliachaguana kwa kupeana zamu ya kuangua makoma kutoka mtini. Walipanga kuwa ikifika zamu ya Liyongo, wamngojee apande mkomani kisha wamfume kwa mishale yao wamuue akiwa mtini.
Kwa uwezo wa kiakili aliokuwa nao Liyongo, akagundua njama hiyo. Badala ya kupanda mtini aliangua makoma akiwa chini aridhini hivyo wakashindwa kumuua.Watu hao walimpelekea Sultani ripoti kuwa haiwezekani kumuua Liyongo.

Mfalme aliwaambia warejee alipo Liyongo wamweleze kuwa mjini ni salama na hapana hatari yoyoyte ili waende naye huko. Waliporudi wakamweleza Liyongo uwongo huo ambao aliuamini kuwa kweli, kwahivyo akawafuata na kuenda nao mjini Pate.
Sultan akaandaa ngoma ya Gungu na mwao na kuwaalika wapenzi wa aina hiyo ya ngoma, Liyongo alikuwa mmoja wao. Ngoma iliposhika kasi, askari walimnasa Liyongo na kumtia korokoroni.
Mfalme na watu wake waliamua kumuua Liyongo akiwa gerezani.
Siku ya mauaji kutekelezwa zilipokaribia, Liyongo akapewa muda wakutoa ombi kwa kitu chochote apendacho. Liyongo akaomba apigigwe ngoma ya mwao naGungu.
Ombi hili likakubaliwa na ngoma ikaandaliwa. Ngoma ilipoandaliwa, Liyongo akatuma ujumbe wa kishairi kwa mama yake kupitia kwa kijakazi Saada ambaye humletea chakula.(beti 104, 105)


Katika ujumbe huo alieleza kwamba siku hiyo ya ngoma apike mkate wa wishwa na ndani yake atie tupa ya kukatia minyororo. Mama yake akafanya vivyo hivyo.
Kijakazi Saada alipompelekea chakula, walinzi wakachukua mikate waliyodhania kuwa mizuri na kuutupilia mbali ule wa wishwa ili umwendee Liyongo. Ngoma iliposhika kasi, Liyongo akatumia nafasi hiyo kukereza minyororo, hivyo akafaulu kuikata. Akavunja Lango kuu la jela na kutorokea msituni.
Mfalme alipoona kuwa ameshindwa kumuua Liyongo, akamshawishi mwanawe Liyongo aende amuulize babake kiwezacho kumdhuru.
Sultani alimpa ahadi ya kumwoza bintiye, kumpa uwaziri katika uongozi wake na mali nyingine ikiwa angefanikiwa.
Mwanawe Liyongo akafululiza hadi Shaka alipokuwa babake na kumtaka amweleze siri ya yeye kutodhurika na kitu chochote.
Ingawa Liyongo alitambua njama ya mahasidi wake ya kupitia kwa mwanawe, alikubali kumfichulia siri.
Alimweleza kuwa kiwezacho kumuua ni sindano ya shaba ikitiwa kitovuni mwake. Sultan alijawa na furaha sana, alipopewa taarifa hii na kijana huyu wa Liyongo.
Kwa hivyo akampatia sindano ya shaba, akampa ahadi zaidi na kumpa zawadi tele.
Akarejea Shaka tena alipo babake, akamngoja alipokuwa usingizini, akamchoma sindano ya shabakitovuni. Liyongo alizinduka na kuamka kwa hasira, akachukua mshale wake na kuelekea kisimani akimtafuta adui.


Akiwa amepiga goti, akatia mshale katika upinde huku akiuelekeza mjini na kukata roho. Umati wa watu walipomwona akiwa katika hali hiyo, wakadhani yuko hai na kaudhika mno. Kwa hivyo walijawa na hofu ya kwenda kuchota maji kisimani.
Walipozidiwa na ukosefu wa maji, walikwenda kumwomba mama yake Liyongo aje ambembeleze aondoke wateke maji. Mama yake akawa anaenda kumpembeleza mara kwa mara lakini alikosa kufanikiwa.
Hatimaye maiti yake iliaanguka ndipo watu wakabaini kuwa alikuwa ameshakufa.
Sultani alipopata habari ya kifo cha Liyongo alijawa na furaha. Akamwarifu mwanawe Liyongo kuwa babake amefariki. Badala ya kuwa na maskitiko, huzuni na maombolezo, yeye alifurahi.
Kitendo hiki kinamuudhi mfalme ambaye alichukua mali yote aliyokuwa amempa. Wanajamii wakamfukuza kijana huyu asitangamane nao. Siku chache baadaye akakumbana na maradhi yasiyokuwa na tiba ambayo yalimwangamiza.


Sifa za Fumo Liyongo;
Mwandishi Kijumwa (1973), amemsawiri mhusika Fumo Liyongo kishujaa katika utendi wenyewe. Kwa upande wangu nachukua mtazamo huo huo wa kishujaa alioutoa mwandishi ili kubaini sifa zake.
Kwa mujibu wa Wamitila (2003), neno shujaa hutumika kueleza mhusika mkuu katika kazi ya kifasihi ambaye anaweza kuwa wa kike au wa kiume.
Kimsingi neno hili haliashiri wema tu. Kwa upande wake, Mulokozi (1996), anasema kuwa mashujaa wa utendi ni wa aina tatu: Mashujaa wa kijadi wa kiafrika kwa mfano, Fumo Liyongo katika Utendi wa Fumo
Liyongo, mashujaa wa kidini kwa mfano, Mtume Muhammed na masahaba wake katika Utendi wa Ras‘lghuli na mashujaa wa kubuni kwa mfano Tajiri mbaya katika Utendi wa Masahibu.
Mtunzi anamtaja Fumo Liyongo kama jitu nene, lenye kimo kinachozidi cha mtu wa kawaida.
Kimo cha Fumo Liyongo kimeelezwa kwa kina, huku mtunzi akidhamiria kuweka wazi uwezo wa nguvu alizo nazo na umbo lake la kipekee. Alijulikana mno kwa unene wake kiasi cha kuwashangaza watu wengi. Watu walitoka mbali kuja kumtazama, kwani Vimo vyao vilimfikia magotini: (beti za 6 na 16).

  1. Liyongo kitaka,mali
    akabalighi rijali
    akawa mtu wa kweli
    na haiba kaongeya.
  2. Wagalla wakipulika
    kwa dhihaka wakateka
    wakanena “twamtaka”
    na sisi kumwangaliya. Mtunzi anaeleza alivyosafiri safari ya mbali kwa siku chache mno, hali ambayo ni tofauti na ya mwanadamu wa kawaida. Kwa mfano, aliwahi kutembea kutoka Shaka hadi jijini Pate, safari ya siku nne lakini yeye akachukua siku mbili tu. Liyongo ni mwenye vipaji kadhaa: Anawashinda maadui katika kulenga shabaha anapotumia upinde na mishale kuchuma mikoma bila kukwea mkomani.
    Juu ya yote alikuwa muungwana sana na mfano wa kuigwa na watu. Talanta inayojikeza hata zaidi ni, ufundi wa kutunga nyimbo na mashairi yaliyojulikana kama Gungu. Kwa mfano, akiwa kizuizini, aliitumia talanta hii kumtumia mamake ujumbe wa kishairi huku akiomba tupa ambayo aliitumia kukata minyororo ili kujiweka huru: (beti za 104 na 108).
  3. kama sada nakutuma
    Enda kamwambie mama
    Afanye mkate mwema
    Kati tupa aitiya.
  4. zilizo kikaza kusi
    alikikata upesi
    hata zikikoma basi
    inukani kawambiya.

Liyongo alikuwa hodari katika vita, aliwashinda maadui wake wote hata Wagala walishindwa vita na Liyongo. Vimo vyao vilimfikia magotini hali hivyo ikawawia vigumu kumshinda vitani.
Pia katika nguvu za kiakili, Liyongo alitumia akili kukataa kupanda mkomani ili aangue makoma(ubeti wa 65).

  1. Akawambia ngojani
    akatowa mkobani
    chembe katiya ngweni
    makoma kiwanguliya.
    Alikuwa na nguvu za kimwili yaani ubabe na mabavu, kama inavyodhihirika katika (beti za 40, 41, 46).

Pia, Liyongo likuwa na nguvu za kiakili na kivita. Liyongo alikuwa na uwezo wa kiakili, kuvumbua mambo mbalimbali na nguvu za kivita alikuwa nazo.Vilevile sifa ya uganga na sihiri, Liyongo ana sifa ya uganga. Hivyo alisema hawezi kudhurika kwa njia ya kawaida inayomdhuru mwanadamu yeyote. Kile ambacho kingemdhuru yeye ilikuwa siri ambayo aliifichua kwa mwanawe. Yaani nikwa kudungwa sindano ya shaba kitovuni: (ubeti wa 143)

Liyongo ana mshikamano na kundi au makundi ya watu. Aliishi porini na Watwa na kushirikiana nao. Ushirikiano wake ndio unaomnusuru na njama za mfalme za kutaka kmuua. Liyongo anapokufa watu wengi waliompenda wanaomboleza kwa masikitiko makubwa: (ubeti wa 224).

Vilevile kulikuwa na ushirikiano wa kifamilia kati ya Liyongo na mamake, ushirikiano huu unamsaidia kutoroka gerezani baada ya mamake kumpelekea mkate wa wishwa uliotiwa tupa ndaniye: (beti za 107, 110)

Nakwahivyo, utendi wa fumoliyongo unafunza hasa wanaume kuwa washujaa na wababe, rijali (ub 13), kukiimu mahitaji ya jamii na familia (ub 25), kuwa masihiri ( ub 143) na masuala hayo yana msingi ya kiume katika jamii ukizingatia nadharia ya ubabedume inayojikita katika kutambua na kuchunguza nafasi na majukumu ya mwanamume katika jamii ya waswahili.

Mambo kuhusu utamaduni katika utendi wa fumoliyongo;
Utamaduni ni jinsi binadamu anavyokabili maisha katika mazingira yake. Hivyo inajumlisha imani, ujuzi, sanaa, maadili, sheria, mila na desturi, ambavyo mtu anapokea kutoka jamii anamoishi.
Kama sifa maalumu ya binadamu inayomtofautisha na wanyama wengine, utamaduni ni suala la muhimu katika anthropolojia ukihusishwa na yale yote kama vile lugha inayowaunganisha watu wanaohusika, fasihi, mafungamano, ndoa, michezo, ibada, sayansi na tekinolojia (ustaarabu).
Utamaduni pia ni mkusanyiko wa maarifa, itikadi, na tabia za wanadamu ambazo hutegemea sana uwezo wa kuwasilisha mawazo na mafunzo ya kijamii kwa njia ya ishara.
Utamaduni ni jumla ya tabia za watu pamoja na akili, imani, sanaa, sheria, mila, dsturi, na tabia za watu wa waishio katika jamii moja.
Nakwahivyo, Utamaduni ni jumla ya mitazamo , kaida, malengo na maadili yanayotambulisha asasi, shirika, au kundi fulani la watu.
Ukilinganisha fasili hizo, utagundua kuwa utamaduni huwa ni tabia na mienendo ya watu wa jamii fulani.

Mambo kuhusu utamaduni katika utendi wa fumoliyongo yatagusia vipengele kama imani, mila, desturi, ndoa, lugha, michezo na burudani yapatikanayo katika utenzi huo huo. Yafuatayo ni baadhi ya mambo hayo;
Utendi wa fumoliyongo umeegemea utamaduni wa imaani ya dini ya uislamu. Utendi wa Fumo Liyongo, unatumia mianzo maalumu na kumalizia kwa miisho maalumu yenye dalili za dini ya kiislamu. Utendi huo umeanza kwa duwa na kumalizia kwa duwa. Duwa hiyo, anaombwa Mwenyezi Mungu Mmoja, ambaye ndiye Mwenye uwezo wa kila kitu. Aidha, katika duwa hizo, ametajwa Mtume Muhammad (S .A .W), ambaye ndiye Mtume wa mwanzo na wa mwisho katika ulimwengu huu. Kwa mfano, ubeti wa kwanza, kuna duwa:
Bismillahi nabutadi
Kwa ina la Muhammadi
Nandikie auladi
Nyuma watakaokuya
Kutokana na ubeti huo wa kwanza, Utendi wa Fumo Liyongo, mtunzi anaanza jina tukufu la Bismilahi, kisha, anamtaja Mtume Muhmmad (S.A.W). Hii ni desturi ya waumini wa Dini ya Kiislamu, ambapo, kila jambo, hulianza kwa mtajo wa Allah (S.W), yaani Bismi Llahi Rahmani Rahimi.
Vile vile, katika Utendi wa Fumo Liyongo, mtunzi anamalizia kwa kumuomba Mwenyezi Mungu (S.W), katika ubeti wa 228 na wa 229, ili akirimiwe, na AIlah (Mwenyezi Mungu). Mfano;

  1. Tumeziya kukhitimu
    Hapo ndio wasalamu
    Ilahi tatukirimu
    Kwa Baraka na afiya
  2. Rabbi tatusahiliya
    Na uzito wa duniya
    Tena tatujaaliya
    Kuwa njema yote niya
    Katika mifano hiyo hapo juu, mtunzi anamuomba Mwenyezi Mungu, Amuepushie uzito wa dunia. Pia, anamuomba Mola, Aifanye vyema niya yake. Mwenyezi Mungu, Ameoneshwa kuwa, ndiye Mwenye uwezo wa kila jambo kwa mja wake. Mifano hiyo inadhihirisha utamaduni wa imani ya dini ya uislamu katika utendi wa fumoliyongo.

Kuna utamaduni wa serikali ya utawala wa kifalme katika utendi wa fumoliyongo.
Inasemekana kuwa babake liyongo alikuwa mfalme wa pate na alipofarika, kakake liyongo ajulikanaye kama Daudi mrinngwari ndiye alilithi uongozi wa babake. Sultwani alikuwa mtawala wa Pate. Mwanzo alikuwa na mapenzi na Fumo Liyongo.
Hata hivyo, mwisho alijenga uwaduwi mkubwa juu ya Fumo Liyongo. Mtawala huyo, ndiye aliyefanya kila hila, ili amwangamize Liyongo;

  1. Mfalume kipulika
    Liyongo ametoweka
    Nde mui meanguka
    Haya aliazimia.
    Mfalme huyo alikuwa ni muuwaji.
  2. Fitina zikamngiya
    Mfalume miya miya
    Kwa hila kakusudiya
    Kumuuwa fahamiya.
    Beti hizo zinathibitisha serikali ya utawala wa ufalme katika utendi wa fumoliyongo.

Utamaduni unazingatia mfumo wa kuumeni.Tamaduni za waswahili zinamtaja Mwanamume kama Mkimu Jamii katika utenzi wa fumoliyongo. Hili linadhihirika na tukio la kikoa na makoma, Fumo Liyongo anapata usawiri wa kuwa mkimu jamii. Anajiunga na wanaume wenzake kukidhi hitaji la jamii la chakula. Wanashirikiana kutungua makoma kwa zamu.
Katika beti zifuatazo tunafahamishwa namna walivyounda kikoa ili kuhakikisha jukumu lao la kukidhia jamii linatekelezwa kwa utaratibu:

  1. Siku moya wakanena
    natuleni waungwana
    kikowa ni tamu sana
    karamu ‘sotindikiya
  2. Likisa shauri lao
    wakenenda kwa kikao
    mkoma waupatao
    hupanda mtu mmoya
    Doyle (1985:107) anadokeza kuwa mwanamume anapaswa kukimu familia kikamilifu kulingana na matakwa na matarajio ya jamii ya kiasili. Wanakikoa walitaka kutumia tukio la kuunda kikoa kwa nia mbaya ya kupata nafasi ya kumdhulumu Liyongo kwa kunuia kumwangamiza. Imebainika wazi kwamba, Liyongo ametimiza matakwa na matarajio ya jamii kuwa mkimu wa jamii akiwa mwanamume. Kwa hivyo, katika jamii ya kitamaduni ambayo huzingatia mfumo wa kuumeni, Liyongo ana hadhi na haki ya kudai nafasi yake kama mwanamume, hususan katika jamii ya Waswahili kwa sababu ametekeleza wajibu wake wa kukidhi jamii kama mwanamume. Asingepata tunuku la hadhi ya mwanamume pasipo kutimiza jukumu hili.

Utendi wa fumoliyongo umetumia lugha ya kiamu. Utendi huo umetumia lugha ya asili, kutokana na uasili wa kisa cha Fumo Liyongo.
Aidha, wanajamii, hiyo ndiyo lugha yao, waliyokuwa wakiitumia, na bado inatumika hadi leo katika eneo hilo. Beti za 14 na 50 zinadhihirishia misamiati ya lugha ya Kipate kama ifuatavyo:

  1. Ghafula kikutokeya
    Mkoyo hukupoteya
    Tapo likakuwiliya
    Ukatapa na kuliya
  2. Liyongo akatambuwa
    Huzengea kuuwawa
    Pale Pate kayepuwa
    Barani akitembeya.
    Beti hizo hapo juu, yaani ubeti wa 14 na 50, kuna matumizi ya maneno ya lugha ya Kiamu. Kwa mfano, katika ubeti wa 14, neno mkoya, lina maana ya mkojo, na neno “ukakuwilia,” lina maana ya “kutetemeka”. Aidha, katika ubeti wa 50, neno “kapepua” lina maana ya “akajiepusha”. (Mulokozi, 1999) anasema kutoka ubeti wa kwanza hadi 56 zimetumia lahaja ya kiamu.

Utendi wa Fumo Liyongo umetumia, kwa kiasi kikubwa, misamiati ya Kiswahili cha Kiamu kama beti

  1. kuwa liyongo mekwima
    Uko nde ya kisima
    Sasa watu wamekoma
    Mai hawapati ndiya.

Utamaduni katika utendi wa fumoliyongo unaheshimu muda wa michezo na burudani. Hili linadhihirika tunapoona fumoliyongo anaomba achezewe densi za gungu kabla ya kuuawa. kwamfano katika ubeti wa 98.
98. Akajibu “usikhini”
Kamwambie sulutwani
Mwao nieutamani
Na gungu liwe pamoya.

  1. Liyongo nikwambiao
    Shaha wa gungu na mwao
    Tena ni mkuu wao
    Huwashinda wut’e pia.
    Beti hizi zinaonyesha aina za nyimbo na burudani kama kipengele kimoja cha utamaduni katika jamii yao.

Mambo kuhusu uislamu katika utendi wa Fumoliyongo;
Utafiti unaonesha kuwa, Utendi wa Fumo Liyongo umebeba mambo ya dini ya Kiislamu wakati Utendi huo unapoanza kwa mtunzi kuomba duwa kwa Mweyezi Mungu mmoja na kumaliza kwa duwa. Nabii Muhammad (S.A.W), pia anasifiwa katika utendi huo.
Dua inatangulia maandishi ya utenzi wa fumoliyongo (ub 01) pia huwa ni njia mojawapo ya kuimarisha imani ya Kiislamu.Aidha kwa mujibu wa Koran tukufu, dua ni kigezo muhimu sana katika kuimarisha imani ya waumini wa dini ya kiislamu:
Kwa mfano;(ub 01)

  1. Bismillahi nabutadi
    Kwa ina la Muhammadi
    Nandikie auladi
    Nyuma watakaokuya
    Kutokana na ubeti huo wa kwanza katika Utendi wa Fumo Liyongo, mtunzi anaanza kwa jina tukufu la Bismilahi, kisha, anamtaja Mtume Muhmmad (S.A.W). Hii ni desturi ya waumini wa Dini ya Kiislamu, ambapo, kila jambo, hulianza kwa mtajo wa Allah (S.W), yaani Bismi Llahi Rahmani Rahimi.
    Vile vile, katika Utendi wa Fumo Liyongo, mtunzi anamalizia kwa kumuomba Mwenyezi Mungu (S.W), katika ubeti wa 228 na wa 229, ili akirimiwe, na AIlah (Mwenyezi Mungu). Mfano;
  2. Tumeziya kukhitimu
    Hapo ndio wasalamu
    Ilahi tatukirimu
    Kwa Baraka na afiya
  3. Rabbi tatusahiliya
    Na uzito wa duniya
    Tena tatujaaliya
    Kuwa njema yote niya
    Katika mifano hiyo hapo juu, mtunzi anamuomba Mwenyezi Mungu, Amuepushe na uzito wa dunia. Pia, anamuomba Mola Aifanye vyema niya yake. Mwenyezi Mungu Ameoneshwa kuwa ndiye Mwenye uwezo wa kila jambo kwa mja wake.
    Chittick na Murat (1994) vision of Islam, wanasema “Kuwa mwanadamu kamili ni kutekeleza matendo ya mungu alivyotenda.” Ni wazi kuwa maandishi yaliyomo, kwenye Koran yanatoa mwongozo wa maisha jinsi mwislamu alivyostahili kuishi. Aidha mandishi yanamtaja fumoliyongo kama kielelezo bora cha kuigwa hasa kwa waislamu.

Kuimarishwa kwa dini ya kiislamu; Matukio ya kushangaza katika Utendi wa fumoliyongo yamejengwa ili kuimarisha imani ya waumini wa Kiislamu.
Mwandishi anaonyesha adhabu mbalimbali ambazo watu wanapewa ilikulipia matendo yao maovu. Kwa mfano mtotowe liyongo alipomaliza kumsaliti babake na kumdunda shindano ya shaba, alifukuzwa mjini pate na mwishowe akakumbwa na madhabu yaliyomwangamiza. (ub 179

  1. Kamtiya kitovuni,
    Naye ulele kwa t’ani
    Achamka hamuoni
    Kiyana amekimbiya. 216, 213
  2. mfalme kabaini
    Kabisa huna imani
    Epuka mwangu matoni
    Na nyumbani nitokeya.
  3. mfalme kamtowa
    Nguo zakwe kamvuwa
    Na watu akatukiwa
    Khabari ikaeneya.)
    Hayo yote yanatokana matendo maovu.Tukio hili na mengine ni kama onyo kali kwa waislamu wasitende maovu ya aina hiyo.
    Kwa hivyo imani ya dini yaoinaimarika.Waislamu wana imani kuwa wanadamu wote wanaotenda kinyume na matakwa ya Allah wataadhibiwa vikali:
    Utetezi wa binadamu ni ishara ya matendo mazuri katika Koran na hadith. Fumoliyongo katumwa na nabii muhamed kama Mtume. Hili ni dhihirisho kuwa katika maisha ya sasa, Mungu huwateua watu wake ambao anawatwika kusimamia binadamu, kama vile,fumoliyongo. Mungu ana mamlaka ya kuchagua awapendao, na kuwapa majukumu yampendezayo. Liyongo ametumiwa kudhihirisha utukufu wa Mungu kwani Mungu hapendezwi na nyoyo chafu, za akina Daudi mringwari na mtoto wake liyongo aliyemsaliti.
    Nguvu za mwenyezi mungu pia ni somo hasa kwa waumini waisilamu; Matukio yanayomkumba Liyongo ni dhihirisho la nguvu za Mwenyezi Mungu. Kutokanana sifa tele za Fumoliyongo, tunatoa rai kuwa yeye ametumiwa kama mwongozo bora kwa waumini wote wa Kiislamu. Jukumu lake kuu ni kuwa kilelezo au mfano bora wa kuigwa kwa kila muumini kama watume.
    Wakatimwingine, utendi wa Fumoliyongo umekiuka matakwa ya dini tukufu ya uislamu, kinyume na mafundisho ya hadith na koran tukufu kama;
    Matendo ya Sultan wa pate Bw Daudi mringwari kakake Fumoliyongo ya kumpangia njama za kumwangamiza Liyongo yanayodhihirishwa na mwandishi katika utenzi wa fumoliyongo (beti 87, 71,53) yanakiuka na kuvuka mipaka na kuvunja sheria za hadith pamoja na Koran tukufu. Mtume Mohamed(SAW) Alikuja kuokoa watu kuhubiri utendaji mazuri kwa wengine sio kutenda maovu, kwamfano
  4. Mfalme kawambiya
    ‘‘Liyongo kunipatiya
    Kitwa mukanieteya
    T’awapa riale miya’’
  5. Mwambieni tusafiri
    Hata pate tukajiri
    Hapana tena khatari
    Habari tumesikiya.
  6. Akatiwa gerezani
    Kafungiwa kijumbani
    Asikari mlangoni
    Kwa zamu wakachangaliya.
    Mipango hiyo yote inayooneshwa kwenye beti hizi yanakiuka matakwa ya mtume muhamadi kutendea watu maovu.
    Pia, tendo la kumuoza liyongo kiholela na mke wa kigalla linakiuka mipaka ya ndoa katika dini ya kiislamu ambapo muislamu anapaswa kuozwa kirasmi na kiongozi wa msikiti. (ubeti 45
  7. Sharuti wakatimiza
    Liyongo wakamuoza
    Kwa furaha na kuteza
    Nyumbani akaingiya.
  8. mke katukuwa mimba
    Akazaa mwane simba
    Mwanamume wa kutamba
    Mwane liyongo sikiya.
    Tendo la mtoto wa liyongo la kumsaliti kwa kumdunda sindano ya shaba na kumuua haliambatani na mafundisho ya dini ya kiislamu. (ubeti 179)
  9. kamtiya kitovuni
    Naye ulele kwa t’ani
    Achamka hamuoni
    Kiyana amekimbiya.
    Mungu hapendezwi na nyoyo chafu, za akina Daudi mringwari na mtoto wake liyongo aliyemsaliti. NakwahivyoWaislamu wana imani kuwa wanadamu wote wanaotenda kinyume na matakwa ya Allah wataadhibiwa vikali.

Katika utenzi wa Fumoliyongo, kuna maswali ambayo pengo halijazibika ama hakika haikutambulika wazi kama;


Muhamad kijumwa aliandika kuhusu utenzi wa Fumoliyongo kutokana na wenyeji wa mwambao wa Kenya, je matendo ya liyongo ni ya kweli au mwandishi kaongeza utamu kwa kuweka zaidi ya aliyoambiwa?
Hadithi inaanza kwa kutuelezea kuwa liyongo alikuwa anaishi mwituni hata kabla ya kuwa na ugomvi na kakake mringwari, je kama mtoto wa kifalme kwanini aliamua kuishi mwituni na wadahalo pamoja na makabila mengine sio pate kwenye Ufalme, huenda ulikuwa uongo?
Hatimaye, nakamilisha mjadala huu kwa kusema, uchunguzi zaidi kuhusu maisha na matendo ya liyongo unahitajika kwa kutembelea hasa panaposemekana kuwa aliishi halafu historia yake ikagunduliwa rasmi na wenyeji.

Islamic morals

Morality in Islam encompasses the concept of righteousness, good character, and the body of moral qualities and virtues prescribed in Islamic religious texts.(Hadith and Quran)

The principle and fundamental purpose of Islamic morality is love ie love for God and love for God’s creatures.

The religious conception is that mankind will behave morally and treat each other in the best possible manner to please God.

Teachings on morality and moral conduct constitute a major part i eIslamic literature. The Quran and the Hadith which are referred to as the central religious texts of Islam and serve as the primary source for these teachings.

Both the Quran and the hadith often instruct Muslims to adopt a morally upright character.ie

1.Showing kindness to people and charity to the poor and the helpless are the most emphasized moral virtues in the Quran.

2. Helping people in their time of need.

3. Forgiving others’ offenses.

4. Respecting parents and elders.

5. Fulfilling promises.

6. Being kind to people and to animals.

7. Being patient in adversity.

8. Maintaining justice.

9. Being honest.

10. Controlling one’s anger appear as major virtues in the Islamic concept of morality.

Alfabeti ya kiswahili

Tafsiri.

Whenever Mr. Brown went to that village, he spent long hours with Akunna
in his obi talking through an interpreter about religion. Neither of them
succeeded in converting the other but they learnt more about their different
beliefs.
“You say that there is one supreme God who made heaven and earth,” said
Akunna on one of Mr. Brown’s visits. “We also believe in Him and call Him
Chukwu. He made all the world and other gods.”
“There are no other gods,” said Mr. Brown. “Chukwu is the only God and all
others are false. You carve a piece of wood – like that one” (he pointed at the
rafters from which Akunna’s carved Ikenga hung), “and you call it a god.
But it is still a piece of wood.”
“Yes,” said Akunna. “It is indeed a piece of wood. The tree from which it
came was made by Chukwu, as indeed all minor gods were. But He made
them for His messengers so that we could approach Him through them. It is
like yourself. You are the head of your church.”
“No,” protested Mr. Brown. “The head of my church is God Himself.”
“I know,” said Akunna, “but there must be a head in his world among men.
Somebody like yourself must be the head here.”
“The head of my church in that sense is in England.”
“That is exactly what I am saying. The head of your church is in your
country. He has sent you here as his messenger. And you have also
appointed your own messengers and servants. Or let me take another
example, the District Commissioner. He is sent by your king.

Wakati wowote Mheshimiwa Brown alipokwenda kijiji hicho, alitumia muda mrefu na Akunna katika Obi yake akizungumza kupitia mkalimani kuhusu dini. Wala wao hawakufanikiwa kugeuza wengine lakini walijifunza zaidi kuhusu imani zao tofauti. “Unasema kuwa kuna Mungu mmoja mkuu ambaye aliumba mbingu na dunia,” alisema Akunna juu ya moja ya ziara za bwana Brown,. “Pia tunamwamini na kumwita Chukwu. Aliumba ulimwengu wote na miungu mingine. “”

Hakuna miungu mingine, “alisema Bw Brown. “Chukwu ndiye Mungu pekee na wengine wote ni wa uongo. Unavaa kipande cha fimbo – kama kile “(aliashiria kwenye fimbo  Akunna alilofanya kutoka mbao  Ikenga hung.),” na unamwita Mungu. Lakini bado ni kipande cha fimbo.

“” Ndiyo, “alisema Akunna.
“Ni kweli ni kipande cha fimbo, alisema Akunna. Mti huo uliumbwa na Chukwu, kwa kweli miungu yote wadogo walikuwepo. Lakini chukwu akatuma wajumbe wake ili tuweze kumkaribia kuwapitia . Ni kama wewe mwenyewe. Wewe ni kichwa/mjumbe wa kanisa yako. “”

“Hapana”, “alipinga bwana Brown. “Mkuu wa kanisa langu ni Mungu mwenyewe.”

“Najua,” alisema Akunna, “lakini lazima pawepo mkuu wao katika ulimwengu miongoni mwa wanadamu. Mtu kama wewe mwenyewe lazima awe mkuu hapa. “”

Mkuu wa kanisa langu kwa maana hiyo Yuko Uingereza. “”

Naam, hayo maneno ndiyo ninayosema na maana ndio hiyo. Mkuu wa kanisa lako Yuko nchini mwako. Amekutuma hapa kama Mtume/mjumbe wake. Na pia umewaweka wajumbe wako na watumishi wako. Au napenda kuchukua mfano mwingine, Kamishena wa Wilaya. Yeye anatumwa na mfalme wako.

jifunzekiswahili.art.wordpress.com.

Kidato Cha kwanza

WATU WA NYUMBANI.
1.  Baba-Father.
2. Mama-Mother
3. Mjomba-Uncle.
4. Dada-Sister.
5. Kaka- Brother.

Kutunga sentensi kwa kumtumia msamiati wa watu was nyumbani.(Construction of Sentences Using Vocabulary of Home people.)

i,. Baba yangu ni dereva wa basi.
(My father is a bus driver)

ii. Mama yangu ni mwalimu wa Kiswahili.
(My mother is a kiswahili teacher.)

iii. Dada yake Peter anafundisha katika Chuo Kikuu cha Kyambogo.
(Peter’s sister teaches at Kyambogo University.)

iv.  Kaka yangu anasomea katika Chuo cha walimu cha Kabale. (My brother studies at National teacher’s college Kabale)

v. Tafadhali niitie yule kaka yangu.
(Please, call me my brother)

vi.Dada yako anaitwa nani?
(What’s the name of your sister?)

arigumaho810@gmail.com
Jifunzekiswahiliart.wordpress.com
Arigumahop5.(Twitter)
0778514179(WhatsApp)

Hisabati na Tarakimu
Msamiati wa hesabu/hisabati unaangazia: majina mbalimbali ya tarakimu/nambari; kuandika tarakimu kwa herufi.maneno; tarakimu za kiarabu; akisami (fractions) na asilimia (percentages).

Tumekuandalia:
Nambari za Kimsingi (0-9) Kiswahili na Kiarabu
Kumi na (11-19) Kiswahili na Kiarabu
Makumi/Ukumi (10-90)
Akisami (fractions)
Mifano Kadhaa
NAMBARI ZA KIMSINGI
Haya ni majina ya tarakimu mbalimbali zinapoandikwa kwa herufi (badala ya nambari) yenye asili ya Kiswahili/Kibantu na pia yale yenye asili ya Kiarabu. Pia, tumeongezea majina ya makumi mbalimbali (10-90)
TARAKIMU KISWAHILI KIARABU
0 sufuri sufuri
1 moja wahed
2 mbili thenini
3 tatu thelatha
4 nne aroba
5 tano hamsa
6 sita sita
7 saba saba
8 nane themania
9 tisa tisa
KUMI NA
Majina ya ya tarakimu kutoka (11-19) kwa Kiswahili na kwa Kiarabu.
10+ KISWAHILI KIARABU
11 kumi na moja edatashara
12 kumi na mbili thenashara
13 kumi na tatu thelathashara
14 kumi na nne arobatashara
15 kumi na tano hamsatashara
16 kumi na sita sitatashara
17 kumi na saba sabatashara
18 kumi na nane themantashara
19 kumi na tisa tisatashara
MAKUMI
Kuandika tarakimu mbalimbali katika hali ya ukumi. (11-99).
*10 JINA MFANO
# KISWAHILI KIARABU
10 kumi 12 kumi na mbili thenashara
20 ishirini 27 ishirini na saba saba wa ishirini
30 thelathini 32 thelathini na mbili thenini wa thelathini
40 arobaini 42 arobaini na mbili thenini wa arobaini
50 hamsini 52 hamsini na mbili thenini wa hamsini
60 sitini 61 sitini na moja wahed wa sitini
70 sabini 76 sabini na sita sita wa sabini
80 themanini 89 themanini na tisa tisa wa themanini
90 tisini 93 tisini na tatu thelatha wa tisini
AKISAMI
Akisami hutumiwa kuonyesha sehemu ya kitu kizima. Kwa mfano, ukigawa kilo moja kwa visehemu vinne vinavyotoshana, kila kisehemu kitakuwa na uzani wa robo kilo ( sehemu ya nne au moja kwa nne ) ya kilo.
1/# JINA MFANO
1/2 nusu 1/2 nusu moja kwa mbili
1/3 thuluthi 2/3 thuluthi mbili mbili kwa tatu
1/4 robo 2/4 robo mbili mbili kwa nne
1/5 humusi 3/5 humusi tatu tatu kwa tano
1/6 sudusi 4/6 sudusi nne nne kwa sita
1/7 subui 6/7 subui sita sita kwa saba
1/8 thumuni 7/8 thumuni saba saba kwa nane
1/9 tusui 3/9 tusui tatu tatu kwa tisa
1/10 ushuri 6/10 ushuri sita sita kwa kumi
1/100 asilimia 72/100 asilimia sabini na mbili sabini na mbili kwa mia moja
MIFANO ZAIDI
Andika nambari zifuatazo kwa maneno/herufi:
3 – tatu
952 – mia tisa hamsini na mbili
680 – mia sita themanini
4521903 – milioni nne, na mia tano ishirini na moja elfu, na mia tisa na tatu
556100016 – mia tano hamsini na sita milioni, na mia moja elfu, na kumi na sita
Andika tarakimu zifuatazo kwa nambari
sufuri – 0
mia tatu ishirini na mbili – 322
sabini na tatu elfu, na mia nane hamsini na tano – 73855
mia tano sabini na nane elfu, na mia tatu hamsini na tisa – 578359
mia sita tisini na sita milioni, na mia tisa tisini na nane elfu, na mia saba ishirini na tatu – 696998723
Andika akisami zifuatazo kwa maneno

Ulimwengu wa kiswahili unavutia.@Chawakama Conference Kyambogo University 2019 Kampala-Uganda” on YouTube

Wakereketwa.

ELIMU NA MAISHA MTAANI.

USINGOJEE UGANDA MPYA au FULANI KUKULINDIA KESHO YAKO
.Hii ni makala maalum kwako wewe mhitimu mpya. Nakuandikia makala hii katika kipindi ambacho vyuo vingi nchini UGANDA vitakuwa katika msimu wa mahafali au graduation wakti mchache mbele hapo. Ni kipindi cha furaha kubwa kwako, na kwa ndugu, marafiki na walimu wako pia. Kifupi, hiki ni kipindi muhimu sana kwako, ambapo unavuka rasmi mstari unaotenganisha maisha ya chuo na maisha halisia nje ya darasa.

Katikati ya furaha hii, ukiwa unasheherekea kumaliza chuo na kutunukiwa cheti, stashahada, shahada ya kwanza au shahada ya uzamili, usije ukajisahau. Unapaswa kukumbuka kuwa sasa ndio unaingia rasmi kwenye ‘maisha halisia’. Ndio, una shahada, lakini hicho unachopewa mkononi ni kipande cha karatasi tu ‘kinachovutia’. Usipoweza kukibadilisha kuwa pesa kitabaki kikaratasi tu, na hakitakuwa na maana.

Juzi juzi katika gazeti moja la nchi jirani limekutana na maoni ya msomaji mmoja wa gazeti hilo yakisema, “mimi kama mmoja wa wahitimu wa chuo kikuu, BISHOP STUART wakati fulani nawaona watoto wamevalia sare zao nzuri wanaenda shule…najiuliza hivi hawa wanasoma ili waende wapi…wakati mimi nazunguka na vyeti vyangu kutoka ofisi moja kwenda nyingine mjini humu Kampala wala sijaiona hiyo ajira”.

Hapa Uganda pia katika mtandao mmoja nimekutana na bango lililobebwa na kijana mmoja likiwa limeandikwa, “ndugu zangu WanaUganda naombeni ajira…ni mimi mwalimu wa kiswahili (mtaalamu wa lugha na fasihi) ambaye sina mtu wa kunishika mkono.” Huyu ni mmoja wa vijana wengi wanaomaliza vyuo, wanaingia mtaani kutafuta kazi. Je unajua mtaani kukoje?b

Lengo la makala hii ni kukutaarifu wewe mwanachuo unayeingia mtaani, kuwa ajira (kuajiriwa) kwa sasa zinazidi kuadimika. Hii inatokana na idadi ndogo ya ajira zinazozalishwa katika uchumi kupitia sekta binafsi na sekta za umma…ikilinganishwa na idadi ya wanafunzi wanaoingia katika soko la ajira kila mwaka. Vilevile nakusudia kutoa maoni ya nini cha kufanya.

Kimsingi kuna changamoto kubwa inayowakabili vijana wengi kwa sasa. Ni changamoto ya ukosefu wa ‘ajira rasmi’ serikalini, katika mashirika ya umma/binafsi, au katika taasisi zingine. Na kwa kuzingatia hili ndio maana tunasema ni wakati sasa vijana wetu wajitambue, na wayajue mazingira yalivyo sasa ki-uhalisia ili wachukue hatua stahiki.

Hapa kuna vitu kadhaa vya kujadili. Wakati fulani unaweza kuinyooshea kidole serikali, kwa kushindwa kuwa na mikakati ya kuzalisha ajira katika uchumi. Tena unaweza kuwanyooshea kidole wazazi, kwa kuwasisitizia watoto njia moja tu, ya elimu ya darasani, kama msingi wa maisha yao. Au unaweza kuinyooshea kidole mitaala ya vyuo, au walimu, kwa kushindwa kuwapa watoto stadi za maisha nje ya darasa.

Kutokana na hayo, ni muhimu sasa kuzingatia kuwa, pamoja na maarifa ya darasani, watoto wajifunze pia maarifa nje ya darasa, yaani wayajue maisha halisi, ya mtaani. Haya ni maisha ya kutumia akili na ubunifu binafsi…na yakichanganywa na yale ya darasani, mseto unaopatikana una tija kubwa.

Mwandishi Scott Berkun anaandika kwamba kuna aina mbili ya watu ‘smart’ (wenye akili). Kuna Book Smart na Street Smart . Anasema book smart ni mtu mwenye akili au maarifa mengi ya darasani. Kwa bahati mbaya haya ni maarifa yaliyochaguliwa na watu fulani, kwa lengo lao fulani. Wanampatia mtu maarifa haya kwa kiasi na utaratibu fulani, ili akifaulu awafanyie kazi yao fulani kwa utaratibu fulani, halafu wanamlipa mshahara fulani.

Mhitimu huyu akiajiriwa anafanya kazi kwa miongozo maalum (rules, theories au principles) aliyofundishwa. Huyu akipata tatizo, haraka anakimbilia kusoma miongozo inasemaje, na anaifuata hiyo ili kutatua tatizo. Anapofikiria kupanda cheo anaomba kwenda kusoma shahada ya juu zaidi ambako anafundishwa theories na principles mpya ili azitumie akiwa katika nafasi ya juu kazini.

Watu ambao ni book smart , hupenda sana kijiendeleza kielimu kwenye fani zao, na wengi ni wazuri sana darasani, na ndio maana baadhi ya waajiri huwatafuta hawa inapotokea nafasi ya kazi. Tatizo la hawa, wasipoajiriwa, hawana plan B, na hii huwachanganya sana. Hawa huwa hawana macho ya kuona zaidi ya ‘upeo wa ajira’. Hawazioni fursa na wakitokea kuoneshwa hawana ujasiri wa kupambana.

Kwa upande mwingine kuna street smart. Hawa ni wale vijana ambao wanaweza kuwa na elimu ndogo tu, lakini wana maarifa ya ziada kichwani. Haya ni maarifa ya nje ya darasa. Watu hawa wana uwezo mkubwa wa kujenga fikra bunifu (imaginations), na kuziona fursa. Hawa wana ujasiri/uthubutu wa kuanza na kupambana ili kuyatafsiri mazingira yao kuwa kipato.

Maisha ya vijana hawa huwa hayana kanuni maalum wala hayaongozwi na principles – bali ujasiri na uthubutu. Vijana hawa, kwa kutumia fikra bunifu, wana uwezo wa kuanzisha biashara yoyote…wakaongeza kitu juu ya biashara hiyo…au wakapunguza, kulingana na mazingira yalivyo, na kwa kufanya hivi wakajitengenezea kipato kizuri kwa ajili ya maisha yao.Sasa jichunguze mwenyewe, hivi wewe ni book smart au street smart?

Ukiichunguza mitaala ya elimu yetu utaona kuwa bado ina misingi ile ile ya kikoloni – yaani kuwaandaa vijana wachache, kwa kuwapa elimu ya darasani inayolenga kuwapatia wahitimu maarifa yanayotakiwa katika kufanikisha shughuli zao za kiutawala, na siyo kuwapa maarifa ya kuwawezesha kujitegemea.

Kwa hiyo hata sasa vijana wanaendelea kuamini katika hili – kwamba wanasoma ili waje kuajiriwa. Kwa aina hii ya mtaala kijana akimaliza chuo anabaki na elimu ya darasani tu. Hana maono…hana fikra bunifu…hazioni fursa na hivyo hawezi kujiajiri. Huyu asipoajiriwa anaona huu ndio mwisho wa dunia!

Sisemi kwamba kujiajiri ni kitu rahisi, hapana, sio rahisi na kuna changamoto nyingi, hasa kwa wanaoanza, na hasa wanaotoka katika chungu cha taaluma, vyuoni. Kuna suala la mtaji, ushindani katika soko, uzoefu mdogo wa biashara, na uwezekano wa kupata hasara kwa kile unachokifanya.

Wala sijasema maarifa ya darasani sio muhimu, la hasha. Ninachosema ni kwamba kila mtu ajitahidi kupata elimu ya darasani, lakini wakati unaingiza maarifa haya usisahau kuwa kuna maarifa mengine muhimu pia nje ya darasa. Ukiwa na maarifa haya unakuwa na balance nzuri katika maisha, na utaepuka kuwa tegemezi wa ajira pekee.

Vijana wenye maarifa nje ya darasa utawaona jinsi ‘wanavyochacharika’ na kujaribu kila kinachowezekana. Hawa huwa hawaoni haya, hawaogopi jua, vumbi wala mvua. Vijana hawa hawachagui kazi – wao kilicho muhimu kwao ni kipato halali na matamanio ya ‘kutoboa’. Hawa si watu waoga, ni watu wenye ujasiri na uvumilivu.

Vijana hawa utawaona wakikaanga chips , samaki, chapati, pan au mihogo na kuitembeza mitaani. Wengine utawaona wakiuza juisi za miwa na wengine wakitengeneza sabuni na viungo vya mboga. Utawaona wengine wakilima bustani za mboga na wengine wakipamba maharusi na kupika vyakula vya sherehe, ili mradi kila mmoja anaingiza kipato na kuendesha maisha yake.

Wengi wa vijana hawa hawana vyeti vya kitaaluma kutoka vyuoni, wanatumia uzoefu wao wa maisha ya ‘kitaa’. Sasa wewe ‘msomi’ ukiingia mtaani na majivuno yako ya vyeti vya stashahada au shahada, utabaki unashangaa! *Wakati unamaliza soli za viatu ukizunguka na bahasha yako ya kaki, au ukijibizana na wadogo zako mkigombea remote ya TV, ukisubiri msosi, vijana hawa wako mtaani wakiingiza. pesa

Ni aibu kwa msomi wa chuo kikuu kuwa tegemezi kwa wazazi au ndugu zako. Tena wapo wasomi ambao hawana hata aibu, huwasumbua vijana waliowaacha mtaani, ambao wengine ni darasa la saba tu, wakiwaomba hadi hela ya nauli, kwenda mjini kampala kutembea kupeleka barua zao za maombi Shule fulani Kibuli🤦‍♀️🤦‍♀️, kampuni fulani Namanve😅😅 , Jibunie ndugu….

Msomi usieweza kuziona fursa na kuzichangamkia, wewe ni msomi butu. Unazidiwa na kijana wa darasa la saba, halafu unajitutumua hapa…! Mimi nilipata shahada ya uzamili MAKERERE halafu inabaki huko Kikoni ukila vikomando na kutisha mawe kwenye magari ya rais KYAGULANYI😂😂😅😅Hivi maana ya elimu ni nini? Elewa usomi sio vyeti, ni uwezo wa kutengeneza vitu au thamani katika jitihada za kujitengenezea kipato.

Hatua ya kuchukua: kijana unaliyemaliza chuo na sasa unafanya mahafali una kitu muhimu cha kujifunza. Kitu hicho ni kujitambua. Tambua kwamba wewe ni msomi, na una maarifa, lakini kwa mfumo wetu wa elimu, bado unatakiwa kujiongeza. Jiepushe na kushupaza shingo kwa kufikiria ajira peke yake…kwani ajira hazipo za kutosha sokoni. Unapaswa kuelewa kuwa watu wanakwenda shule ili kupata maarifa, siyo kazi. Kazi ikitokea… sawa!

Ile kasumba inayokumbatiwa na wazazi wengi, kwamba mwanangu nakupeleka shule/chuo kizuri, soma kwa bidii ‘masomo ya maana’ ili ufaulu vizuri mitihani, upate alama za juu, baadaye kidogo utaajiriwa na kampuni nzuri, na utalipwa mshahara mkubwa, imepita! Hali imebadilika sasa. Ndio maana tunahimiza vijana wajifunze stadi za maisha ili wawe na mbinu mbadala za kupambana na kujitengenezea kipato bila kusubiri ajira.
Eti Mimi namungojea kunilindia kesho😂😂
Angalia Uganda mpya tu✊🏾✊🏾

jifunzekiswahiliart.wordpress.com
Uyaache yasiyokuhusu.

arigumaho810@gmail.com

RAIS MUSEVENI NDANI YAKE.

Yoweri Kaguta Museveni (* 1944 Ntungamo, Wilaya ya NtungamoUganda) ni Rais wa Uganda tangu 29 Januari 1986. Alichukua madaraka baada ya kushinda vita vya msituni chini ya kundi la National Resistance Movement na kushinda katika chaguzi za urais za mwaka 1996, 2001 na 2006.

Yoweri Museveni, 2015

Kwa muda mrefu, kabla ya kuwa rais wa Uganda, Museveni aliongoza vita vya msituni dhidi ya serikali za Idd Amin aliyetawala toka mwaka 1971-79, na serikali ya Milton Obote aliyekuwa madarakani mwaka 1980-85.

Kutokana na mafanikio ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi na kukubali kwake kufuata sera za Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani, Museveni alipata sifa kubwa toka kwa viongozi wa mataifa ya Magharibi. Mwishoni mwa miaka ya 1990, Museveni alikuwa akielezewa kuwa ni mfano bora wa kizazi kipya cha viongozi wa Afrika.

Hata hivyo uongozi wake umetiwa dosari na mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na ushiriki wake katika vita vya wenyewe kwa wenyewe katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda. Mambo mengine ni pamoja na ukiukwaji wa haki za kisiasa unaofanywa na serikali yake dhidi ya wapinzani kama vile Kizza Besigye , Bobiwine na wengine na kitendo cha kubadili katiba ya nchi hiyo ili aweze kugombea urais mwaka Hadi kifo.

DHANA YA JAMII LUGHA

Kwa mujibu wa Mekacha (2011) dhana ya jamii lugha imetafsiriwa kwa mitazamo mbalimbali, hata hivyo wataalamu wengi wanakubaliana na maana ya jumla kuwa jamii lugha ni watumiaji wa lugha wanaoishi katika eneo moja ambao hubainishwa kwa mahusiano yao ya kuendelea kutumia aina fulani ya lugha tofauti na watumiaji wengine wa lugha hiyohiyo.

Licha ya fasili hii kuonekana kuwa ni rahisi kueleweka, bado ina utata katika kupata data wakati wa uainishaji wa wazungumzaji wake na uchanganuzi wa data za isimujamii.

Utata huu unajibainisha katika mambo yafuatayo;

i. Kujua mahali ambapo mipaka ya watumiaji wa lugha inaanzia na kuishia na kama inawezekana kukawa na mipaka ya eneo moja la jamii lugha isiyoingiliana na mipaka ya eneo lingine.


ii. Uwezekano wa wazungumzaji wa lugha katika jamii lugha moja, kuzungumza lugha moja au zaidi. Je, wanatumia lahaja, lugha sanifu, misimu, lafudhi au wanatumia lugha zote?


iii. Vigezo vinavyotumika kuwabaini au kuwaainisha watumiaji wanaopatikana katika jamii lugha moja na kuwafanya waonekane kuwa wa jamiilugha husika.Maswali haya na mengine mengi yanaifanya tafsiri ya dhana ya jamiilugha ionekane kuwa ni tata kinadharia na kiutendaji.

Tutatumia misingi mitatu ili kuifahamu dhana ya jamiilugha:

i. Msingi wa kutumia lugha
Imezoeleka katika jamii nyingi lugha kutumika kama nembo ya jamii fulani ambapo watu wanaotoka au wanaopatikana katika jamii fulani hutambulishwa kwa lugha yao. Mfano tunaweza kupata lugha ya Kiswahili (Waswahili), Kichaga (Wachaga), Kiingereza (Waingereza), Kijaluo (Wajaluo), Kikalenji (Wakalenji) nakadhalika.Katika utambulisho huu jamii au taifa linalotumia lugha moja ndilo linalopewa lugha moja. Kunapokuwa na matumizi ya lugha zaidi ya moja taifa au jamii husika haitambulishwi kwa Lugha, kwa mfano hutuwezi kuwa na jamiilugha ya Watanzania, Wakenya, Waghana, waganda nakadhalika. Jamii hizi huwa ni muktadha halisi wa matumizi ya lugha na si mtu mmojammoja kwa vile lugha ni mali ya jamii.Hii ni kusema, Jamiilugha hujidhihirisha katika mawasiliano ambayo hufanikiwa katika misingi ifuatayo;
 Kuelewana kwa wazungumzaji wa lugha miongoni mwao kunatokana na wazungumzaji wenyewe kuwa ni zao la jamii moja
 Watumiaji wa jamiilugha moja huelewana kiurahisi kwakuwa wanazielewa kanuni na taratibu za mawasiliano zinazotumiwa na watumiaji lugha wote
 Wazungumzaji wa lugha hiyo huwa na ujuzi na uzoefu wa muda mrefu wa kutumia lugha hiyo kwa nia ya kurithishana.Kwa mantiki hii, lugha ndio inayojiwekea mipaka ya jamiilugha. Mipaka huanzia na kuishia mahali lugha inapoishia. Tatizo la mtazamo huu ni kuwa kwanza, kuwepo kwa baadhi ya watu kuanza kutumia lahaja tofauti, Pili kunakuwa na matumizi ya lugha zaidi ya moja na hivyo kuwa vigumu kupata jamiilugha kirahisi kwasababu kunapotokea jamii zaidi ya moja kila jamii hujiona bora kuliko nyingine.ii. Msingi wa kutumia mahali/Eneo
Watu wanaounda jamiilugha moja wanakaa katika eneo moja lenye mipaka mahsusi ya kijeografia. Wanassosholojia hutumia msingi wa mahali katika kubaini jamiilugha. Huamini katika msingi kuwa, watu wanapokuwa katika eneo moja kwa muda mrefu hujiundia kanuni na taratibu zao za namna ya kuishi, yaani mila na desturi. Watu hawa hujiwekea mipaka yao ili kujitofautisha na jamii nyingine, mipaka hii yawezakuwa milima, mabonde, mito, misitu minene nakadhalika. Mipaka hii ya kijeografia huheshimiwa daima na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Hivyo, ili kujua jamiilugha wataalamu wa lugha hawana budi kutumia misingi ya mahali mahali na lugha kuibaini jamiilugha kwakuwa ni vitu vinavyotegemeana na kukamilishana.iii. Msingi wa makubaliano wa kimazoea.
Ni msingi unaohusu jamiilugha ndogondogo ndani ya jamiilugha kubwa katika eneo fulani. Jamiilugha hizi zaweza kuwa za wafanyakazi wa kampuni fulani, wanafunzi, wanachuo, wafanyabiashara, vijana, jinsia fulani nk. Msingi wa makubaliano ya usemaji unatokana na mazoea ya muda mrefu kutokana na kuwa pamoja katika shughuli au mahali fulani. Tatizo la jamiilugha za aina hii ni utata katika kupata idadi halisi ya jamiilugha kutokana na kukosa ukomo. Hii inatokana na ukosefu wa mipaka dhahiri ya jamiilugha moja na nyingine kwa kuwa mtu mmoja anaweza kujibainisha katika jamiilugha zaidi ya moja. Mfano, mtu kuwa mfanyabiashara, mwanafunzi na vilevile mfanyakazi wa bandarini. Msingi huu unaelekea kuwa si imara.

MAKUNDI YA JAMIILUGHA.

1. Jamiilugha zinazotumia lugha moja
Ikiwa jamiilugha inatumia lugha moja, basi jamiilugha hiyo inasemekana kuwa yenye kutumia lugha moja (Monolingual speech community). Lugha hii hutumika katika maeneo yote ya matumizi ya lugha, maeneo rasmi ya utawala na serikali na yasiyo rasmi ya matumizi ya lugha kama vile majumbani katika kiwango cha familia na mtu na mtu. Wanajamii wote wandhaniwa kuielewa na kuitumia lugha husika kiufasaha katika shughuli zao za kila siku.Hata hivyo,

katika karne ya leo ambapo kuna maingiliano na mawasiliano bora zaidi miongoni mwa wanajamii duniani ni vigumu kupata jamiilugha yenye kutumia lugha moja tu katika mawasiliano yake.

Ugumu huu unatokana na maingiliano kupitia njia mbalimbali kama uhamiaji, utalii, elimu, dini, ndoa, ukimbizi, mawasiliano ya kimtandao nk.

Vilevile hata katika jamiilugha yenye kutumia lugha moja bado kunaweza kutokea suala la tofauti za kilahaja.

Kwa upande mwingine watumiaji lugha wa mipakani hulazimika kujifunza lugha nyingine zaidi kutokana maingiliano ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni na watu kutoka katika jamiilugha wanayopakana nayo. Hii inawafanya wawe na lugha mbili tofauti (jamiilugha uwili) kwa wakati mmoja..Kimsingi dhana ya jamiilugha inayotumia lugha moja ilikuwepo kwa nchi za Afrika mashariki kabla ya ujio wa wakoloni ambapo kila jamii ilitumia lugha moja.

Kwamfano chini Uganda, kulikuwa Wanyankore, waganda, wakonjo, waluo, wateso na kabila nyingine…kwahivyo, lugha hizi ziliathiriwa na lugha za wakoloni. Hivyo kukazuka na mataifa makubwa zaidi kama ya Kenya, Tanzania na Uganda. Hapo ndipo muingiliano ukawa mpana zaidi.

2. Jamiilugha Uwili
Ikitokea katika jamii kuwa na matumizi ya lugha mbili kwa wakati mmoja tunaweza kusema jamii husika ni jamiilugha uwili. Kigezo kinachotumika ni idadi ya lugha zinazotumika. Inawezekana kupata jamiilugha uwili katika mazingira ya Tanzania ambapo watu wanaweza kuzungumza lugha ya Kiswahili na wakati huohuo wanazungumza lugha mojawapo kati ya lugha za asili. Hata hivyo, kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, mtu mmojammoja wanajua lugha zaidi ya mbili. Kiswahili, Kiingereza/ Kifaransa, Lugha ya/za asili nk.3. Jamiilugha Ulumbi
Katika mzingira ya kawaida kwa watanzania kuna wakati wazungumzaji humudu lugha zaidi ya mbili. Mfano, mtu anaweza kuzungungumza lugha moja au zaidi kati ya lugha za asili, Kiswahili na lugha moja au zaidi. Mfano, anaweza kujua lugha ya Kinyakyusa, Kisafwa, Kiswahili na Kiingereza hivyo kujua lugha nne. Mwingine anaweza kujua lugha moja ya asili mfano Kisukuma, Kigogo na Kiswahili tu na akawa anajua lugha tatu nk. Hivyo, idadi ya lugha katika jamiilugha ulumbi hutofautiana kati ya mtu na mtu na jamiilugha na jamiilugha. Vilevile ikumbukwe kuwa kiwango cha umahiri katika lugha anazojua mzungumzaji si lazima kiwe sawa. Kuna atamudu vizuri zaidi lugha fulani ikilinganishwa na nyingine.Sababu za Kutokea Ulumbi
Ulumbi katika jamiilugha inasemekana kuwa unasababishwa na mambo ya ndani ya jamii yenyewe na mambo yanayotoka nje ya jamii. Kwa ujumla mambo hayo ni pamoja na uhamiaji, ukimbizi, ukoloni, biashara, elimu, dini, mipaka ya kimataifa, Nguvu za dola, teknolojia ya habari na mawasiliano, nguvu [kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni] nk. Ieleweke kwamba sababu za kutokea kwa ulumbi hutofautiana kati ya jamii na jamii na msemaji mmoja na mwingine.Matatizo ya Jamiilugha Ulumbi
Tatizo la kuteua lugha ya kutumia kitaifa kati ya lugha zinazotumika. Mfano, kupata lugha ya taifa, lugha ya kufundishia na lugha rasmi. Kila jamiilugha inaweza kuwa na nguvu kimatumizi au kwa idadi ya wazungumzaji kiasi cha kutaka kuteuliwa na hivyo kuwa vigumu kupata lugha kiurahisi.Hata hivyo, inashauriwa kuwa uteuzi wa lugha kitaifa unapaswa kufanyika kwa uangalifu sana kwa kushirikisha makundi mbalimbali ya kijamii ili kuepuka minyukano ya kimaslahi miongoni mwa wanajamii.Vilevile ulumbi unaweza kusababisha ukosefu wa umoja na mshikamano miongoni mwa wanajamii kwa vile kunakuwa jamii zinazojibainisha katika lugha na kila jamii inakuwa na utamaduni wake na hata mazingira yake.

MATUMIZI YA LUGHA
Katika kipengele hiki tunatarajia kuchunguza jinsi matumizi ya lugha yanavyojibainisha miongoni mwa watumialugha na jamiilugha. Ni kwa nini lugha hutumika tofautitofauti kati ya jamii moja na nyingine

.Sababu za kutofautiana kwa matumizi ya lugha:
Umri, elimu, jinsia, dini, matabaka [kisiasa, kiuchumi, kijamii], makabila, jiografia, nk.Makundi ya lugha za Tanzania
Tanzania ni nchi inayoonekana kama eneo la makutano ya makundi ya lugha za asili katika Bara la Afrika. Makundi haya ni Naija-Kongo (Bantu), Nailosahara, Afroasia (kikushitiki) na Kikhoisani. Haya ni makundi ya msingi.Nailosahara
Ni kundi lingine la lugha ambalo asili yake ni Afrika ya Kaskazini Misri, Ethiopia na Sudani. Mfano wa lugha za kundi hili Tanzania ni KimasaiAfro-Asia
Ni kundi kubwa lilizaa kundi la kushiti ambalo linajumuisha lugha kama Iraqw[kimbulu] 500,000 na lugha nyingine za Burunge, Alangwa,Gorowa na Ma’a (Mbugu) zina jumla ya wazungumzaji 40,000. Sifa moja kubwa ya lugha hizi ni sauti ya mkwaruzo kooni inayodhihirisha kuwa asili yake ni Uarabuni.Khoisani
Asili yake ni Afrika kusini. Mfano wa lugha TZ ni Kisandawe na Kihazabe . Sifa kubwa ya lugha hii ni konsonanti za kukisi.Bantu
Hili ni kundi linatokana na kundi la Benue Kongo ambalo lilitokana na kundi la Naija-kongo.Kundi hili linalojumuisha lugha nyingi zaidi pamoja wa wazungumzaji nchini Tanzania. Linahusisha lugha kama vile Kisukuma, kichaga, kinyakyusa, kiha nk.
Pamoja na kuwepo kwa makundi haya, bado kuna matumizi ya lugha nyingine za kigeni kama vile Kingereza, Kilatini, Kiarabu, Kifaransa, nk ingawa kwa viwango vidogo.Diaglosia
Katika jamii hutokea wakati mwingine lugha mbili kutumika, moja kutumika matika mazungumzo ya kawaida katika familia, mtu na mtu wakati lugha nyingine hutumika katika shughuri lasmi kama elimu mahakama, biashara, bunge nk. Vilevile inaweza kutokea lugha moja kuwa na lahaja tofauti ambapo kunakuwa na lahaja ambayo inatumika katika mawasiliano ya kawaida ilihali lahaja nyingine hutumika katika mawasiliano rasmi. Lugha ua lahaja inayotumika katika mawasiliano ya kawaida hupewa mhadhi ndogo C na inayopewa matumizi katika shughuri rasmi hupewa hadhi ya juu J. kunapokuwa na mahusiano ya namna hii tunasema kuna Diaglosia (kifaransa “diglossie”).

MAMBO YANAYOJIPAMBANUA KATIKA DIAGLOSIAa. Uamilifu
Lugha au lahaja J hutumika zaidi ikilinganishwa na lugha au lahaja C. Hii inatokana na kupewa majukumu mengi zaidi mfano kaika elimu, mahakama, biashara, dini, mahusiano ya kimataifa nk. Ni lugha inayoeleweka na kutumika na watu wengi zaidi ikilinganishwa na lugha ua lahaja C. Wageni wanapotaka kujifunza hupenda kujifunza lugha J. Vilevile maarifa mengi huwa katika Lugha au lahaja J ingawa ufafanuzi wake waweza kufanyika katika lugha au lahaja C.b. Umaarufu
Watumiaji wa lugha huiona lugha au lahaja J kuwa ni bora na maarufu zaidi kuliko C. Matokeo yake watu wengi zaidi hujifunza na kutumia J. mfano, watu watataka kusikiliza nyimbo, filamu, mashairi katika J hata kama hawaelewi ilikinganishwa na katika C. Vilevile katika dini lugha C hutumika zaidi. Mfano Kiarabu, Kiswahili nk.c. Mapokeo katika maandishi
Jamii huamini kuwa lugha iliyo katika maandishi ndiyo kiwakilisho sahihi cha lugha J. Hata tabaka la watumia lugha J huamini hivyo. Matokeo yake lugha J hutukuzwa wakati C hupuuzwa. J yaweza kuwa ya kizazi kilichopita au kilichopo mfano mashairi, dini, falsafa, sheria, sayansi nk.d. Ujifunzaji Lugha
Katika kiwangoi cha familia watu hutumia lugha C. Watoto wanapowasiliana wao kwa wao au na wazazi hutumia Lugha C. Hata hivyo, katika shughuri rasmi kama vile elimu, mahakama, redioni lugha J hutumika. Kanuni na miiko ya sarufi ya lugha J hufundishwa darasani wakati lugha C hufundishwa kimapokeo/kwa kurithishwa.e. Usanifishaji
Lugha J imefanyiwa tafiti nyingi zaidi kuhusu sarufi, msamiati, mitindo, otografia nk na miiko yake.Matokeo yake Lugha J inakuwa imesanifishwa na otografia yake haibadiliki ingawa maana yaweza kubadilika katika muktadha fulani.f. Msamiati
Kunakuwa na mwingiliano mkubwa wa msamiati kati ya lugha J na C. Hata hivyo, lugha J ina msamiati mwingi zaidi wa kiufundi na kigeni ambao unakosa visawe katika J. Vilevile msamiati katika lugha C mwingi sio rasmi. Kwa mifano;
Mother mum

Continue reading “DHANA YA JAMII LUGHA”

MWONGOZO WA TAMTHILIA YA KIJIBA CHA MOYO-Timothy M Arege..

Tamthilia ya kijiba cha moyo iliandikwa na Timothy M.Arege ambaye ni mwandishi mtajika wa lugha na fasihi ya kiswahili. Timothy ni mhadhiri katika chuo kikuu katoliki cha Afrika mashariki nchini Kenya.

Timothy aliandika tamthilia nyingine zikiwemo chamchela, Mstahiki meya na nyinginezo.

Utangulizi.

Moyo hupenda, moyo huchukia, moyo hukinai, moyo huhurumia, lakini moyo unapopatwa na dhiki ni rahisi kujua unaponzwa na nini.”

Tamthilia ya kijiba cha moyo ni tamthilia inayoangazia maisha ya Sele kudhaniwa kuwa mgonjwa, kunyimwa haki zake, na kutotetewa kwa namna yeyote anapopambana na waiotaka kuiba moyo wake halafu akabaki na kijiba.

Sele ni kijana ambaye amebadilika kitabia katika familia, moyo wake umepatwa na kutu, familia yake imekosa kupata utulivu kwa kughasiwa na ugonjwa wake. Sele kila tendo analiona kuwa ni uonevu , sele ana kijiba cha moyo. Je mawaidha ya bibi yatautibu ugonjwa wa Sele?

Dhamira ya mwandishi..

Timothy ananuia kutuonyesha uongozi wa kiimla
uliotapakaa katika nchi nyingi za bara la Afrika na kukita mizizi pale.

Tamthilia hii ni miongoni mwa kazi za kifasihi zinazo chunguza uhusiano uliopo baina ya ubepari wa
mataifa na hali duni ya kiuchumi iliyojiri mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa mtindo wa
kinaya. Mwandishi anatalii maudhui ya kiuchumi na mfumo wa kibepari ambao licha ya
kuwakandamiza wakazi wa mabara ya Afrika unapunguza nafsi za wafanyikazi na
kuwafanya kujihisi kuwa duni. Mahusiano haya yameendelezwa kwenye misingi ya
udhalimu.

Mwandishi ameelezea maonevu haya kwa kinaya akitumia sitiari pevu ili kukejeli mfumo mzima wa uelewaji wa dhana ya uhuru katika uzalishaji mali.


Katika tamthilia hii mwandishi pia analenga kutuonyesha kuwa uongozi uliopata mashiko yake kwenye mfumo wa kibepari, umemiliki nyenzo za kimsingi za uzalishaji mali kupitia kwa ufisadi, uongo na zaidi katika kuwakandamiza wale waliopata mwangaza wa kuona njama hii ya kunyanyaswa. Hili hutekelezwa ili kuzuia juhudi za wale waliopata mwamko mpya
kisiasa dhidi ya kuwazindua wanyonge wengine katika jamii. Mwandishi kupitia kwa
mhusika nguli (Sele), anasawiri uhusiano uliopo baina ya mataifa ya ulimwengu wa
kwanza ambayo huyapa misaada na kuyamiliki mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa
kuyafanya yakose kujitegemea. Mwandishi anasawiri kwa kina misaada inayotolewa kwa
mataifa machanga na kuonyesha kuwa misaada hii haiwafai Waafrika ila tu ni chombo
kinachotumiwa ili kuweza kupata fursa ya kuwanyonya Waafrika rasilimali zao. Hii ni
kinaya kwa kuwa Waafrika wenyewe hawaelewi hali hii.


Arege analenga kutuonyesha kuwa hali ya uhitaji katika mataifa mengi ya bara la Afrika
imesababishwa na unyonyaji wa nguvu za wakazi wake kwa malipo duni. Anaeleza kuwa
mipango ya kuyasukuma mbele kimaendeleo mataifa machanga barani Afrika ambayo
inaamuliwa na kuwekwa na mataifa yanayodai kujitegemea ni chanzo cha kudorora kwa
maendeleo yanayotarajiwa. Hii inatokana na ukweli kwamba walioshikilia (wakoloni)
nguzo za mfumo huu wa kibepari waliwafumba macho wakazi wa nchi changa kwa
kuwapa misaada isiyowafaa.

Falsafa ya mwandishi.

Mwandishi ameongozwa na falsafa ya “UJinga ni Ugonjwa“Nchi zenye nguvu zinatumia aina zote za kutoa misaada ili kumiliki rasilimali za mataifa aina ya tatu juu ya ujinga na kutoelewa kinachofaa kufanywa. Hili linachorwa vizuri na mhusika sele alipojitoa kupigania haki wengine wakafikiri ni mgonjwa(ujinga).

Mtazamo wa mwandishi.

Mwandishi ameegemea Mtazamo wa kisiasa yaani kiyakinifu; Kuungana, kujitahidi na kujikomboa kimawazo ni suala liwezalo kusaidia waafrika
kujiendeleza kwa misingi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hiki kinabainika baada ya
kutamatisha kusoma tamthilia hii ambapo inabainika kuwa ugonjwa wa Sele si
ule wa kawaida kama ulivyochukuliwa na wahusika tamthiliani bali kuzinduka kutokana na mwamko mpya wa kisiasa na kijamii.

Msimamo wa mwandishi. katika tamthilia ya kijiba cha moyo mwandishi anamsimamo wa kimapinduzi kwani amejadili matatizo yanayochangia kukwama kwa ujenzi wa jamii mpya. Msimamo wake umebainishwa kutokana na jinsi alivyochora mhusika Sele, akijaribu kujiokoa na kujikomboa kimawazo wengine wakifikiri ni mgonjwa lakini akakosa kupata washabiki werevu. (kijiba)

Wahusika katika tamthilia ya kijiba cha moyo.

Wahusika ni viumbe wa kisanaa wanaopatikana katika kazi ya fasihi na wenye sifa za
kibinadamu. Aghalabu huwa na sifa za kimaadili, kitabia, kiitikadi, kifalsafa ambazo
hutambulishwa na wanayoyasema (mazungumzo) na wanayoyatenda (matendo),
Wamitila (2002).

1.Sele- mumewe Aisha na mtotowe Musa na Zainabu. Sele kulingana na tamthilia ana sifa zifuatazo;

. Ni mdadisi: katika Kijiba cha Moyo tunaweza kusema Sele ni
mdadisi kutokana na tabia yake ya kuuliza maswali mengi. Alimdadisi daktari
alipokwenda hospitalini pia tunajuzwa kuwa Sele alimuuliza daktari
maswali mengi alipokuja kwao kumtibu. Kwa mfano:
Sele: Naelewa lakini nipe nafasi kuuliza swali
kabla ya kuanza.
Daktari: (Hana stahamala tena.) Sitaki maswali yako
mengi. Siku ile nyingine umeniuliza maswali
mengi ya kunipotezea muda. Mimi ndiye
daktari; nakuuliza maswali wajibu. (Kimya)
wewe ni wa kujibu, Sasa wewe unataka
kunihoji . Hili tendo linadhihirisha udadisi wa mhusika Sele.

Sele, Ni mwenye kughasiwa na ugonjwa wa moyo.

Sele ni mgonjwa kutokana na mavazi ya wagonjwa aliyovaa na daktari si mgonjwa bali ni
daktari kwa sababu amevaa sare za kazi na glovu tayari kutibu wagonjwa.(uk 52)

.Ni mwenye huruma. Tendo la Sele la kukataa kuwala vidagaaa, linamsawiri kama
mhusika mwenye huruma. Sifa hii imedhihirika kupitia mazungumzo ya Zainabu na
Bi. Rahma(uk 15-16) Sele anakwepa kula vidagaa, kwa kuwa anawaonea
huruma kwa kuliwa na papa naye awale.

. Ni mtetezi wa wanyonge. Sele anaonekana kama mtetezi wa wanyonge. Kwa kusema „vinavyoliwa huku
vinatazama‟ inamaanisha vidagaa ni wanyonge hawawezi kujitetea. Hivyo basi
anapinga tendo la papa la kuwala vidagaa; kwa kutokula vidagaa yeye mwenyewe.

. Ni mwenye kutoridhika. Tendo la Sele katika tamthilia ya Kijiba cha Moyo la kutaka kufanyiwa „plastic
surgery‟ linadhihirisha sifa yake ya kutoridhishwa na maumbile yake na nia yake ya
kutaka kuyabadili. Hili limedhihirika katika kurasa 31-36. Hali hii ya Sele
inawakilisha mataifa ya Kiafrika yasiyoridhishwa na hali zao na kutaka kuiga mataifa
ya ng‟ambo.

. Ni mwenye hasira. Sele amesawiriwa kama mwenye hasira na
asiyependa kusumbuliwa. Haya yamedhihirika kupitia namna anavyoongea kwa
ukali kama ifuatavyo:
Sele: (Kwa sauti ya juu.) Wewe umejua kama
mimi sitaki mtu kunisumbua halafu unanijia
kwa fujo. Dharau tu! (uk.33)

.Ni mwenye kujichukia. Sele anavyochukia maumbile yake. Hivyo
kumfanya kujichukia. Chuki hii ndiyo chanzo cha ndwele yake na ndicho kijiba chake
cha moyo. Chuki hii ya Sele inaashiria jinsi mataifa yanayoendelea yanavyokosa
kujithamini.(uk33-34)

.Ni mwenye sura ya kupendeza.

Sele kama kijana mwenye sura
ya kupendeza yenye pua laini iliyochongeka vizuri na midomo mikubwa. Vilevile ana
mataga na weusi uliokoza na kukolea. (Uk 43)

.Ni mkaidi. Tunamuona Sele anakaidi mashauri ya jamaa zake na pia anakaidi kumeza dawa kwamba yeye si mgonjwa.

2. Aisha-mkewe Sele.

.Ni mwenye kupenda raha.  Hili linadhihirishwa pale alimomwambia mumewe kwamba waende kujistarehe (uk 03)

.Ni mwenye mapenzi na kumjali mume wake. Hili linadhirika anapoingia chumba walimo wazee wake na kuwapuuza akienda mbio kutafuta vitabu kuvisoma ili aelewe ugonjwa wa mume wake ili aweze kumsaidia.(uk20)

.Ni msomi. Amesawiriwa kama msomi. Sifa hii inadhihirika kupitia tabia
yake ya kusomasoma vitabu. Hili linadhihirika kupitia mazungumzo baina ya Aisha,
Zainabu na Bi. Rahma(uk18)

.Ni mwenye heshima. Heshima ya Aisha inadhihirika pale anapowheshimu wazee wake kwa kutowaita majina.

3.Zainabu-mamake Sele na mkewe Musa.

.Ni mwenye kumjali mwanawe Sele. Zaiabu tunamuona anatembea juu chini akimtafutia dawa la kumtibu. Tena mwenye hamu kusikiliza muuguzi Jamila wakati alipokuwa anamtibu kwake nyumbani (uk88)

.Ni mvumilivu kwani tunamuona katika tamthilia nzima anavumilia na ugonjwa wa mtotowe hata ingawa alimtusi wakati mwingine.

.Ni mwenye matumaini kuwa mtoto wake atapona ugonjwa wa moyo.

4.Jamila-Bintiye Hassan.           Ni msomi. Jamila anadhihirika kama msomi na kupitia maelezo yake
tunaweza hatimaye kuufahamu ugonjwa wa Sele.(uk90)

.Ni muuguzi Aliyemuugua sele.

.Alisoma na Sele . Hili linathibitishwa kwenye (uk88) wakati zinabu na Bi:Ramhma walipokuwa wanamgojea Jamila na Bi Rahma akasema “watu waliosoma pamoja hawakosi kupatana”

5.Daktari.

.Ni mkatili kwani tunamuona katika tamthilia ndiye aliongoza waliomtembelea sele na kumpekuapekua alipokuwa amelala. Pia alimkataa kuuliza maswali kuhusu ugonwa wake Sele.

.Ni msomi kwani ni daktari kiutaalamu.

6.Amri-Babu yake Sele.

.Ni mwenye mapenzi hasa wa Sele juu ya ugonjwa wake.

7.Musa-Babake Sele.

Hajali kuhusu ugonjwa wa sele.

Maudhui katika tamthilia ya kijiba cha moyo.

Maudhui katika kazi ya fasihi ni jumla ya mawazo yote yanayozungumzwa pamoja na mtazamo wa mwandishi juu ya mawazo hayo.

1. Ubepari. Ni mfumo wa kiuchumi unaowezesha watu wachache kumiliki rasilimali na njia kuu za uchumi wa nchi kwamfano Madaktari watatu waliomjia Sele wakati alipolala kitandani na kumpekuapekua hudhihirisha ubepari.

Mwandishi kupitia mhusika Sele anasawiri uhusiano uliopo baina ya mataifa ya ulimwengu wa kwanza (viongozi) ambayo huyapa mataifa ya ulimwengu wa tatu misaada isiyofaa kv matibabu ya Sele, ila tu ni chombo cha kupata fursa ya kugawanya rasilimali zao.

2. Ugonjwa/Magonjwa. Ni kuwa katika hali ya kusababishiwa hali mbaya kwamfano Sele anaoekana akivaa sare za wagonjwa na Daktari kavaa sare za udaktari maanake kuna mgonjwa na mtibu.

Pia tunamuona Sele ni mgonjwa wa moyo, Jamila anathibitisha kwenda kwake hospitalini anapotoka kumhudumia(uk 88)

Muuguzi jamila pia anaeleza kwamba ugonjwa wa sele haujafikia kiwango cha kutisha (uk89).

3. Elimu. Ni mfumo wa mafunzo yanayopatikana shuleni, vyuoni, au katika maisha.

Jamila ni msomi kwani ni muuguzi aliyemhudumia sele. Mazungmzo ya Zinabu na Bi Rahma kwamba Sele na Jamila walisoma pamoja unadhihirisha usomi wake.(uk 88)

4. Mapenzi. Ni hali ya kuingiwa moyoni kuthamini mtu au kitu zaidi ya mwingine au kingine.

Aisha anamoenda sana mumewe Sele ndiposa anaingia chumba walimo wazee wake na kuwaluuza akitafuta vitabu akikusudi kusoma ili aelewe ugonjwa wa Sele aweze kumsaidia(uk18)

5. Mabadiliko. Ni hali ya kubadilika kutoka hali moja kwenda hali nyingine.

Sele alibadilika baada ya kugundua kwamba anagandamizwa lakini wengine hawakumuelewa ili wamtolee msaada ya kujikomboa na kuwatetea wanyonge -mambo hayakufaulu.

7. Ukoloni. Ni hali unapokuta nchi moja inatawaliwa na nchi nyingiine.

Tendo la madaktari kumzungukazunguka na kumpekuapekua Sele mara wakishauriana na kumuashiria kisha kusema kwa pamoja “bado amelala” kinaashiria wakolni walivyokuja bara la Afrika wakachunguza rasilimali, na wakaona bado waafrika wamelaala na ndipo kuamua kutwaa rasilimali hizo. (Uk79)

8. Unyanyasaji. Ni hali ya kudharau mtu kwa kiburi au kwa kujiona bora dhidi yake.

Tendo la madaktari watatu kuja kumpekuapekua huku na kule mwili mzima ni ishara ya kudharau na kumnyanyasa.

Tena kunyimwa fursa ya kuuliza daktari na kutopewa habari kuhusu tests zake hospitalini ninishara ya kumnyanyasa kiakili.

9. Ukatili. Ni hali ya kutokuwa na huruma.

Ukatili unajitokeza pale daktari anapompiga dawa sele akiwa anajua sele si mgongwa ila tu kwa hamu ya kumyakua pesa zake.(uk52-53) “staki kupoteza muda, time is money bwana” ni ishara ya ukatili.

10.Utumwa. Ni mfumo unaotoa fursa kwa binadamu kumiliki binadamu mwingine kama mali yake.

Utumwa unadhihirika pale ambapo Sele ananyimwa fursa ya kupata matokea ya habari kuhusu “tests” zake hospitalini (uk60, 61)

11.Utabaka. Hi ni hali ya ubaguza wa kiuchumi, kisiasa na kijamii inayotenganisha watu wa hali duni na wale wa hadhi ya juu. Utabaka unadhihirika pale tunapoona Sele anahudumiwa lakini kwa ghari na akasema nipe “deposit yangu” (uk. )

12. Ndoa. Ni maafikiano rasmi baina ya mwanamke na mwanamume. Ndoa inashihirika kati ya Sele na Aisha pamoja  Musa na Zainabu.

13. Uvuvi.

14. Ukosefu wa nidhamu.

Ukosefu wa nidhamu katika tamthilia ya kijiba cha moyo unaonyeshwa pale Aisha alipoingia chumba waliomo wazee wake na kuwapuuza baada ya kuwasalamia tu na akaingia kwenye chumba kingine akaaanza kutafuta vitabu vya kusoma iki aelewe ugonjwa wa sele. (Uk20)

Tamathali za Usemi katika tamthilia ya kijiba cha moyo.
Kazi ya fasihi, haihusiani na kuwasilisha mawazo tu, bali kuyawasilisha mawazo hayo
kisanaa. Habari au wazo fulani haliwezi kuelezwa au kuwasilishwa kwa wasomaji bila
kuzingatia hali ya kuwepo kwa usanii wowote. Mawasiliano yote ya kisanaa huhitaji
kuwasilishwa kwa mbinu za kimvuto, ile njia inayompa raha au ladha tamu msomaji
anapojaribu kuufuatilia ujumbe wa mwandishi wa kazi ya fasihi. Nakwahivy, zifuatazo ndizo baadhi ya tamathali za Usemi nilizoweza kuchambua katika tamthilia ya kijiba cha moyo;

1.Tashbihi ni tamathali ya usemi ambapo watu ama vitu viwili au zaidi hulinganishwa au
hufananishwa na watu ama vitu vingine.

Kwa mfano, Sele akielezea umahiri wake katika uogeleaji
anasema:
… Kisha nikapumzika juu ya mawimbi
kama gogo huku chini yangu maji yakipiga
na kutoa povu. (uk. 2)

“Na mimi nahisi kama sisi
tunayumbishwa mithili ya miti
msimu wa kipupwe… “(uk. 29)

“Linaweza kuwa dogo na athari
zake ziwe kubwa, kama tone la
mafuta ya taa kisimani- huhangaisha
mtaa mzima… “(uk. 50)

2. Tashihisi. ni tamathali ya kukipa kitu kisichokuwa
na uhai mkamilifu sifa za kitu chenye uhai kinachojitegemea katika mazingira yake.

Katika tamthilia ya Kijiba cha Moyo,
Sele anatuchorea taswira ya starehe ya bahari na uzoefu wake katika uogeleaji. Anaeleza:
“…Nikapiga mbizi. Nikapambana na Mawimbi chini kwa chini. Nikayapenya.
Nikataka nitokezee huko wanakokaa papa.
Nilipoibuka nilikuwa palee! Mbali huko.
Kisha nikapumzika juu ya mawimbi kama
gogo huku chini yangu maji yakipiga kutoa
povu. Mimi juu, papa chini. Siku hizo nilitaka
niwe bingwa wa dunia”. (uk. 2)

Mtindo huu pia unajitokeza katika maelezo ya Aisha kuonyesha namna ilivyomwia
vigumu katika kutambua ugonjwa anaougua Sele. Anaonyesha kuwa hali hii ni ngumu
anaposema:
“…Kama lililotiwa hamira, linafura
na kujaa fikirani. Kichwa kinakuwa
kizito kama nanga…” (uk. 20)
Jambo limepewa uwezo wa kufura na kujaa na pia kufanya kichwa kuwa kizito. Hii ni
tashhisi ambayo mwandishi ametumia ili kuonyesha namna mchanganyiko wa mawazo
ulimpata .

3.Methali ni kifungu cha maneno yanayotumiwa
pamoja kisanii, kwa njia ya kufumba na kupigia mfano jambo fulani.

Tamthilia ya Kijiba cha Moyo imetawaliwa na methali mbalimbali kwa nia ya mwandishi
ya kukuza ujumbe wake. Bi. Rahma analalamikia mapishi ya kisasa na kushuku kuwa
huenda ndiyo yanamkosesha Sele hamu ya chakula. Anamwambia Zainabu:
“… Watavilaje vyakula vya kuharakishwa?
Heri huvutwa kwa subira mama. Vyakula
visivyopata kutua sufuria, vipi vitatua
moyoni?” (uk. 14)
Methali anayoitumia Bi. Rahma ina maana kwamba kizazi cha kisasa hakina subira
katika kutekeleza majukumu hasa kimapishi.

Mwenye nguvu mpishe (uk 29)

Mchana watasema usiku watalala(uk 34)

Pole pole ndio mwendo (uk26)

Methali nyingine katika tamthilia ni “mhitaji zote ni mtumwa” (uk25).

Continue reading “MWONGOZO WA TAMTHILIA YA KIJIBA CHA MOYO-Timothy M Arege..”

NGELI ZA LUGHA YA KISWAHILI.

Lugha ya Kiswahili ina ngeli nyingi sana.Baadhi yazo bado yafanyiwa utafiti na wataalam mbalimbali wa lugha ili kuidhinisha matumizi yake.K.m Ngeli ya VI-VI ambayo ina nomino nomino moja tu inayojumuishwa humo yaani vita. Ngeli zinazotumika aghalabu ni kama zifuatazo. Ngeli ya A-WA-Hii ni ngeli ya vitu vilivyo na uhai kama vile wanyama,ndege, binadamu, wadudu n.k.Baadhi ya maneno yanaanza kwa kiambishi cha ngeli M(umoja) na Wa(wingi). Mengine huanza kwa Ki(umoja) na Vi(Wingi).Kuna miundo mingine mingi ambayo ipo katika ngeli hii. Ngeli ya LI-YA-Hii ni ngeli ya vitu visivyokuwa na uhai.k.m gari.Aidha ngeli hii hubeba majina yaliyo katika hali ya ukubwa.K.m janajike Majina mengi hapa huwa na muundo wa JI(umoja) na MA(Wingi). Ngeli ya KI-VI-Hii pia ni ngeli ya vitu visivyokuwa na uhai.Isitoshe,hubeba majina katika hali ya udogo.K.m Kijumba-Vijumba.Majina mengi hapa huanza kwa MA au ME katika wingi. Ngeli ya U-I-Nomino nyingi huanza kwa M(umoja) na MI(Wingi).Hii ngeli pia hubeba majina ya miti au mimea.K.m Mpera-Mipera Ngeli ya U-ZI-Majina mengi huanza kwa U(umoja) na ZI(wingi).Majina yenye silabi mbili huongezwa /ny/ katika wingi.Majina yenye silabi tatu au zaidi hubadilishwa kwa wingi kwa kutoa kiambishi cha ngeli U. Ngeli ya YA-YA-Ngeli ya nomino za wingi.Majina haya hayana umoja.Mengi yazo huanza kwa MA katika umoja na wingi.K.m Maji-maji Ngeli ya I-ZI-Ngeli hii hubeba majina yasiyobadilika katika umoja na wingi.Majina haya huchukua viambishi tofauti.Mengi yazo huanza kwa viambishi kama vile /ny/,/mb/,/ng/,/u/. Ngeli ya U-YA-Majina yaliyoko hapa huanza kwa U(umoja) na YA(wingi). Ngeli ya I-I-Hii ni ngeli ya majina ya wingi ambayo huchukua kiambishi I katika umoja na wingi vilevile.K.m Jua, mvua n.k.Majina haya hayana muundo maalum. Ngeli ya U-U-Hii ni ngeli ambayo majina yaliyomo huanza kwa U katika umoja na wingi.Kwa upande mwingine,kuna pia yale majina yasiyoanza kwa U katika wingi.K.m uzi-nyuzi, ugonjwa-magonjwa n.k Ngeli ya PA-KU-MU-Hii ni ngeli ya mahali/pahali.PA hudhihirisha mahali palipo wazi,KU hudhihirisha mahali kusikojulina ihali MU huonesha/humaanisha ndani kabisa.

arigumaho810@gmail.com

Ujumbe wa pasaka.

Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari. Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani. Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!” Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki. Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe. Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba. Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa). Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.

Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua. Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha. Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi .” Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.” Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu, basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!” Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe! Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana. Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa. Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni anamwita Eliya.” Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.” Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.

Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini. Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!” Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome. Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu. Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato, Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu. Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.

Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili. Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi. Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.

Mwalimu Johnpaul Arigumaho anawatakia pasaka njema.

arigumaho810@gmail.com

Hadithi za Burudani.

TAMATHALI ZA USEMI

Tamathali za Usemi ni matumizi ya maneno kwa namna fulani ili kuifanya lugha iwe ya kuvuitia na kuifanya kazi ya sanaa iwe ya kupendeza.

Kuna aina mbili za tamathali za usemi:

Mbinu au Fani za Lugha– Ni uteuzi wa maneno ili kuifanya lugha iwe ya kupendeza na kuvutia. Pia, Mapambo ya Lugha. Fani za Lugha zinaweza kutambulikana moja kwa moja bila kusoma kifungu kizima.

Mbinu za Sanaa– Ni ubunifu wa kisanaa unaojitokeza baada ya kusoma au kusikiliza masimulizi. Angalau unahitaji kusoma sentensi kadhaa au hata hadithi nzima ili kutambua mbinu ya sanaa iliyotumika.

Mbinu za Lugha.

Tanakali za Sauti -Ni mbinu ya kutumia maneno yanayoiga sauti au hali fulani au namna kitendo kilivyofanyika. Milio.

Tashbihi -Hii ni mbinu ya lugha inayolinganisha vitu au hali mbili tofauti kwa kutumia maneno ya kulinganisha; ‘kama’, ‘mithili ya’, ‘sawa na’, ‘ja’. Tashbiha. Similes. Istiara -Ni mbinu ya kulinganisha vitu viwili moja kwa moja kwa kutumia kiungo ‘ni’ ama ‘kuwa’. Istiari. Sitiari. Imagery Jazanda – Ni kulinganisha vitu viwili moja kwa moja bila kutumia viunganishi.

Taashira -Ni matumizi ya lugha ya ishara kuwakilisha ujumbe fulani. Jina au kitu fulani kinatumika kumaanisha kitu kingine chenye uhusiano na kile kilichotumiwa. Symbolism Taswira – Ni matumizi ya lugha/maneno yanayojenga picha ya hali au jambo fulani kwa msomaji.

Tashihisi -Hii ni mbinu ya kupatia kitu kisicho hai sifa za kiumbe mwenye uhai (sifa za kibinadamu).

Chuku -Ni kutumia maneno yaliyotiliwa chumvi ili kusisitiza ujumbe fulani au kusifia kitu. Kutilia Chumvi. Hyperbole Takriri -Ni mbinu ya kurudiarudia neno moja au kifungu cha maneno ili kusisitiza ujumbe fulani. (Repetition) Tanakuzi-Tanakuzi ni mbinu ya kusisitiza ujumbe kwa kuambatanisha maneno ya kinyume au yanayokinzana. U(Ukinzani )

Majazi – Majazi ni pale tabia za wahusika zinapoambatana na majina yao halisi.

Lakabu – Ni mbinu ya mhusika kupewa/kubadikwa jina na wahusika wengine ama yeye mwenyewe kujibandika jina linalooana na tabia/sifa zake. Semi – Ni fungu la maneno linapotumika kutoa maana nyingine, badala ya ile ya maneno yaliyotumika. Semi hutumika kuficha ukali wa maneno au kupamba lugha. Kuna aina mbili za semi: Nahau – huwa na vitenzi Misemo – haina vitenzi Methali –

Methali ni misemo ya hekima yenye maana iliyofumbwa. Mhusika, mwandishi wa fasihi anaweza kutumia methali kupitisha ujumbe.

Maswali ya Balagha -Tashititi au maswali ya balagha ni maswali yanayoulizwa na msimulizi au mhusika ambayo hayahitaji jibu. Mubalagha. (Rhetorical questions)

Uzungumzi Nafsiya – Mhusika hujizungumzia, ama kwa kuongea au kuwaza, bila kukusudia kusikika na yeyote. Ritifaa – Mbinu ya kuzungumza na mtu aliyekufa (au asiyekuwepo) kana kwamba yuko pamoja nawe.

Utohozi – Kutohoa ni mbinu ya kuswahilisha maneno ya lugha nyingine, yatamkike kama ya Kiswahili.

Kuchanganya Ndimi – Kuweka maneno yasiyo ya Kiswahili katika sentensi ya Kiswahili. Kuhamisha Ndimi – Ni kuingiza sentensi ya lugha nyingine katika kifungu cha lugha ya Kiswahili. Kinyume na Kuchanganya ndimi (ambapo mwandishi huchanganya maneno katika sentensi moja, katika kuhamisha ndimi, sentensi kamilifu ya lugha nyingine hutumika miongoni mwa sentensi za Kiswahili sanifu. }

Mbinu za Sanaa Kinaya – Kinaya ni mambo katika sanaa kuwa kinyume na matarajio ya hadhira. Irony

Kejeli -Kejeli ni mbinu ya sanaa inayotumia maneno kudharau au kukemea kitendo au mtu fulani.

Taharuki -Taharuki ni mbinu ya kusimulia au kuandika riwaya/hadithi kwa kufanya hadhira na/au wahusika wajawe na hamu ya kutaka kujua kitakachotokea baadaye; hamu ya kutaka kuendelea kusoma/kusikiliza. Baadhi ya hadithi huishia kwa taharuki na kuilazimisha hadhira yake ijikamilishie au ibaki ikijiuliza maswali. Suspense.

Sadfa – Sadfa ni kugongana kwa vitendo viwili vinavyohusiana kana kwamba vilikuwa vimepangwa, japo havikuwa vimepangiwa. (Coincidence)

Kisengere Nyuma – Mwandishi ‘hurudi nyuma’ na kuanza kusimulia kisa kilichokuwa kimetendeka kabla ya alichokuwa akisimulia. Aidha, mwandishi hubadilisha wakati wa masimulizi na kuwa wakati wa kisa hicho. Hutumika sana kuonyesha mhusika anapokumbuka kitu, au kutupatia msingi wa jinsi mambo yalivyoanza.

Kisengere Mbele – Mwandishi anapobadilisha wakati na kusimulia mambo yatakavyokuwa siku za usoni; au kutumia lugha isiyo moja kwa moja kutabiri yatakayojiri.Utabiri. Foreshadow

Njozi au Ndoto – Mwandishi hutumia ndoto kutabiri jambo litakalofanyika au kufumbua jambo lililokuwa limefumbwa.

Upeo wa Juu – Ni sehemu ya hadithi ambayo matukio yanafanyika kulingana na mapenzi ya hadhira au msomaji. Climax.

Upeo wa Chini – Ni sehemu ya hadithi ambayo matukio yanafanyika kinyume na mapenzi ya hadhira au msomaji. Aghalabu upeo wa chini hutokea baada ya upeo wa juu. anti-climax .

Nyimbo – Nyimbo na/au mashairi yanaweza kutumika katika hadithi kwa madhumuni mbalimbali.

arigumaho810@gmail.com. +256778514179/757223817

FASIHI YA KISWAHILI.

Fasihi ni sanaa inayotumia lugha. Fasihi hutumia lugha kutoa sanaa mbalimbali katika jamii.

Tanzu za Fasihi

Kuna tanzu mbili kuu za fasihi, na kila utanzu una vipera vyake: Fasihi Simulizi na Fasihi Andishi: Fasihi Simulizi ni kama vile Hadithi (Ngano) – hekaya, mighani, visasili, Nyimbo – za jandoni, za ndoa, za kazi, Maigizo – michezo ya kuigiza, ngomezi, Tungo Fupi – methali, vitendawili n.k

Fasihi Andishi huwa ni fasihi inayoelezwa na kuhifadhiwa kimaandishi.kv

1) Hadithi Fupi – hadithi isiyokuwa ndefu iliyochapishwa katika mkusanyiko wa hadithi nyingine

2) Riwaya – Hadithi ndefu iliyochapishwa katika kitabu chake pekee

3) Tamthilia – Mchezo wa kuigiza uliowekwa kwa maandishi

4) Ushairi* – Mashairi yaliyoandikwa.

Tofauti kuu kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi ni kwamba, fasihi simulizi huwasilishwa kwa njia ya mdomo au matendo ilhali fasihi andishi huwasilishwa kwa njia ya maandishi.

Tanbihi:Ushairi ni kipera cha nyimbo lakini pia mashairi yanaweza kuwa chini ya fasihi andishi, ikiwa yamechapishwa.

Tofauti kati ya Fasihi Andishi na Fasihi Simulizi

Fasihi simulizi huwasilishwa kwa njia ya mdomo na/au matendo ilihali fasihi andishi huwasilishwa kwa njia ya maandishi

2. FS ni mali ya jamii lakini FA huweza kuwa Kazi na mali ya mwandishi (na mchapishaji)

3. Msimulizi anaweza kubadilisha sehemu fulani lakini Kitabu kilichoandikwa hakiwezi kubadilishwa

4. FS huhifadhiwa akilini ilihali FA huhifadhiwa vitabuni

5. Kazi simulizi hubadilika na wakati lakini kazi andishi haibadiliki na wakati.

6. FS huhitaji msimulizi au fanani na hadhira yake wawe mahali pamoja wakati wa masimulizi lakini Msomaji anaweza kusoma kitabu cha hadithi peke yake, mahali popote, wakati wowote.

7. Katika FS, Mtu yeyote anaweza kutunga na kusimulia lakini FA Ni lazima mwandishi na msomaji wawe na uwezo wa kusoma.

8. FS hutumia wahusika changamano (wanyama, watu, mazimwi nakadhalika lakini FA hutumia wahusika wanadamu.

Umuhimu wa Fasihi Katika Jamii

  1. Kuburudisha jamii. Takribani vipera vyote vya fasihi huwa na kusudi la kufurahisha, kutumbuiza na kusisimua hadhira.

2. Kuelimisha. Fasihi hukusudia kuelimisha hadhira kuhusu jamii, mazingira n.k Kudumisha maadili katika jamii kwa kuelekeza, kuonya na kunasihi hadhira jinsi ya kufuata mwelekeo unaokubalika katika jamii.

3. Kuunganisha jamii. Fasihi huleta pamoja watu katika jamii. Kwa mfano, katika nyimbo, miviga, vichekesho.

4. Kukuza lugha. Aghalabu tungo zote za fasihi hutumia lugha. Isitoshe, fasihi hutumia mbinu nyingi za lugha. Wasimulizi na waandishi wa fasihi huhitaji kuwa na ukwasi wa lugha.

5. Huhifadhi mila, tamaduni na itikadi za jamii. Aghalabu kazi za fasihi (hasahasa Fasihi Simulizi) huambatanishwa na desturi mbalimbali za jamii husika.

6. Hukuza uwezo wa kufikiri. Vipera vingi vya fasihi huwachochea hadhira kufikiri sana ili kupata suluhisho. k.m vitendawili, ngano za mtanziko nakadhalika…

arigumaho810@gmail.com.

Tulia moyo Ndugu.

Mpendwa rafiki yangu, Hakuna sehemu ambayo ni salama kwa kila kitu. Kila mmoja wetu kuna changamoto fulani anayopitia kwenye maisha yake. Unapojikuta uko katika hali fulani ya changamoto ndiyo sehemu ya maisha hivyo unatakiwa tu kujifunza namna ya kuikabili hiyo hali. Unajua vitu vyote vitapita na kuisha lakini changamoto hazitokuja kuisha ila vitaisha kwako tu pale tu utakapokufa lakini kama uko hai, maisha ni changamoto na pambana ili uishi vile unavyotaka wewe. Huwa kuna watu wanatabia ya kuchukua mambo ya kazini na kuyaleta nyumbani, na wengine na kuchukua ya nyumbani na kuyapelekea kazini. Vitu kama hivi vinakuwa vinaathiri utendaji wa kazi wa sehemu zote mbili kwa kiasi kikubwa sana. Acha kila sehemu ijitegemee yenyewe, kama ni mambo ya nyumbani yaache yaende nyumbani na kama ni ya kazini yaachie huko kazini. Kumbuka mafahari wawili hawakai zizi moja kama wasemavyo waswahili.

arigumaho810@gmail.com

Our logo.

Kiswahili kidato Cha kwanza 2022. UMSSN: Arigumaho Johnpaul na Mukama Chrispus.

Msamiati wa ukoo

Watu wa nyumbani huwa ni binadamu tunaoishi nao nyumbani kwetu. Watu wa nyumbani husaidia kutekeleza majukumu ya nyumbani ili familia kuwa na maendeleo mazuri.

Kuna watu tofauti tunaoishi nao nyumbani kwetu, yaani mama, baba, kaka, dada, binamu, babu, nyanya, shangazi, ami nk

Msamiati wa Majina ya Ukoo

Haya ni majina ya heshima yanayotumiwa na watu mbalimbali katika familia kulingana na uhusiano wao. Pia huitwa msamiati wa nasaba/jamaa/jamii.

Mifano

Familia Ndogo

Hii ni familia ya karibu, familia ya nyuklia (nuclear family) ambayo uhusisha tu wazazi na watoto wao.

Familia ndogo (nuclear family)
  1. baba: (father) ni mzazi wa kiume.
  2. mama: (mother) mama ni mzazi wa kike.
  3. mwana: (child) mtoto wako
  4. mzazi: (parent) mtu aliyekuzaa.
  5. ndugu: (sibling) mtoto wa mzazi/wazazi wako. Mara nyingi ‘ndugu’ hutumika kurejelea watoto waliozaliwa baada yako, au watoto wa kiume waliozaliwa na wazazi wako.
  6. kaka: (brother) mvulana aliyezaliwa na mzazi/wazazi wako. Aghalabu kaka hurejelea mvulana aliyekutangulia kuzaliwa.
  7. dada: sister)
    msichana aliyezaliwa na mzazi/wazazi wako. Aghalabu dada hutumika kurejelea wasichana waliokutangulia kuzaliwa.
  8. bin: (son, mwana) mtoto wa kiume
  9. binti: (daughter) mtoto wa kike.
  10. kifungua mimba: (first born) mtoto wa kwanza kuzaliwa
  11. Kifunga mimba: (last born)
    mtoto wa mwisho kuzaliwa
  12. mapacha: (twins)
    watoto wawili waliozaliwa siku moja na mama mmoja
  13. mke: wife (bibi, wife) mwanamke mliyefunga ndoa pamoja kuanzisha familia.
  14. mume: (husband) mwanamume mliyefunga ndoa pamoja ili kuanzisha familia.
  15. baba wa kambo:(stepfather)
    mwanaume aliyeoa mamako, na ambaye si baba yako wa damu.
  16. mama wa kambo: (stepmother)
    mwanamke aliyeolewa na babako, na ambaye si mama yako wa damu

Familia Kubwa

Familia Kubwa huhusisha familia ndogo pamoja na wazazi wa baba/mama, ndugu za baba na mama, pamoja na watoto wao. Kwa Kiingereza, familia hii huitwa Extended Family.

Familia kubwa (extended family)
  1. babu: (grandfather) mzazi wa kiume wa mzazi wako. baba ya mama yako au baba yako.
  2. nyanya: (grandmother, bibi)
    mzazi wa kike wa mzazi wako. mama aliyemzaaa mamako au babako.
  3. mjukuu: (grandchild)
    mtoto wa mtoto wako
  4. mjomba: (uncle), baba mkubwa, baba mdogo.)
    mvulana aliyezaliwa na babu au nyanya yako. Aghalabu mjomba hutumika kurejelea ndugu wa kiume wa mama yako. Katika mfumo huo, mvulana aliyezaliwa kabla ya babako huitwa baba mkubwa naye yule aliyezaliwa baada ya babako huitwa baba mdogo
  5. shangazi: (aunt), mama mdogo, mama mkubwa.)
    msichana aliyezaliwa pamoja na mzazi wako. Aghalabu shangazi hutumika kurejelea ndugu wa kike wa baba yako. Katika mfumo huo, msichana aliyezaliwa kabla ya mamako huitwa mama mkubwa naye msichana aliyezaliwa baada ya mamako huitwa mama mdogo
  6. mpwa: (nephew, niece)
    mtoto wa ndugu yako
  7. amu: (mjomba)
    ndugu wa mzazi wako.
  8. binamu: (cousin)
    mtoto wa mjomba wako
  9. bintiamu: (cousin)
    mtoto wa kike wa mjomba wako. binamu wa kike.
  10. shemeji: (sister-in-law, brother-in-law, relative by marriage) ndugu wa mkeo au mumeo. ndugu wa mke wa kakako, ndugu wa mume wa dadako. undugu unaotokana na ndoa.
  11. wifi: (sister-in-law)
    mke wa ndugu yako.
  12. mkwe: (mother in-law, fatherher in-law)
    mzazi wa mke wako au mume wako.
  13. mkaza mjomba: (aunt-in-law)
    mke wa mjomba wako
  14. mkaza mwana: (mkaza, daughter-in-law)
    mke wa mtoto wako
  15. bavyaa: (father-in-law) (baba mkwe, father-in-law)
    baba mkwe. baba aliyemzaa mke wako au mume wako
  16. mavyaa: mother-in-law (mama mkwe, mother-in-law)
    mama mkwe. mama aliyemzaa mke wako au mume wako.

Nasaba – Vizazi

Huu ni mpangilio wa watu wa ukoo mmoja kulingana na vizazi mbalimbali. Orodha hii imepangwa kulingana na mpangilio wa mzazi.

  1. babu mkuu, nyanya mkuu: (great grandparents)
    mzazi wa babu au nyanya yako
  2. babu, nyanya: (grandfather, grandmother) mzazi wa baba yako au mama yako
  3. mzazi: (parent) mtu aliyekuzaa.
  4. mwana: (child)
    mtoto wako.
  5. mjukuu: (grandchild)
    mtoto wa mtoto wako
  6. kitukuu: (great grandchild)
    mtoto wa mjukuu.
  7. kinying’ina: (great-great grandchild) mtoto wa kitukuu.
  8. kilembwe: (great-great-great grandchild) mtoto wa kinying’ina.
  9. kilembwekeza: (great-great-great-great grandchild) mtoto wa kilembwe.
  10. kitojo:(great-great-great-great-great grandchild)
    mtoto wa kilembwekeza.

Watu hao huwa na majukumu tofauti nyumbani kv

Mama hupika chakula nyumbani.

Dada hufagia nyumbani.

Kaka hukama ng’ombe.

Baba analipa Karo za shule.

SALAMU NA ADABU ZA KISWAHILI
Swahili greetings depend on the age of the participants, time of the day, and the context (formal or informal). Swahili greetings tend to be long and are usually initiated by the young persons to the older ones although the vice versa does happen.


Msamiati / Vocabulary
Habari (news) Nzuri, salama, safi, njema/fine

Habari za Juma, Alex, vicent News of Juma, Alex, Vicent

Asubuhi morning
Mchana day time
Jioni evening
Usiku night
Familia family
Baba dad
Mama mom
Kaka brother
Dada sister
Chuo university
Kazi job
Rafiki friend
Mbwa. dog
Paka cat
Nyumbani. home

Hujambo How are you?
Sijambo I am fine
Katongole hajambo How is katongole?
Katongole Hajambo katongole is fine
Doreen na shaimah hawajambo How are doreen and shaimah?
Hawajambo They are fine
Kwaheri Goodbye (1)
Kwaherini Goodbye all
Asanteni Thank you all.

Shikamoo
Shikamoo is a respectful greeting used by a young person to an older or superior person
Marahaba” is the Response of shikamoo.

Itwa called
Ninaitwa am called
jina langu ni My name is
Nina I have
Sina I do not have

Mambo?; Sasa?; Niaje?; Mambo vipi?; Vipi? Maneno?
What’s Up?

The reply for all that could be, Poa, freshi, safi, hakuna nk (cool)


Salamu : Hujambo.
Hujambo is one of the most common greetings in Swahili. It is usually used among agemates. However, if someone who is older than you greets you using hujambo, you respond to the greeting word normally and greet them back using an age appropriate greeting.


Mfano
Asha: Hujambo, Ali?
Ali: Sijambo, Asha. Na wewe je, hujambo?
Asha: (Mimi) sijambo.
Ali: Kaka hajambo?
Asha: (Yeye) hajambo. Je, dada hajambo?
Ali: Hajambo pia.
Asha: Kwaheri Ali.
Ali: Kwaheri Asha.


Kazi mradi I: Hujambo.
Katika makundi, jaribisha kusalimiana kwa kutumia hujambo
(In pairs, practice to greet in Swahili using hujambo)


Mfano .
Allen: Hamjambo Asha na Jamila?
Aisha na John: (Sisi) hatujambo Ali. Wewe hujambo?
Allen: (mimi) sijambo. Baba na mama hawajambo?
Aisha na John: (wao) hawajambo, asante. Je, dada zako hawajambo?
Allen: (wao) hawajambo. Kwaherini.
Aisha na John: Kwaheri, tutaonana baadaye.


Kazi mradi : Hamjambo?
Katika vikundi vyenu, tunga mazungmzo kwa kutumia salamu hamjambo.


Sarufi (Grammar): viwakilishi vya Kiswahili (Swahili Pronouns)
You may have noticed that the jambo greeting changes depending on how many people are involved. There are 3 personal pronouns that exist both in singular and plural. The pronouns are also marked in verbs to make them grammartical as shown below.


Kiwakilishi/Pronoun/ umoja-singular
Mimi /me or I
Wewe /you
Yeye /him or her

Pronoun and Verb itwa/called
Mimi ninaitwa Asha
Wewe unaitwa Ali
Yeye anaitwa Jamila


Pronoun/kiwakilishi/ Plural/wingi
Sisi/us or we
Nyinyi/ you all
Wao/they


Kiwakilishi na kitenzi “itwa”/Pronoun and Verb itwa/called
Sisi tunaitwa mbogo
Nyinyi mnaitwa kondoo
Wao wanaitwa sungura


Mfano .
Baraka: Hujambo rafiki?
Pili: Sijambo rafiki. Mimi ninaitwa Pili. Na wewe je, unaitwa nani?
Baraka: Mimi ninaitwa Baraka. Nimefurahi kukufahamu, Pili.
Pili: Nimefurahi kukufahamu pia, Baraka. Je, unasomea wapi?
Baraka: Mimi ninasomea Shule ya upili Bright Seeta. Na wewe je, unasomea wapi?
Pili: Mimi ninasomea shule ya upili ya seeta high.
Baraka: Kwaheri Pili.
Pili: Kwaheri Baraka.


Zoezi: Ninaitwa In pairs, greet each other and introduce yourselves in Swahili.


Salamu : Habari Gani?/What is the News?
The habari? habari gani? greeting is also a general form of greeting in Swahili. Just like with hujambo, it is mostly used among agemates. If an older person greets a younger person using the habari greeting, the younger person responds to the habari greeting normally and then greets the older person using the age appropriate greeting, shikamoo. The response to the habari greeting can either be nzuri, njema, salama, or safi, all which translate to fine or good. Just like with hujambo greeting, you can use the habari to inquire about the state of affairs of the person whom you are greeting such as work, school, family, e.t.c.


mfano .
Bahati: Habari gani rafiki yangu?
Musa: Salama rafiki, jina langu ni Musa; ninatoka lweza mukono.
Bahati: Mimi ninaitwa Bahati; ninatoka kamukuzi Mbarara. Habari za asubuhi?
Musa: Nzuri sana na wewe je?
Bahati: Safi. Habari za safari?
Musa: Njema. Nyumbani hawajambo?
Bahati: Hawajambo.
Musa: Karibu mukono.
Bahati: Asante.
Musa: Ninakutakia siku njema.
Bahati: Asante, ninakutakia siku njema pia.

Kazi mradi : Habari
In pairs, greet each other using habari/habari gani greeting, introduce yourselves, and bid each other goodbye.
How would you greet someone in Swahili using the habari greeting at the following times of the day?
Asubuhi
Mchana
Jioni
Usiku
How would you bid one goodbye in Swahili at the different times of the day shown below?
Asubuhi
Mchana
Jioni
Usiku

Salamu III: Hujambo?/Habari gani?/Shikamoo?

In this section, we shall learn how to use the shikamoo greeting together with hujambo and habari greeting words. Shikamoo is used by a young person to an adult, professor, or parent, public figure, president .

Mfano V: Mwanafunzi na Mwalimu.

Mwanafunzi: Shikamoo mwalimu Johnpaul.

Mwalimu: Marahaba. Hujambo victor?

Mwanfunzi: Sijambo, mwalimu. Habari za mchana mwalimu?

Mwalimu: Salama, asante. Nyumbani hawajambo?

Mwanafunzi: Hawajambo Mwalimu.

Mwalimu: Karibu kiti.

Mwanafunzi: Asante sana, mwalimu.

Mfano VI: Mwalimu na Wanafunzi.

Mwalimu: Hamjambo wanafunzi?

Wanafunzi: Hatujambo mwalimu, shikamoo?

Mwalimu: Marahaba. Habari za asubuhi?

Mwanafunzi I: Salama, asante.

Mwanafunzi II: Njema.

Mwanafunzi III: Nzuri sana.

Mwalimu: Karibuni ofisini.

Wanafunzi: Asante sana, mwalimu.

(baada ya mazungumzo/after the conversation)

Mwalimu: Kwaherini na muwe na siku njema.

Wanafunzi: Kwaheri na uwe na siku njema pia mwalimu Johnpaul.

Kazi mradi V: Kazi ya Vikundi

In pairs, rehearse how you will initiate a Swahili conversation with your director (mkurugenzi) during the office hour by using the age and time appropriate greetings.

Salamu IV: Mambo?,Mambo vipi?, Sasa?, Niaje?

These are informal greetings that Swahili speakers use in their informal interactions. These greetings are majorly used by the youth in the same age in their daily conversations. (salamu hizi zinatumiwa hasa na vijana wa rika moja)You can use any of the following greeting words in informal greetings: mambo? Mambo vipi? Sasa?, or Niaje? Jipya? Maneno?, all which translate to what’s up?/how is the going?,what’s new? The following responses are used interchangeably: poa, freshi, or fiti, safi, hakuna, all which translate to cool.

Mfano VII: Mazungumzo ya vijana

NISSI: Mambo vipi Tano?

GINUS: Freshi! Niaje tano?

NISSI: Poa sana. Za mchana?

GINUS: Safi! Mambo yanakwendaje huko dada?

NISSI: Salama na wewe je?

GINUS: Freshi! Baadaye Dada, kuna dilo pale.

NISSI: Baadaye pia bwana, kesho Tukutane huko?

GINUS: safi, usiku mwema dada?

NISSI: Na wewe pia dada.

Kazi mradi VI: Kazi ya Vikundi

Katika makundi, jaribisha salaamu zisizorasmi. (In pairs, practice to use informal Swahili greetings)

MAELEZO YA BAADHI YA SALAMU NA MAJIBU.

SALAMU (Greeting)JIBU (Response)
Hujambo? How are you?Sijambo. Am fine.
Hamjambo? How are you all?Hatujambo. We are all fine.
Sabalkheri? Good morning?Subalkheri/ alkheri.
Masalkheri? Good afternoon?Masalkheri/ alkheri.
Umeamkaje? How have you waken up?Salama. All is well.
Mmeamkaje?  How was your night?Salama. All was well.
Jambo. Hello?Jambo. Hello?
Habari gani? What is the news?Ni nzuri/ njema. Good.
Habari ya asubuhi? What is the news this morning?Sio mbaya? Not bad. Maana ni (nzuri)
Mambo vipi? Whatsup?Safi, poa, freshi. Cool.
ShikamooMarahaba
U hali gani? How are you?Njema, fine.
Mhali gani? How are you all?Nzuri we are all fine.
Usiku mwema? Good night?Na wewe pia. And you as well.

 MANENO YA ADABU (words of respect and manner)

Neno la adabuJibu
Hodi hodiKaribu. Welcome.
KwaheriKwaheri ya kuonana
HongeraAsante. Thank you.
Asante kwa kazikaribu
Uende salamaAsante sana.
Pole. Am sorry for your misfortune.Ni maisha. (its life). Asante.
Tafadhali? Please! “politely”Haidhuru.
Karibuni (welcome)Asante (thank you)
Tuonane (we meet each other)Nashukuru (I appreciate)
Samahani (excuse me)Naam (yes, excused)
Shikamoo. (please accep my respect)Marahaba.

Funzo h. Kusoma na kuigiza mazungumzo

Shughuli 10.

1 Kusoma na kuandika1.Katika jozi, someni na kuigiza mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali.

Tom : Habari ya siku nyingi rafiki?

Rehema : Ni nzuri, labda zako?

Tom : Mimi ni mzima. Umepotea sana siku hizi!

 Rehema : Ndiyo, mama yangu amekuwa mgonjwa.

Tom : Eee! Pole sana, sasa yuko vipi?

 Rehema : Tumempa dawa, atapata nafuu.

Tom : Hebu tuombe Mungu apone haraka

Rehema : Amina. Hebu niende nyumbani, Alamsiki!i.

Swali. Kwa kutumia kamusi, tafuteni maana ya maneno mapya kutokana na mazungumzo.

ii.Tambua na kuandika salamu na maneno ya adabu yaliyotumika katika mazungumzo.

Maneno ya adabu na unyenyekevu

  •  Tafadhali: Neno la heshima la kumwomba mtu afanye jambo kwa  niaba yako.
  •  Shikamoo: Salamu ya heshima itolewayo kwa mtu aliyekuzidi umri.
  •  Samahani: Neno la kuombea msamaha. Neno la kuomba upewe nafasi  au usikilizwe.
  •  Asante: Neno la kuonyesha shukrani kwa yale uliyotendewa.
  •  Ninasikitika:Neno la kuonyeshea hisia za huruma au kuionea hali ya  mtu huruma.
  •  Simile: Neno la adabu la kuomba kupishwa njia.
  •  Ashakum: Neno la kuombea msamha kabla ya kusema jambo  unalofikiria linaweza kumwudhi mtu anayekusikiliza.
  •  Mjamzito: Mwanamke aliyebeba mimba.
  •  Kujifungua:Kupata mtoto.
  •  Msalani/pembeni:Pahali pa kwendea haja.
  •  Pole: Neno la kumwonea mtu huruma au kumsikitikia kutokana na hali mbaya k.v. ugonjwa, kuumia n.k.

Mwenyezi maisha.

Unakubali au?

Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia. https://jifunzekiswahiliart.wordpress.com