SARUFI FAFANUZI.

Sarufi fafanuzi inakusudi kutoa maelezo yasiyo ya hukumu ya muundo wa kisarufi ya  lugha fulani. Ni uchunguzi wa jinsi lugha inavyotumika, kwa maandishi na kwa usemi/mazungmzo. 

Wanaisimu ambao wamebobea katika sarufi fafanuzi huchunguza kanuni na mifumo ambayo inategemea matumizi ya maneno, vishazi, virai, na sentensi.
Kwa maana hiyo, kivumishi "fafanuzi" ni cha kupotosha kidogo kwani sarufi fafanuzi hutoa uchambuzi na ufafanuzi wa sarufi ya lugha, sio ufafanuzi tu.

Sarufi fafanuzi haitoi ushauri bali inaelezea kwa kina njia au kanuni ambazo wasemaji wa asili/ wazaawa hutumia katika lugha yao. 

Sarufi fafanuzi ni uchunguzi wa lugha kwa undani na matumizi yake.
Kwa lugha yoyote hai, sarufi fafanuzi kutoka karne moja itatofautiana na sarufi fafanuzi ya karne ijayo kwa sababu lugha itakuwa imeishabadilika.

Mfano katika ya kinyankore-kikiga  ya karne ya kumi inatofautiana na hii inayotumiwa katika karne hii ya ishirini ( 20th century). Mfano neno “taata” maana yake ikiwa mzazi wa kiume limebadilika kuwa “muzeeyi” katika karne za hivi karibuni.

Kwaufupi sarufi fafanuzi ni sarufi matumizi.

Sarufi fafanuzi ni seti ya sheria na kanuni kuhusu lugha kulingana na jinsi inavyotumika. Katika sarufi fafanuzi hakuna lugha sahihi au mbaya.Inaweza kulinganishwa na sarufi ya maagizo, ambayo ni seti ya sheria au kanuni kulingana na jinsi watu wanafikiria lugha inapaswa kutumiwa.

Kama ilivyoelezewa hapo juu, sarufi fafanuzi inajaribu kuelezea matumizi ya lugha kulingana wazungumzaji wa asili ya lugha hiyo. 

Sarufi fafanuzi inadokeza kwamba mamlaka pekee ya kile kilichopo katika lugha ni kile wasemaji wake wa asili wanakubali na kuelewa kama sehemu ya lugha yao. Kwamfano katika lugha ya kinyankore- kikiga tunakubali kwamba neno “empunu” maana yake ni nguruwe na ni hivyo hivyo tu isipokuwa labda neno limekatazwa na wanyankore kutolitumia kwa maana hiyo. Lakini kila mzungmzaji atakuwa anaelewa kuwa “empunu” ni nomino yenye maana ya nguruwe.

Kwa kuhitimishwa suala la isimu fafanuzi, ikumbukwe kwamba isimu fafanuzi ya lugha hubadilika wakati baada ya mwingine na pia isimu fafanuzi ya lugha moja ni toafauti na ya lugha nyingine kwa kutegemea watumiaji lugha hiyo.






arigumaho810@gmail.com.




Leave a comment