HISTORIA YA NDOA ZA ANKOLE

Ndoa na Familia za Ankole.

Ndoa; Wakati wasichana walipotimiza miaka minane au tisa, haswa kati ya Bahima, maandalizi ya ndoa yakaanza.

Hawakuwa huru tena kukimbia na kucheza bila kudhibitiwa kwa namna moja au nyingine.

Wasichana walikuwa wakiwekwa ndani ya nyumba, ambapo walikula ugali wa mtama na nyama ya ng’ombe na pia walilazimishwa kunywa maziwa kwa wingi ili wanepe.

Kuwa mnene ulikuwa unahusishwa na uzuri/urembo, na kunywa maziwa kunasemekana kuchangia uzuri wa mtu kisura na kimwili.

Mara tu matiti ya msichana yalipoibuka, alionywa na wazazi wake kujiepusha na vitendo vya ngono ambavyo vinaweza kusababisha ujauzito na kudhalilisha familia.

Hapo zamani ujauzito nje ya ndoa uliadhibiwa kwa kifo au kufukuzwa nyumbani.

Baba wa Mnyankole mara kwa mara akisaidiwa na jamaa zake, alilazimika kupata mke wa mtoto wake kwa kulipa mahari/utajiri uliohitajika. Mahari/utajiri huu ulijumuisha ng’ombe wawili, mbuzi watatu, na vyungu kadhaa vya pombe kati ya Bairu.

Kati ya Bahima Iliweza kuwa wastaani ng’ombe wawili hadi ishirini, kulingana na jinsi mtu alivyotajirika.

Ndoa ziliweza kupangwa na wazazi wa wenzi hao au mvulana kupendekeza msichana wakati wa ujana.

Mara baada ya kulipwa mahari, maandalizi ya harusi huanza. Siku ya harusi baba ya bi-harusi anamchinja ng’ombe dume (bull) kwa chakula. Aina nyingine za vyakula na kiasi kikubwa cha pombe viliandaliwa kwa ajili ya karamu nyumbani kwa bi-harusi.

Hii inafuatiwa na karamu nyingine nyumbani kwa bwana harusi ambapo ndoa inakamilikia.

Katika sherehe za harusi shangazi ya msichana huyo alitakiwa kuthibitisha kuwa bwana harusi ana nguvu za kitanda na kuhakikisha kuwa bi-harusi alitetea ubikira (virginity) wake kabla ya ndoa kukamilika.

Wakati wa sherehe ya harusi, msichana angeandamana na miongoni mwa wengine shangazi yake kufanikisha mila hizo. 
Baadhi ya mila hudai kwamba mume angeingia mapenzi/ngono kwanza na shangazi kabla ya kuendelea kufanya mapenzi na bi-harusi. 
Hadithi nyingine inasema kwamba jukumu la shangazi lilikuwa kuthibitisha uwezo wa bwana harusi kwa kutazama tu au kusikiliza ngono kati ya bwana harusi na mpwa wake. Inasemekana kuwa jukumu lake lilikuwa kumshauri msichana huyo jinsi ya kuanza ndoa kwani Ankole, wasichana walipaswa kuwa na ubikira hadi kuolewa kirasmi. 
Tamaduni hizi za kwanza maswali yanabaki kunichukiza kwasababu mara nyingi shangazi angekuwa mwanamke mzee karibu umri sawa na mama wa bwana harusi, sasa ingefanyikaje kulala na mvulana kijana wa miaka changa hiyo-pamoja na nguvu zake! Hivyo kando, tamaduni na mila nyingine zilishikilia kwamba, Ikiwa wazazi wa msichana walijua kwamba binti yao hakuwa na ubikira, habari hii ilikuwa inawasilishwa kwa mume kabla kwa kukabidhiwa msichana. 
Kati ya zawadi nyingine zikiwemo sarafu iliyotoboleka au kitu kingine kilicho na kashimo ndanicho vingetolewa.
 

Tofauti ya kijamii kati ya Bahima na Bairu ilianzishwa kwa kuzuia kuoana kati yao. Bahima wangeona ni chukizo kuoa Mwiru.

Sio hivyo tu bali, ilikuwa ni kinyume cha sheria kwa Muhima kumpa Mwiru ng’ombe. Wanaume wa sehemu ya Bairu hawakuwa na ng’ombe wa kutoa mahari kuoa mke wa Muhima kwani kile tu walikuwa nacho ni ng’ombe wasio na tija na ndama wa ng’ombe dume (bull calves). Ng’ombe walikuwa muhimu sio tu kwa uhalali wa ndoa lakini pia kwa uhalali wa watoto waliozaliwa nje ya uhusiano wa ndoa.

Mwanamke asiye na watoto hana hadhi yoyote kati ya Banyankole, na wanawake wengi walipenda/wanapenda kuolewa na kuzaa watoto wengi.

Ikiwa mwanamke hawezi kuzaa watoto, mumewe anaweza kufikiria kuchukua mke wa pili. kuoa mke mmoja ulikuwa ukawaida ingawa kuoa zaidi ya mmoja halikukatazwa.

Mfalme wa Ankole (Mugabe) na tajiri Banyankole walikuwa wanahusiana sana na mitala/kuoa mke zaidi ya mmoja. Leo ndoa ya mke mmoja inabaki kuwa njia kuu ya ndoa iliyoathiriwa na nchi za Magharibi, Ukristo, elimu, na mitindo ya jadi ya Banyankole.

Leave a comment