BAHORORO UNAWATAMBUA!
Wahororo au Bahororo ni kabila linalozungumza lugha za Kibantu ambao wanaishi hasa kaskazini mwa iliyokuwa Wilaya ya Kigezi kusini-magharibi mwa Uganda.
Mnamo 1905, walielezewa na afisa mmoja wa Uingereza kama ” watu watulivu, wasiokera” waliokuwa wamiliki was ng’ombe.
Wahororo Wanaundwa zaidi na kabila la Bahima na kabila la Bairu .
Wanaishi hasa kusini-magharibi mwa Uganda na wanahusiana na watu Banyankole, Banyoro, Batooro, Basongora na Watutsi.
Bahororo wanazungumza lahaja ya Runyankore-Rukiga/Ruhororo .
Wamegawanywa katika koo zinazofanana na zile za ufalme wa Ankole.
Tofauti na Ankole, ambayo ilitawaliwa na ukoo wa Bahinda , Bahororo waliongozwa na ukoo wa Bashambo.
la tafakari ✍️🤷♂️

